sosten2013
Member
- Jan 1, 2014
- 7
- 0
Ccm wote ni wezi hakuna mwenye unafuu.
Ila nape kiukweli kabisa, Muambie Katibu Mkuu aache hii biashara ya Meno ya Tembo inatutia aibu sana watanzania aisee.
Kama vipi tumpe kisiwa cha mafia basi aachane na hiyo kitu, Mbona kuna biashara nyingi tu.
hujui igunga waliua wakala wa chadema na sikichache walishasema... hata hivyo nilikuwa nazungumzia nape kupanda jukwaa moja kumnadi mkwe wa lowasa...
Nape Sacha kumwandama Lowasa, haumwezi kwani anakubalika hataufanyeje. Lowassa ni mchapakazi na mwadilifu.
Hivi utajiri wa Lowasa kaupataje vile?Nape punguza mdomo usijifanye mungu mtu,mimi naunga mkono lowasa kuwa mgombea kwasababu uweza anawo sababu anayo mwisho anamaamuzi magumu nchi itanyooka
Kweli Maccm ni manafiki sana, yanamshadadia Zitto kutangaza kugombea huko wao wakizuiana kutangaza nia
Acha kupotosha watu weka chote nilichosema. Nilichosema ni kuwa yeyote anayekiuka taratibu za chama katika mchakato ANAJIONDELEA SIFA za kuwa mgombea wa chama hichi!(Labda Chama kiamue kutofuata taratibu zake chenyewe, na kikiziacha hakina namna ya kuendelea kuaminiwa)!
Sasa si swala la Lowassa ni swala la KILA ANAYEKIUKA TARATIBU!kama naye anakiuka anaingia kwenye mkumbo huo, sio kwasababu ni Lowassa ila kwasababu ni mwana CCM na taratibu za CCM haziruhusu! Sio swala la Nape ni swala la taratibu,kanuni na sheria zilizowekwa kabla hata Nape hajazaliwa!
Haiwezekani watu wagawe rushwa hovyo tukae kimya tu kisa anayegawa flani!!!! Hivi kuna uwezekano wa kuingia na kiti moto msikitini ukapigiwa makofi?!! Unaweza kupigiwa makofi na kupewa uongozi wa kanisa wakati humwamini Yesu Kristo?!! Watanzania tusiogope kusema ukweli maana ndio utakaoiponya nchi yetu.
Kama mnamgombea ana sifa atachaguliwa tu huna haja ya kuongezea sifa zake kwa rushwa! Haya si yangu ya CCM, na ni kwa madiwani, wabunge na hata urais!
HERI YA MWAKA MPYA 2014!
Hata umpambe kwa namna ipi,huyo ni mwizi na watz wote wanajua hivyo!
Kila chama na funza wake anayepekenyua. CCM Lowassa, Chadema Zitto. TLP Mrema mwenyewe, Cuf Hamad Rashid, NCCR-Mageuzi Kafulila. Duh, noma!
Mkuu Tuko hawa CCM ni wanafiki tu, na wameshindwana wao kwa wao wanaingilia mambo ya ndani ya CHADEMA sasa.