Nashindwa kumweleza ukweli

Nashindwa kumweleza ukweli

HAONI

Member
Joined
Jan 30, 2012
Posts
8
Reaction score
0
Wife alipokuwa mjamzito aliniomba tukapime VVU. Nilimchenga chenga kidogo lakini hatimaye niliamua kwenda nje ya mji kupima peke yangu kabla sijaambatana nae. Baada ya counseling ya docta alinielekeza chumba cha kupimia. Nilipoingia ndani nilikutana na mtu wa vipimo ambaye ni rafiki na mke wangu na alishawahi kututembelea home. Nikuwahi kujua sehemu anayofanyia kazi. Alinipokea vizuar na kuchukua damu yangu na kuniomba nisubiri nje kidogo. Nilishangaa kidogo na kupatwa na hofu kwani majibu yangu yalichukuwa zaidi ya nusu saa kuyapata (kwa kawaida huwa inachukua not more than ten mts).
Majibu hayakuwa mazuri (nilionekana nina maambukizi),
1) sijawahi kumweleza mke wangu na huu ni mwezi wa tatu tangu kupata majibu
2) yule dada aliyenitoa damu na kufanya vipimo ameongeza safari za kuja kukutembelea home (kila weekend)
3) sina hakika kama keshamweleza mke wangu status yangu (wife hajaonyesha tofauti yoyote)

naomba ushauri wenu wadau
 
Ushauri upi sasa unataka; ukishajitabua chukua hatua tu.
 
Mkuu hilo ni zito!kama unaweza kupima tena pengine fanya hivyo.nshauri pia ukae chini uongee na huyo mpimaji ambaye pia ni family friend muone mnafanyaje,.afu wakati huo jaribu kutafuta namana sahihi ya kumlinda mkeo dhidi ya maambukizi.
 
heee,im sorry nimeshangaa kwa sauti,pole aisee, hii ngumu,ni mtoto wenu wa ngapi huyo aliyepo kwenye ikulu ya uzazi,kama ni wa kwanza nendeni mkapime wote hapo ndio iwe kupasua jipu,ni ngumu lakini hakuna ujanja maana kupima mama mtarajiwa ni lazima siku hizi.
 
Duh hapa ni pagumu sana sana na Jipe moyo kwanza kwa hali yako. Mpimaji naamini atatunza siri za mgonjwa wake ila kabla hajamwambia mkeo ni bora mchukuane nae mkapime na hilo lipasukie pale pale kuliko aje apaet habari kama hizo kwa mtu wa tatu
Jipe moyo na naamini kwa nguvu za Mungu inaweza kutokea mtoto akazaliwa bila maambukizi na mkaendelea na maisha na kama mama hajaathirika ni bora zaidi kwa upande wa mtoto. Jitunze na mtunze mkeo kwa sasa japo najua huwezi kuanza tuu from nowhere umwambie tuanze kutumia kinga ndo maana nasisitiza mkapime wote wawili ili kama ni kuanza kutumia kinga uanze nazo
 
Nakushauri ukapime tena sehemu nyingine na kama majibu ni hayo hayo.Inabidi umkalishe chini mkeo umueleze ukweli...IT WILL BE WORSE WHEN SHE HEARS IT FROM SOMEONE ELSE AND NOT YOU...Na inabidi na yeye apimwe lakini nadhani kawaida mjamzito yoyote lazima apimwe ukimwi...Dah hebu nikulaumu kwanza..WHAT THE HECK WERE YOU THINKIN MAN??
​
 
sidhan kama unastahli kulaumiwa wala mtu kukushangaa. ishatokea na huwezi kurudisha muda nyuma, cha msingi kwanza kabisa acha kuendelea kula tunda na mkeo (ikilazmu tumia kondom hadi hapo utapojrdhsha na hali zenu wote, nenda kapime tena sehem nyngne hata mbili tofauti kama majibu ni hayo hayo nenda kapime na mkeo kama itatokea hana hewala kama anao ishini pamoja kwa upendo na Mungu atawaongoza.
 
Kama kweli mkeo ni mjamzito nina uhakika anajua hali yake...hivyo hata hali yako anaifahamu.

Suala la yeye kukuomba kwenda kupima nahisi alitaka kujiridhisha au alitaka nyote mtambue hali zenu kwa pamoja.

Mkuu watu8 haya mambo hata kuyafikiria ni magumu sana na yanauma sana
Iwapo mkewe anajijua hali yake imagine maumivu anayoyapata kwanza kujifikiria hali yake ya ugonjwa na kiumbe wake na maisha yake baada ya kujifungua na maisha ya mtoto(watoto) kama anao wengine ni ngumu sana
haya mambo yasikie kwa wengine yasitokee kwenye familia yako.
Na hapa inaonekana jamaa aliupata huko nje kwenye nyumba zake ndogo maana haionekani kama walikuwa nao wakati wanaoana na ndo maana inamtisha na kumuogopesha huyu jamaa kwenda kupima
 
Last edited by a moderator:
cha msingi kwanza kabisa acha kuendelea kula tunda na mkeo (ikilazmu tumia kondom hadi hapo utapojrdhsha na hali zenu wote,

Mkuu yaani out of nowhere aanze tu kutumia kondomu mind mkewe ni mjamzito....sasa hiyo kondomu sijui mkewe akiuliza kwa nini yavaliwa jamaa atajibu nini...

Suala la muhimu ni huyu jamaa kwa kuwa anajua hali yake, akae chini na mkewe na kumueleza. Kuwa na HIV sio ndio kwamba u marehemu...kila mtu ataonja mauti ni vile hakuna ajuaye ni namna gani roho yake itavyochukuliwa.
 
ni vyema ukaenda na mkeo kupima

Then mtajia jinsi ya kumkinga mtoto na kuepuka maamhukizi mapya

Na mkiwa wawili mtalikabili hilo tatizo vyema pamoja na kuzuia huyo anayejifanya nyumbani kwako anapajua saaaana
 
Kama kweli mkeo ni mjamzito nina uhakika anajua hali yake...hivyo hata hali yako anaifahamu.

Suala la yeye kukuomba kwenda kupima nahisi alitaka kujiridhisha au alitaka nyote mtambue hali zenu kwa pamoja.

ni kweli...labda tumuulize mimba ya mama imefikisha umri wa kwwenda kliniki?usikute jamaa anapata wakati mgumu bure kumbe wife ameshajua zamani anawaza amweleze vipi...wanawake ni wazuri sana kuficha siri...

swali jingine..uyo rafiki wa familia/mkeo ana historia gani na nyie?walisoma wote au?au wamejuana tu kiaina aina..usikute walujuana hapo hapo....btw maisha lazima yaendelee.....fanya haraka mama aanze program ya PMTCT ya kumkinga mtoto
 
Mhh kazi kweli kweli............

Dunia ina mambo hii hadi mwili umenisisimka.........
 
1) sijawahi kumweleza mke wangu na huu ni mwezi wa tatu tangu kupata majibu
2) yule dada aliyenitoa damu na kufanya vipimo ameongeza safari za kuja kukutembelea home (kila weekend)
3) sina hakika kama keshamweleza mke wangu status yangu (wife hajaonyesha tofauti yoyote)

naomba ushauri wenu wadau

Huyo rafiki wa mkeo ambaye ni mhudumu wa afya kimaadili 'hapaswi' kumweleza mkeo. Ni kosa la kimaadili na la jinai kwa mhudumu wa afya kutoa siri ya client wake..anashtakiwa mahakamani na anafungwa/futiwa leseni/kupigwa faini..hata angekuwa dada yake.

BUT...tafadhali mueleze mkeo wewe mwenyewe, anahitaji kujua ili naye akapime ajue ameambukizwa au la. Pia mfikirie mtoto ambaye mkeo amembeba tumboni, unaweza kumuokoa kwani siku hizi kuna njia za kuzuia maambukizi toka kwa mama muathirika (kama mkeo naye atakuwa ameathirika) kwenda kwa mtoto. Hivyo mkazaa mtoto hasiyekuwa na maambukizi. Kwa kuficha kutomuambia mkeo atakosa hiyo huduma, mtoto wenu atazaliwa na maambukizi..tafadhali pata moyo wa kuzuia hilo..

Unaweza kuwa umemuambukiza mkeo bila hatia...zuia kumuambukiza tena malaika wa mungu bila hatia!

Mweleze mkeo, nendeni hospitali mpate msaada husika.
 
Kama kweli mkeo ni mjamzito nina uhakika anajua hali yake...hivyo hata hali yako anaifahamu.

Suala la yeye kukuomba kwenda kupima nahisi alitaka kujiridhisha au alitaka nyote mtambue hali zenu kwa pamoja.

Mtu akiwa na Mimba si huwa inashauriwa aende wewe na mwenza wako kupima........

Labda ndio maana alikuwa anamsisitiza waende!!!!!nachojiuliza ni hiyo miezi 3 si lazima ali DO

na mkewe tu.............
 
Wewe kweli huoni....sasa unataka kipi cha kushauriwa, hapa ni kumwelezao mkeo na kama wote mmepata maambukizo muanze maisha mapya ya kujaliana na kuzingatia lishe bora. Ila mkuu huo ni mtihani.
 
jikaze moyo umwambie,inawezekana yeye anajijua kama yuko +ve au hapana,pia inawezekana yeye anao ama hana!!
 
pole sana
ongea na mkeo
n nijuavyo wajawazito huwa wanapima HIV mapema tu
wengine huwa wanakua HIV -ve huku wenza wao wanakua HIV +ve Mentor njoo huku
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom