Nape unatumika
Nape unatumikia kundi la wanaokutuma na sio Chama cha Mapinduzi.
Nape inatosha kwa Lowassa,Nape bakisha maneno,Nape kwa nini unakosa hofu ya Mungu kwa kuhakikisha wanaokutuma unawafurahisha na kumuumiza Lowassa,Nape bila aibu unasingizia Lowassa anawapa watu vyakula na kuwapa nauli na posho,naamini umetumiwa na shetani kwa sababu nimeshuhudia ujio wa watu hawa na wanahabari wenzangu hapakua hata na soda wala chakula kwa Lowassa,
Nape tamaa ya madaraka huwa tamu lakini punguza kwa maslahi ya nchi,unamtisha nani nape?
Nape unajua Membe amehonga basi kama kampeni kwa kanisa katoliki Tabora,askofu aligoma maana alihonga wakati askofu akiwa matibabu tuna picha za ushahidi siku membe Ameitwa kuonywa na Askofu wa Tabora,nape huyu kwa kuwa mungu wako wewe huwezi kumsema hadharani,
Nape mungu wako Membe na Gotham wamegawa rushwa zanzibar wakati nchi inaomboleza kifo cha Komba,kumbe Nape ulikua unaimba kishetani huku moyoni ukifurahia kufa kwa Komba maana Gotham na akina Makonda walikaa vikao kabla kufa Komba wakipanga kutafuta mtu wa kumpa band ya TOT hata kabla Komba hajafa,nape tunarekodi ya waliyoyasema walikuwepo wasanii akiwemo koppa na akina cheni haya tumeyatunza kwa wakati muafaka,
Nape tunarekodi ya mawasiliano yako na January makamba mlivopanga kuchafuana Edward,Nape unapinga simu kushinikiza gazeti la u huru kuipa coverage habari ya kishetani iliyofikia kwa Farisayo anayejifanya malaika wa asubuhi
Nape Farisayo mwenzio January huwezi kumkemea kwa sababu wakubwa mlitumia mbinu kumtoa kwa edward kumleta kambi yenu akagawa simu zaidi ya 790 kwa wana UVCCM na kuhonga wanavyuo Malaki,Nape Farisayo huyu Makamba akaanda kitabu alihonga magazeti akitoa machapisho yakafika kwa kila mjumbe wa mkutano mkuu ukiwa umefunga bakuli lako kwa kuwa anafanya kazi Za mabwana zako,
Ufarisayo wako haujaisha wewe umeanza kampeni mtama kila ilipotoa msaada tunajua na mahali ulipotoa pesa ,Nape Muogope Mungu Kakobe anakuuliZa Umeokoka Nape?
Nape unajua kanuni za chama chetu haziruhusu kufanya kampeni za kuligawa taifa
mtoto wa Rais Ridhwani aliandaa watu kuligawa taifa kuwa Rais wa nchi hawezi kutoka kaskazini Nape ulikua unajua hili linaweza kuligawa taifa lakini kwa kuwa ni bwana unaemtumikia ulikaa kimya Ridhwani hagusiki acha wanachama wanyonge tubaguliwe hata nyombo vya dola vilikaa kimya leo nasikia kwenye mzalendo eti vinafuatilia wanaofanya siasa kuligawa taifa hawawezi kuanza na Ridhwani kwa kauli yake ni mtoto wa mkubwa huyu hagusiki hata akitukana mashekhe wanyonge watatulia
Nape inatosha,maumivu uliyompa Lowasa tunanyenyekea kwako ewe mwenye kipaji cha kuzimu inatosha,Nape mnapanga mbinu ovu ili edward akatwe jina ili uendelee kuenjoy cake ya wanyonge,hawa wanaokuja kwa Edward Lowassa sio wana ccm ,ccm ni wewe Ridhwani,Gotham na Membe jengeni chama japo mlikiasi na kuunda CCJ,
Mh Jakaya Kikwete najua ujumbe huu utakufikia,utaacha mpaka lini viongozi wenye heshima watukanwe mpaka na watu ambao unaweza kuwaonya?Hivi tumekosa Jakaya huruma kwa Edward hata kidogo Ni kweli Edward amekua kinyago cha kushambuliwa ukikaa kimya?
Mangula wewe unasema umeokoka,ni ukristo gani wakushangilia akina Makonda wakimtukana Lowassa mmekaa kimya,nawaambia mnapanga mbegu Ngumu katika nchi
Nape,Mangula,Ridhwani,na Gotham na Membe kwa nini mnatumia turufu ya kumkata jina Lowasa huku mkijua anakubalika kwa umma,mnayafanya haya kwa maslahi ya nani?je ni ya wananchi au ya wale wa mezani aliowasema Jerry Slaa?
Jakaya kiokoe chama,muhurumie Edward Naye ni Binadamu,kuna maisha baada ya siasa Nape,
Namaliza kwa kusema,Nape pamoja na kazi nzuri unayofanya kuwarishisha waliokuweka hapo ulipo kionee huruma na chama,Lowassa amevuja damu muacheni watu ninyi!
Mungu mbariki Edward Lowassa na kumlilia
Mungu ibariki Tanzania