Napingana na wanaosema Afya ya Rais si siri

Nimpongeze Mhe. Rais kwa kuamua kukaa chini na kufanya kazi za ofisi ikiwemo kuhakikisha mambo nyeti yaliyokuwa yanasimamiwa na Marehemu Balozi Kijazi yanakabidhiwa kiutaratibu kwa mrithi wake.

Kuondoka ghafla kwa Mhe Kijazi si Jambo dogo kwenye utawala wa nchi, huyu alikuwa mshauri mkuu wa Rais na aliyahifadhi mengi ambayo hakuna mwingine aliyeweza kuyafahamu isipokuwa watu wawili labda na wasaidizi wao.
Kufikia hapa, unapiga propaganda tu hakuna lolote linalohusiana na kichwa cha mada yako; kwa hiyo tayari umekwishaififisha mada yenyewe.

Basi ngoja nijibu kichwa cha mada, maanake nimechoka kupoteza muda kusoma hadi huko chini.

"Napingana na wanaosema afya ya rais si siri"

Ikiwa ni siri watu watajua kuwa huyo rais hawezi kuumwa?

Wewe umejuaje kuwa hayo uliyobuni ndiyo sababu rais haonekani hadharani!
 
Suala la afya ya Mh. Rais yajadiliwa kwa mapana huku yakiangaliwa pia masuala kadhaa mtambuka

 
Kama ni siri zile pushap zilikuwa kutuonesha nini ama alikuwa anajifurahisha?
Zile pushups alifanya kwenye Jukwaa la Mkutano wa hadhara wa kampeini kuonyesha yuko imara baada ya minong'ono ya hali ya Afya yake kuzagaa mitaani na alishinda Uchaguzi na kuongoza nchi miaka 5 bila tatizo lolote la kiafya. Katika Uongozi wake alijiwekea utaratibu wa kujionyesha kwa kila alichofanya au alichosema ili asifiwe na kupongezwa mpaka wakati mwingine tabia hii ikawa inawakera watu na kuwafurahisha wengine. Pale Ikulu shughuli ndogo tu ikifanyika, makamera yote ya Luninga yatakuwa pale kuujulisha ulimwengu kinachoendelea na viongozi wa Chama, Mashekhe, Maaskofu, Wakuu wa Vyombo vya Usalama, uongozi wa Bunge, Mahakama nk watakaribishwa kushuhudia. Wasiwasi ulianza kujitokeza siku Mabalozi 3 wa Nchi za Nje walipokuja kwa mara ya kwanza kuwasilisha Hati zao Utambulisho ili waanze kazi Tanzania, badala ya kupokelewa na Rais Ikulu kama ilivyo kawaida, walipokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje bila mbwembwe zilizozoeleka. Huko nyuma tumeona Rais anakwenda Kivukoni kununua samaki au ananunua mahindi ya kuchoma au kununua jogoo au kule Ikulu Chamwino tumeona anajianika kwenye mawe kama mjusi kwa dunia yote kumwona. Kama hayupo Ikulu ya Dar atakuwa Ikulu ya Dodoma au Chato na wananchi watajua alipo maana misafara yake ya kuelekea huko haijawahi kuonekana toka tupate Uhuru na kabla. Wananchi kuulizia Kiongozi wao kama mgonjwa si kosa kabisa ila kusema mgonjwa anaugua ugonjwa fulani ni kosa kwa sababu hata mgonjwa mwenyewe anaweza asijue anaugua nini mpaka aambiwe na Daktari baada ya kumpima. Tatizo kuna magonjwa yanajulikana bila Daktari!
 
Nimpongeze Mhe. Rais kwa kuamua kukaa chini na kufanya kazi za ofisi ikiwemo kuhakikisha mambo nyeti yaliyokuwa yanasimamiwa na Marehemu Balozi Kijazi yanakabidhiwa kiutaratibu kwa mrithi wake.

Kuondoka ghafla kwa Mhe Kijazi si Jambo dogo kwenye utawala wa nchi, huyu alikuwa mshauri mkuu wa Rais na aliyahifadhi mengi ambayo hakuna mwingine aliyeweza kuyafahamu isipokuwa watu wawili labda na wasaidizi wao.

Kwa kiongozi anayeliwazia mema na Taifa na kiongozi aliyefanya kazi kubwa ya mageuzi kwenye utumishi na mfumo wa serikali ikiwemo kupambana na ufisadi lazima akae ayapitie majalada yote nyeti nakutoa marlekezo kwa Katibu Mkuu Kiongozi.

Lakini pia ipo hoja ya kuumwa, sidhani kama kukaa ofisini ukafanya kazi zako kumekatazwa kikatiba, hakuna sehemu katiba inamtaka Rais anatakiwa aonekane mara ngapi kwa wiki, mwezi au mwaka. Hivyo kukaa kwake kimya si kinyume Cha sheria.

Tatu Rais haendeshwi kwa matakwa ya watu flani wenye maslahi yao binafsi kwamba leo watamwambia ongea akaongea na kesho wakamwambia nyamaza akanyamaza. Rais ni mkuu wa nchi na hapaswi kuendeshwa na genge flani la watu. Hawa hawa mwaka jana walivumisha habari hizihizi lakini matokeo yalionekana. Tusipende kuibaka katiba kwa kuitumia vibaya au kuitafsiri tutakavyo.

Kama yupo mwenye ushahidi kwamba anaumwa aweke wazi na hapo ndipo zitaibuka hoja za kisheria na kikatiba na serikali itawajibika kujibu.

KUENDELEA KUMTAKA RAIS AJITOKEZE AACHE KAZI ALIZOKABIDHIWA NA SERIKALI NI UTOVU WA NIDHAMU DHIDI YA TAASISI HII NYETI. HATA AKIKAA MWAKA HAKUNA SEHEMU KATIBA INAMLAZIMU AJITOKEZE KUFANYA KAZI KWENYE MEDIA.

HONGERA SERIKALI KWA KUWEZA KUDHIBITI UPEPO WA WAHUNI WA MITANDAONI
😂😂 SI KWELI. Labda ingekuwa suku 2, 3 au 4. Lakini how come sasa iwe karibu mwezi sasa Jiwe halionekani...??

Unasema anapitia mafaili ya nini eti?

Ya marehemu KM Balozi Kijazi...?

Kwani yeye Magufuli alisafiri safari ndefu ya mwezini na kumkuta KM wake Kijazi kafariki na sasa amerudi na anataka kujua kuna nini ktk mafaili hayo...??

Inafurahisha sana. Maana wengine wanasema eti yuko chimbo anapitia jina la Katibu Mkuu wa CCM kisha ateue...

Huyu huyu arrogant & boastful Magufuli asiwe kwenye Spotlights kwa karibu mwezi sasa?

ABSOLUTELY, IMPOSSIBLE. JIWE ANA SHIDA, ANA TATIZO SI BURE....!;
 
Nimpongeze Mhe. Rais kwa kuamua kukaa chini na kufanya kazi za ofisi ikiwemo kuhakikisha mambo nyeti yaliyokuwa yanasimamiwa na Marehemu Balozi Kijazi yanakabidhiwa kiutaratibu kwa mrithi wake.

Kuondoka ghafla kwa Mhe Kijazi si Jambo dogo kwenye utawala wa nchi, huyu alikuwa mshauri mkuu wa Rais na aliyahifadhi mengi ambayo hakuna mwingine aliyeweza kuyafahamu isipokuwa watu wawili labda na wasaidizi wao.

Kwa kiongozi anayeliwazia mema na Taifa na kiongozi aliyefanya kazi kubwa ya mageuzi kwenye utumishi na mfumo wa serikali ikiwemo kupambana na ufisadi lazima akae ayapitie majalada yote nyeti nakutoa marlekezo kwa Katibu Mkuu Kiongozi.

Lakini pia ipo hoja ya kuumwa, sidhani kama kukaa ofisini ukafanya kazi zako kumekatazwa kikatiba, hakuna sehemu katiba inamtaka Rais anatakiwa aonekane mara ngapi kwa wiki, mwezi au mwaka. Hivyo kukaa kwake kimya si kinyume Cha sheria.

Tatu Rais haendeshwi kwa matakwa ya watu flani wenye maslahi yao binafsi kwamba leo watamwambia ongea akaongea na kesho wakamwambia nyamaza akanyamaza. Rais ni mkuu wa nchi na hapaswi kuendeshwa na genge flani la watu. Hawa hawa mwaka jana walivumisha habari hizihizi lakini matokeo yalionekana. Tusipende kuibaka katiba kwa kuitumia vibaya au kuitafsiri tutakavyo.

Kama yupo mwenye ushahidi kwamba anaumwa aweke wazi na hapo ndipo zitaibuka hoja za kisheria na kikatiba na serikali itawajibika kujibu.

KUENDELEA KUMTAKA RAIS AJITOKEZE AACHE KAZI ALIZOKABIDHIWA NA SERIKALI NI UTOVU WA NIDHAMU DHIDI YA TAASISI HII NYETI. HATA AKIKAA MWAKA HAKUNA SEHEMU KATIBA INAMLAZIMU AJITOKEZE KUFANYA KAZI KWENYE MEDIA.

HONGERA SERIKALI KWA KUWEZA KUDHIBITI UPEPO WA WAHUNI WA MITANDAONI
wacha nikugeuzie kifuu, kama wewe una ushahidi kwamba haumwi weka wazi hapa, na sio ushahidi wa fulani kasema.
Taifa lina haki kabisa kuuliza alipo rais wao pale anapotokea kutoonekana kupita desturi yake. Wewe mwenyewe unakumbuka ni lini toka jiwe awe madarakani kushindwa kurushwa hutuba zake za kanisani kila jumapili? Hilo halikufanyi kujiuuliza ni kwa nini ghafla asionekane? Hushangai ni kwa nini ameshindwa kuhudhuria mkutano wa viongozi wa EAC ambao ulikuwa virtual? Kwa nini awe popote pale alipo alishindwa kuhudhuria? Yote hayo bado bichwa lako linakubali kudanganywa tu?
 
Safi sana mleta mada...Katiba inasema pia Rais anayo mamlaka ya kukataza vyama vya Upinzani kufanya siasa ila ni Chama chake tu kinacho ruhusiwa kufanya Siasa wakati wote na sehem yoyote
 
K

Kwani akiamua kuchukua faragha kwa muda fulani ili atekeleze na kufuatilia kwa karibu mambo fulani katika utawala wake hapo kuna shida gani? Anaweza kujitakia faragha pia kwa ajili ya kuliombea Taifa dhidi ya Corona (mfano tu) hapo kuna shida gani? Naamini ni kwa faida ya kitaifa kuwa kwa sasa anafanya kazi bila kuonekana hadharani. Hata kama hauelewi ndivyo ilivyo.
Unaongea kama mtoto, uliwahi kuona wapi kiongozi wa nchi akifanya kazi hivyo.

It's just a matter of time before we know the truth something that will be a setback to the government.
 
Safi sana mleta mada...Katiba inasema pia Rais anayo mamlaka ya kukataza vyama vya Upinzani kufanya siasa ila ni Chama chake tu kinacho ruhusiwa kufanya Siasa wakati wote na sehem yoyote
Atupe kifungu cha katiba kinachompa hayo mamlaka.
 
Bila kutetea upande wowote. Unfortunately, once a Public figure you cease having a private life - your life is for public consumption and scrutiny. Ndio maana wengine hawajaingia kuwa viongozi wa dini, siasa, royal family n.k kwa sababu hii. Waulize hata wale wanaojiita Emir wa ISIS.

Kwa kila choice we make - there are sacrifices.
 
Yaani mitandaoni huku wamejaa wahuni watupu mtu anakaa anaamua kuanzisha uzushi kisa ameshiba kande zake.
 
Kwa tabia ya rais kuonekana kwenye vyombo vya habari kila siku toka aingie madarakani na sasa kutoweka ghafla kunaonyesha kuwa kuna tatizo pahali.

Kibaya zaidi ni pale serikali inapojaribu kuficha ukweli bila kujua kuwa muda wenyewe unaenda mbio na ndio utakaoleta ukweli siku chache zijazo.

Tumeongea humu mara kadha wa kadha kuwa hakuna binadamu special mbele ya Mungu lakini kuna watu wamekuwa wakimuona rais kama mtu tofauti hata machoni pa mwenyezi Mungu kitu ambacho sio kweli kabisa.

Hakuna kinachoweza kufichwa milele, ukweli utadhihiri tu na huenda serikali ikatafuta pa kuficha kichwa siku chache zijazo.
Nchini kuna vyombo zaidi ya 90% vinamilikiwa binafsi, na pia kuna vyombo vya habari vya mataifa ya nje, na Balozi mbalimbali. Hivi, inaingia akilini upana huo wa kupata na kutoa habari umeshindwa bali tutumie mitandao ya kijamii! JIFIKIRISHE
 
Alituzoesha kumuona mara kwa mara kwenye vyombo vya habari kutoonekana kwake kwa muda mrefu kunatuacha na maswali mengi kichwani lakini majibu ya viongozi wetu kuhusu alipo yamekuwa ya kimipasho kwa kiasi fulani kusema Rais si parish worker au Rais si wa kuzura kariakoo naona majibu haya hayajakaa vizuri Kwani wakisema Rais yupo salama anaendelea na kazi zake kuna shida gani?
Weka orodha ya mwonekano wa Rais hadharani ili hoja yako iwe na uzito.
 
Back
Top Bottom