Nashindwa kumweleza ukweli

Nashindwa kumweleza ukweli

haya mambo ya ujauzito na vvu au ukimwi noma nilimpoteza dadangu hivihivi kidonda hakijapona.Kila akienda hospital anaambiwa apime harudi hospital ile tena clinic ya mtoto haendi kwenye kuzaa akaenda private sijui alihonga akazaa mtoto kinga hana kitoto kikafariki na yeye kuanza kuumwa hapo ndo tukakamata mchuma fasta kumfata alipo na kumpeleka hospital akaanza dawa na tukambeba kuja nae dar.Akasimama na nguvu akapata akarudi kama zamani.Akarudi mkoa anaokaa sijui ibilisi gani aliyemkumba na wakati dawa zinachululiwa dar mi mwenyewe namtumia na kuna dawa za asili za burundi alikuwa anatumiwa akaacha kumeza dawa sie kuja kupata taarifa kaacha na kuanza kuumwa ndani ya wiki kakonda,kavurugika,kukamata mchuma fasta kumfata mkoa i mi na ndugu yangu mwingine ili kumuangalia apate nafuu turudi nae dar ila haikuwa ridhiki baada ya wiki moja ya kuhangaika kumuokoa akaondoka. HAONI mchukue mkeo haraka sana mkapime hata kama kapima anahitaji support yako sana haijalishi kama majibu positive au negative ila anakuhutaji sana kipindi hiki

pole sana amu
 
Last edited by a moderator:
Mkuu kapime hata kwa siri kujua status ya wife usije ukawa unamuua wakati ni mzima na siku hizi watoto tumboni hawapati vvu mradi mama aendelee na dawa muda wote wa uja uzito na baada ya kujifungua anyonyeshe mtoto kwa miezi sita mfururizo bila kumpa chakula kingine. Msirikishe mwenzio mjenge familia bora.
 
Kama kweli mkeo ni mjamzito nina uhakika anajua hali yake...hivyo hata hali yako anaifahamu.

Suala la yeye kukuomba kwenda kupima nahisi alitaka kujiridhisha au alitaka nyote mtambue hali zenu kwa pamoja.

Na njia pekee ni kukubali ombi la kwenda kupimwa wote halafu itaanzia hapo
 
Dah pole sana mkuu, Nakushauri uende ukapime tena then kaa na mkeo mweleze ukweli ili kama yeye atakua na status tofauti na wewe umlinde yeye pamoja na baby wenu alie tumboni na kama huwezi kumweleza mshirikishe huyo family friend wenu ambaye tayari anajua status yako ili akusaidie katika kumshauri mkeo. Mweleze kabla hajayapata kwa watu. Be a man in front of her.
 
Dah pole sana ila haimaanishi utakufa kesho,lakini me nahisi kama mkeo kashapima na inawezekana nae yupo na status kama yako na kashndwa kukwambia alitaka mwende wote mkapate majibu kwa pamoja,na kama kapima hajakwambia hii.itamaanisha nae alikua hajatulia hvyo hawezi kukushtumu kua umeleta ugonjwa maana inawezekana ye ndo kaleta.
Haujawah kuona card yake ya clinic au bado hajaanza kwenda?
Unaweza ukakaa chini ukaongea nae na mkaenda wote kupima huo c mwishowa maisha rafiki.
 
Jana nimetoka kupima, aisee ile ni kazi nzito sana. Asikwambie mtu. Napata picha how you feel man, sorry sana. Kapime tena kuhakiki, kama ni kweli nenda ukamweleze mkeo.
 
kweli kabisa.ni heri kuoa huo nao ni wito
kama ulivo wito wangu
Paul akasema, "lakini kwa habari ya zinaa ni heri kuoa." Lakini amri yangu si sheria ingawa hakunaga watawa warembo ka ww
 
Back
Top Bottom