Napitia katika changamoto kubwa

Napitia katika changamoto kubwa

Wizzy mimi ndoa nimepata,nina mtoto ila mleta mada namuonea huruma na atakavyopata shida humu
 
Pole sana dada, lakini mbona bado unamuda wa kutosha usichanganyikiwe namna hiyo kwasababu haya mambo yanataka uangalifu mdogo wangu. Be very careful

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nitashukuru. Yaani pamoja na unyago wa kwetu hayo ulompa m-dada mi sikuambiwa

Sent using Jamii Forums mobile app


Ndiyo uzuri wa JF utakutana na wanaume wafundaji.

kunamambo mtu anayoona madogo ila yanaweza kubadili maisha yake ya Mahusiano.

Utani Cc ukianzisha uzi basi nije nimwage wino.
 
Mie in a serious means nataka mtoto kabisa.Kama upo tayari tuwasiliane na utapata bila masharti yoyote.Atakuwa wako tu,na pia sijaoa na sina mpango wa kuoa.Am very serious about this,if you wish you can decide.Am old enough na ninazalisha vzr tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habari za jumapili wana jamii.
Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 32 kwa sasa. Napitia katika changamoto kubwa sana.
Hapo mwanzo kipindi ninasoma niliona si vyema kujiingiza katika mahusiano ya kufanya mapenzi kwani niliona yatanivuruga na ningejikuta napitia katika mahusiano mengi kitu ambacho sijawahi kukipanga maishani.
Nikamaliza chuo vizuri namshukuru Mungu.katika kutafuta ilikuwa ngumu kidogo nilitafuta mpaka nikakata tamaa nikaomba Mungu mpaka nikaona inatosha. Katikati ya kukata tamaa nikamuomba Mungu basi anipe kitu kimoja kwanza mme au kazi. Ila la kazi ndio nililoliwekea msisitizo kwani kwa kipindi hicho familia yangu ilikuwa inapitia changamoto nyingi kwa hiyo nikaona kazi itanisaidia kupunguza changamoto ama la basi niolewe ili nipunguze mzigo kwa familia yangu.
Siku isiyotarajiwa nikaitwa interview na nikapata kazi nzuri ambayo sikuwahi hata kufikiria wala kuiwaza.
Nikashukuru Mungu na kuanza maisha mapya ya kazi na kusaidia familia yangu. Nikajikita kwenye kumuomba Mungu anijalie mme mwema atakayenifaa na kuongoza familia tutakayoipata katika misingi ya imani ta dini ya kikristo. Sikubagua kabila wala atakuwa mkirsto wa aina gani maadamu awe anaabudu jumapili maana mimi nilikuwa tiari kuhama katoliki ili tulee familia yetu tukiwa na muongozo wa dini moja.

Sikuwahi kudhani nitafikia huku maana mpaka sasa imekuwa ngumu kama ni Mungu hachelewi ama hawahi basi kwangu mimi kwa sasa imekuwa ni shida kubwa. Nimefunga novena nimesali sana mpaka naona nimeanza kuathilika nahili swala. Mwaka jana tarehe moja nikaona basi kama mme wangu hayupo nipate tu mwanamme nitakae zaa nae lakini awe mkirsto maana siko tiari kumtenga baba na mtoto wake hata kama hamhudumii, nikiamini kuwa uwezo wa kulea mwenyewe ninao hata kama watoto watakuwa zaidi ya mmoja niko tiari kupambana na maisha. Nikaona kwa sababu nitakuwa pekeangu nikaanza kuwekeza ili watoto wangu wanikute nimejiandaa. Na penyewe Mungu akaona wakati wangu bado.
Mwaka huu mwezi wa pili akatokea mme wa mtu kitu ambacho sijawahi hata fikiria kuwa kunasiku nitaangukia huko, Mwanzoni nilitaka tuzungumze mapema kabla hatujazoena sana matakwa yangu lakini akawa mtu wa kuona nampangia sheria mapema na kudai hizo mipango ninazotaka kupanga nae tukiwa hatujafika mbali ni mipango gani. Nikaona isiwe tabu.
Ikafika siku ya kukutana nikamwambia mimi sijawahi kabisa hakuamini na nikamwambia kama anajiamini aendelee ila ajue atakuwa na deni la kulipa, akatafakari akaona viatu ni vikubwa akaondoka.

Chenga zikaongezeka nikajiuliza ni nini shida, tukapanga tukutane ili tuone hatima ni nini kati yetu. Akaja na kudai yeye hayuko tiari kutoa bikira ya mtu asiye na mpango nae. nikamuelewa na nikaona yuko sahihi.Nikamuuliza wewe ulivyoanza ulitegemea mimi ni mti sina hisia za kufanya mapenzi akadai alijua anajihusisha na mapenzi ya kila mtu ana mtu wake hivyo wanakutana kulizishana tu. Akaniambia nahitaji nini hasa kwake nikamwambia kama ulishaona hisia zangu unadhani nahitaji nini? Niliona nisianze kutaja shida niliyonayo kwanza nimsikilize yeye ndio na mimi niseme ya kwangu. Yeye akadai aliona ni mahusiano ya kula na kuondoka. Akaniambia kama niko tiari ataweka sheria za kutuongoza za maandishi ili baadae tusijekupeana shida. Nikamwambia sheria zako utazoniwekea nitazifuata vilivyo japo najijua ninawivu lakini wewe ni mme wa mtu tiari nitavumilia. Akaja na sheria na mipango mingi sana asee.sheria nyingi nilivyotafakari nikaona nyingi zinamlenga mtoto ambaye mimi ndio ninayemhitaji zaidi. na yeye akaona labda ni mmoja tu wakati mimi nishajipangia wakunitosha kabisa. Kwa maelezo yake nikaona hayuko tiari kuwa na mtoto nje ya familia na nikitokea kumpata basi nitoe mimba ama atamchukua. Nilichoka viungo vyote. Akaniuliza unalolote nikamwambia nizungumze nini wakati sheria zimekuwa ngumu.

Haki ya Mungu yaani natamani siku zirudi nyuma nizunguke na wanaume kama wafanyavyo wengine. Hukukujitunza kwangu kunanifanya nilie kila siku na kuomba Mungu usiku kucha kisa nilimtunzia mtu bikira. Jamii inayonizunguka itanitia wazimu maana swali la unaolewa lini limenichosha kabisa. Basi kama siolewi hata mtoto tu ni shida kumpata.

Kwasasa ninashida na mtoto kuliko maelezo na niendako nadhani nitawehuka. Msaada wenu tafadhalini sana.

NB. Hapo mwanzo nilifunga novena kwa muda wa mwaka mmoja na kuomba na kukabidhi mwili wangu uwe kwa ajili ya mtu mmoja tu ambaye ndio atakayekuwa mme au baba wa watoto wangu. Ndio maana inaniwia vigumu kuingia mahusiano mbalimbali.
Nipo tayari kukupa mtoto,Ila Kwa kupima afya Kwanza.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usipaniki mydya tulia
Na uskate tamaa wala kuutesa mwili wako kuna muda tunapitishwa vpnd vgumu ili tupimwe imani zetu na uwezo wetu wa kumwamini Mungu
Nakushauri kabsaa I'm nt 30's but out of experience ucjelogwa kudate na mume wa mtu hao watu ni washenz utajutia maisha yako yote malengo yao wanapanga na wake zao ww ungekua sex machine tu
So do this relax and wait but sali Mungu wetu ni mwaminifu anajibu vzur kabsaa na kwa wakati sahh
Utaulzwa unaolewa lini sababu ni kawaoda kwa jamii yetu bnt ukimalza shule uolewe so its ok kwao kuulza na kukusema pia usiogope kabsaa! Relax and do your thing mpnz if you nid a friend to talk to nipm ntakua best yako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana... miaka 32 bado una bikra... kwa maana hata masturbation hufanyi? Utakua na matatizo...

Anyways... why uzae na mume wa mtu? Usiwe desperate, tafuta unmarried mwenzako muanzishe mahusiano...

Tabu hutoipata wewe, bali mwanao huko mbeleni...


Cc: mahondaw
 
Pole sana... miaka 32 bado una bikra... kwa maana hata masturbation hufanyi? Utakua na matatizo...

Anyways... why uzae na mume wa mtu? Usiwe desperate, tafuta unmarried mwenzako muanzishe mahusiano...

Tabu hutoipata wewe, bali mwanao huko mbeleni...


Cc: mahondaw

kweli kabisa love
 
Pole, sisi tunaoamini ktk Maandiko matakatifu (Bible) inatuambia kila jambo lina wakati wake, upo wakati wa kulima pia upo wakati wa kuvuna, amini wakati wako unakuja na SAA yako itafika. Kosea yote lakini sio kuoa/kuolewa, TAFAKARI CHUKUA HATUA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu dada leo sijui kapata pm ngapi, bikra jamani inawazuzua.
 
Back
Top Bottom