Makanyaga
JF-Expert Member
- Sep 28, 2007
- 10,327
- 6,850
Huyu mtu ana uwezekano mkubwa sana wa kurudi kwenye nafasi yake ya mwanzo kwenye Baraza la Mawaziri linalofuata. Kuna dalili hizo.Asipoingia mwanzoni, basi anaweza akaja akaingia baadaye kule mbele ya safari kama kuna chochote kitatokea! Aliachia ngazi kwa haki kabisa, ila kwangu mimi ni kati ya watu ambao niliwahi kusikitika kuwakosa ndani ya Baraza letu la mawaziri. Mungu azidi kimbariki.APITA BILA KUPINGWA UBUNGE MTAMA Lindi:
Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Mtama mkoani Lindi, Samuel Warioba Gunza amemtangaza Nape Nnauye mgombea ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi kuwa mgombea pekee wa jimbo hilo.
Pia soma => Uchaguzi 2020 - Nape Nnauye anaelekea kupita bila kupingwa Jimbo la Mtama, mgombea CHADEMA alikamatwa jana huku ACT-Wazalendo wakiwa hawana mgombea