Nape ni mwanzilishi wa CCJ

Nape ni mwanzilishi wa CCJ

Kwa hiyo unachotuambia ni nini? Fine alikuwa mwanzilishi wa CCJ then what. Kwa sababu hata yeye alishiriki akiwa bado yuko CCM, je huo siyo unafiki. Kwa nini hakubaki ndani ya CCJ ili aijenge na kuifanya iwe maarufu badala ya kuhamia CDM? Hivi vyama ni kama mitumbwi ya kukuvusha ng'ambo kwa usalama. Lakini lililo la msingi ni kwamba yeye Nape yuko CCM na anatetea sera au misimamo ya chama chake , kama ambavyo na yeye Mpendazoe ana haki ya kutetea sera na misimamo ya Chadema.

Hii siyo contest ya loyalty kwa chama hiki au kile, na ndiyo maana leo tunaona mwanasiasa huyu yuko kule na kesho yuko huku. Hata hiyo loyalty hupimwa wakati ukiwa ndani ya hicho chama na siyo baada ya kuondoka. Je Mpendazoe anataka kutuambia kwamba alipokuwa CCM kwa miaka yote hii hakuwa na loyalty na kwamba jicho lake lilikuwa kwenye upinzani? Naweza kuelewa frustrations za Mpendazoe hasa baada ya vigogo wenzanke kumchuuza ahame na wenzake watamfuata halafu wakamtosa lakini in politics kupima upepo huwa imo. Nani alijua leo hii Ntagazwa angekuwa huko aliko au Dr. Slaa huyu? Katika siasa haya yote hutokea na yanapotokea mtu hutakiwa kila la heri kule aendako na akishindwa na kurudi hasutwi. Waone Makongoro Nyerere, Wasira, Nsazugwanko na hao akina Mpendazoe, Shibuda, Kahigi, Slaa, Ntagazwa na wengine wengi.

hujaeleweka,swala ni kwamba kama kweli ni mpambanaji anaewatakia watanzania mema,angesimaamia maamuzi yake?na hivyo ndivyo alivyofanya Mpendazoe na sasa anapambana.
 
mbio za sakafuni huishia ukongoni...bila shaka dogo kafika kwenye ukingo wake kisiasa....simwoni atachomokaje, kwani hakutuhumiwa ni ukweli mtupu...msaliti wa wenzake asiyeweza tena aminiwa kupewa dhamana yoyote na chama chake...
 
Nina uhakika 100%. Lakini si rahisi kwa mtu aliyelewa ushabiki wa vyama kuamini. Kosa wanalolifanya baadhi ya viongozi wapenda pesa ndani ya CHADEMA litakicost CHAMA hiki ambacho kilikuwa tegemeo la walalahoi for the next 50 years watoto wa nchi tutakapoamua kumwaga mchele hadharani. Ni aibu x 1,000,000!


sasa nimekubali mnatapatapa.
 
Inasikitisha sana Taifa lisilokuwa na uzalendo. Haya ndiyo matokeo ya kubebana, hurumahuruma kumbe ufisadi mtupu! bado naamini CCM hakuna kitu, ni ujanja ujanja tuuuu, hakuna cha kujivua gamba wamba kujichuna ngozi, gamba limeshakomaa hilo, la kobe linaadhali unategemea nini? wazalendo wa kweli wanajua ukweli, Hakuna cha Nape wala cha nani, wote ni wale wale tu, wanatafuta kujaza matumbo yao kwa mgongo wa kupambana na ufisadi, ukichuza sana wanaopiga kelele ndo mafisadi kupita wanaotajwa mafisadi.. Watanzania uamuzi upo 2015 tutakapoonyesha uzalendo wa kweli kuwaambia tumechoshwa na usaniii wao CCM... MABADILIKO YANAWEZEKANA....... Haiwezekani kuendelea na watu wenye rangi zaidi ya kinyonga na kuwafanya watanzania mambumbumbu kila siku... tumechokaaaaa habari ndiyo hiyo.... inawezekanaje anayepigia debe uadilifu katika CCM leo, akawa alihusika kuanzisha chama kipya CCJ, kama sio hadaa? mtu huyu kesho akitemwa CCM si ndo watakaotuingiza msituni hawa kwa sababu za uroho wa madaraka? kuna umakini kweli hapo? tuwakatae!!!!!!!! hatudanganyiki
 
so kabla ya wenye magamba hawajawajibika, atakuwa amewajibika yeye!! siasa bwana. ukiiendea puta utaishia pabaya. nadhani atakua ametuachia vocabulary mpya ya kiswahili baada ya zile za kihiyo, halahala...sasa itauwa nape
 
Siku moja baada ya kamanda Mpendazoe kugongesha yai kwenye shoka! Yule kijana hamnazo aka VuVuzeLa amesema ikithibitika atawajibika,hayo yapo ktk mahojiano na Grace Michael wa gazeti la Majira!

Sijui anataka ukweli gani huyu?
uwajibikaji ulikua enzi za mwalimu... sio enzi hizi za magamba na siasa za maji taka!!! BTW, hivi kuna tuhuma yoyote inayomhusu kiongozi wa chama tawala imeshawahi kuthibitika siku za karibuni?
 
Siku moja baada ya kamanda Mpendazoe kugongesha yai kwenye shoka! Yule kijana hamnazo aka VuVuzeLa amesema ikithibitika atawajibika,hayo yapo ktk mahojiano na Grace Michael wa gazeti la Majira!

Sijui anataka ukweli gani huyu?

Nape, kuvua nguo kwenye kaadamnasi ni wehu, kutembea uchi ni wendawazimu na kubaki uchi ni ukichaaa, je tukuweke kwenye kundi gan? Maana huna mlango wa kutokea
 
Nape Tauro lishandondoka hilo, cha msingi nakushauri ukitaka kuishambulia CHADEMA next time seek consultation.
 
Hahahah....ikithibitika, atajipima na kuchukua hatua atakoyoona yeye inafaa kama walivyowashauri magamba. Moja ya hatua hizo ni kama vile kuacha kuwasiliana tena na washkaji zake aliokua nao CCJ, kuchoma nyaraka zote zilizobaki za CCJ ambazo alikua nazo, na kadhalika na kadhalika na kadha wa kadha. KWISHAAAA....what next!
.
 
Nape, wakati wa kuwajibika kwako ni sasa. Hebu jarabu kupangua hoja za Mpendazoe kwa hoja zako.
Mene mene tekeli na perisi.
Writings on the wall, just google and u will know who u r.
 
Ndio kiongozi wa kesho!!! problem again ni vetting...kuweka bogus people!...kila siku ni trial & error...tutafika lini?
 
Hili gazeti mbona halijaibalance hii taarifa?zimewekwa tuhuma za EPA na tuhuma za Nape kugombea Ubunge kupitia Chadema bila kuweka majibu ya Nape kwenye masuala hayo, hii sio sahihi, i guess hili ni la Tanzania Daima hili, gazeti la Uhuru la Chadema.

Kimsingi sioni hoja hapa, CCM inatambua kuwa kuna wanachama wake waliokuwa wamekatishwa tamaa na mwelekeo ya chama chao na ndipo walipokuja sasa na mpango wa kujivua gamba ili kuwarudishia wanachama hawa matumaini mapya na kuwafanya warudi kundini, kwa mantiki hiyo CCM hawana shida na Nape kuwahi kutaka kujitoa na kuanzisha CCJ, sasa pilipili wasiyoila yawawashia nini Chadema? naona Nape anawapa tabu sana.

Lakini lingine...hivi unaenda Mbambabay unaongelea mambo ya Nape na CCJ wakati wananchi unaowaambia ata hawajui kama CCJ ni mdudu au ni mnyama? Huku ni kupoteza nafasi ya kuwaeleza wananchi mambo yanayowahusu wao na maisha yao na namna gani Chadema itayabeba matarajio na changamoto zao kwa kesho bora zaidi.

Sawa yameongelewa huko lakini na sisi huku tuliokuwa hatujui tumegundua, na hii sio nzuri kwa ccm, inaonyesha wasivyo makini katika kuteua viongozi, kiongozi ni muhimu akawa na misimamo ndani ya Chama na awe tayari kupambana na uovu ndani ya chama na si yule ambaye yupo tayari kukimbia.
 
Tuhuma alizotoa Mpendazoe ni za kina (detailed) sana. Mbona Nape hakanushi kama si kweli hakuandika ile katiba ya CCJ wala akufanya ukuwadi wa kukusanya pesa toka kwa wafadhili wala kutafuta nyumba ya ofisi ya CCJ. Kama alifanya yote hayo kweli atashindwa kuwambia undani wa CCM-Chama chake "kipenzi?"
 
Huyu kijana anapenda sana madaraka! Sidhani kama ana guts za kujiuzulu!

Baada ya kuchakachuliwa UVCCM alipanic na kuanza kufuikiria kuazisha CCJ,kapozwa na uDC na sasa kwenya propaganda ndo basi tena kila siku kwenye media tu.Kazi hazifanyiki kwa mdomo tu.
 
Back
Top Bottom