Kama kiongozi wa shughuli za kiserikali bungeni na kama kiongozi katika baraza la mawaziri na vilevile mtendaji mkuu wa serikali sioni sababu ya yeye kuendelea kuwepo katika hiyo nafasi wakati hakuna ata kimoja kipya alichokifanya. Mh Pinda hana maamuzi kama waziri mkuu,hajawahi kusema lolote ata pale inapobidi anasema ningekuwa na mamlaka ningefanya. Kama hana mamlaka anafanya nini basi? Ajiuzulu tujue Tanzania haina waziri mkuu. Wanatufanya wajinga, wanatukebehi bila hururma, wanakula jasho letu bure. Ifike mahali tuwatoe kwenye magari watembee kwa miguu maana hakuna wanachofanya.
Mchango wa Great Thinker huo!! Ha ha ha haaa...!!!!.Hii tumu ya kutetea makengeza ya serikkali, nikiitizama kwa jicho la ndani kabisa naona ina ilmu ya chuo kikuu cha madrasa. Naipongeza kwa usomi wa ilmu ya juu kabisa na umakini wa kujibu kila hoja kwa mtizamo elekezi..
Mkuu,nakubaliana na ww 100%,kwamba kupitia huyu Pinda nafasi ya Primier imeonekana kama haina maana yyte.Unaweza pia kurejea suala la spika wa bunge kujitwisha jukumu la kumjibia maswali katika vikao mbali mbali vya bunge hivi karibuni,pinda asijue kwamba an udhalilisha u PM,badala yake yye anafikiri anasaidiwa!.Au kwa vile meijaza nafasi ya aliye kuwa bosi wake(EL),anaona hayuko huru(he wasn't JK's first choice!)Nakubaliana na mtoa mada hii na nilitarajia Pinda ampe Rais 'live' kwamba; ama Jairo abakie kwenye serikali yake au yeye Pinda, lakini wote wawili hawawezi kubakia serikali. Haiwezekani. Ukitafakari kauli aliyotoa Pinda baada ya kikao cha CCM bungeni last week ni wazi kuwa alikuwa ameridhika Jairo amekiuka 'kanuni' za utawala bora na hivyo alihitaji tu kum-consult Rais ili hatua za kinidhamu zichukuliwe.
Lakini kama kuna mtu amesoma Tanzania Daima ya leo 22/07/11 kauli aliyotoa Katibu mkuu kiongozi Philemon Luhanjo ni kama yeye katibu mkuu ana mamlaka ya kumchukulia hatua Jairo. Luhanjo anasema amenukuliwa akisema hivi Nimeona niwaambie hili ili tusiendelee kuwaambia wananchi tunamsubiri Rais, wakati mimi mwenye dhamana ya kusimamia nidhamu nipo hapa, nimeshachukua hatua".
Luhanjo anaendelea Kutokana na uzito wa jambo hili, nimelazimika kumwamuru CAG, Ludovick Utuoh, kufanya uchunguzi ndani ya siku 10 na iwapo itabainika kuwa ana kosa, hatua nyingine za kisheria zitafuata .
Sasa tujuilize:
1. Katibu mkuu kiongozi ana mamlaka kumshinda Waziri mkuu wa Nchi?
2. Katibu mkuu kiongozi ana mamlaka kumshinda makamu wa rais ambaye kikatiba ndiye aliyekuwa anakaimu kiti cha urais wakati rais yupo nje ya nchi?
3. Kama Katibu mkuu kiongozi ndiye mtu mwenye mamlaka kwa nini Pinda akapeleka mashauri kwa Rais na sio kwa Katibu mkuu kiongozi?
It is unbelieavable that Katibu mkuu kiongozi anaonekana kuendesha nchi wakati kikatiba Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Spika wa Bunge ndio wako kwenye safu ya kuongoza kama Rais hayupo. Kama Pinda atanyamazia hili (inaonekana kuwa hivyo) akae akijua mawili:
1. Mbele ya watanzania ataonekana mtua asiyekuwa na mamlaka yeyote, asiyejuwa nini kinaendelea na asiyesimamia chochote!
2. Kubwa zaidi, nafasi ya u-waziri mkuu kama kiongozi wa shughuli za serikali inakuwa -obsolete'. na watanzania watakuwa na kila sababu/haki ya kudai nafasi hii ifutwe ili kuondokana na gharama zisizo za lazima maana nafasi ya Katibu mkuu kiongozi inatosheleza! Afte all the person who took action ni Katibu mkuu kiongozi. Prime Minister's office can go.
Kujiuzulu siyo solution ya matatizo yaliyopo