Kama kiongozi wa shughuli za kiserikali bungeni na kama kiongozi katika baraza la mawaziri na vilevile mtendaji mkuu wa serikali sioni sababu ya yeye kuendelea kuwepo katika hiyo nafasi wakati hakuna ata kimoja kipya alichokifanya. Mh Pinda hana maamuzi kama waziri mkuu,hajawahi kusema lolote ata pale inapobidi anasema ningekuwa na mamlaka ningefanya. Kama hana mamlaka anafanya nini basi? Ajiuzulu tujue Tanzania haina waziri mkuu. Wanatufanya wajinga, wanatukebehi bila hururma, wanakula jasho letu bure. Ifike mahali tuwatoe kwenye magari watembee kwa miguu maana hakuna wanachofanya.