Pole sana umenikumbusha mbali sana,nakumbuka nilikuwa na rafiki mmoja a wakati huo alikuwa kama na miaka 33,hana mume wala mtoto,kuona umri unamtupa mkono sababu hata waliokuwa wanampa mambo ikawa shikamo dada,mara ghafla nakutongozwa na maneno kama nakupenda yakapungua,ghafla akajikuta anahitaji mtoto kwa khali na mali,mimba akapata mwisho wa siku akajifungua baada ya wiki moja akafa mtoto akabaki,na mbaya zaidi hata baba wa mtoto aliingia mitini ni kama vile alimlazimisha wazae ingawa inaoneka jamaa hakutaka kabisa,toka dada ana mimba mpaka anakufa jamaa hakutokea kabisa ikabidi siku za kliniki unavaa uhusika sababu tulikuwa tunaheshimiana mno,ushauri wangu kwako usilazimishe vitu unaweza pata hitaji la moyo wako kwa gharama kubwa,yote mkabidhi Mungu
Kuna watu wameolewa lakini hawana vizazi,kuna watu hawajaolewa lakini wana watoto,kuna watu hawajaolewa na pia niwagumba,Mungu ndiye hutoa yote,lakini pole sana
Sent using
Jamii Forums mobile app