Nape: Kingunge afanye anachotaka

Nape: Kingunge afanye anachotaka

Katika hali ya kuonyesha mpasuko ni dhahiri ndani ya CCM, jana Nape amefunguka kuhusu msimamo na kauli za Kingunge na kumwambia afanye anachotaka kufanya.

Huyu Kijana naona mwisho wake ni Oct.2015


Nionavyo ubabe huu lazima CCM watavuna walichopanda na wanacho kipalilia. katika hali isiyo ya kawaida katibu mkuu mstaafu Mzee Makamba kaibuka na kumzodoa Kingunge kwamba anatetea maslahi yàke.

Acha mpambano uendelee.

Makamba bila haya aibu! Hajui mwanaye naye alikuwa sehemu ya wagombea-kwa hiyo yeye hakuwa na Masilahi binafsi?

Jeuri ya CCM ni uwapo wa vijana na watu wazima wa aina hii alafu watu oyeeeeeeeeeeeeee ! Maisha Bora kwa kila mtanzania.



attachment.php


Hili la viuno haikutosha likaja ;



 
CCM ni lazima wshinde kwa goli la mkono. Kama isingekuwa hivyo wangejali mpasuko. Kuwe na mpasuko ama kusiwe, wapiga kura wawachague ama wasiwachague, wao ni washindi kwa goli la mkono!!
 
Atoe ndani ya vikao vya chama ndiyo utaratibu wa CCM. Kingunge asilete utaratibu wa UKAWA na ndiyo maana Nape anasema afanye anachoona kinafaa kwa mtazamo wake, lakini kwa mtazamo wa chama Lowasa nje, maamuzi yameshafanyika. Chombo cha juu kabisa cha maamuzi ndani ya chama ni CC ikifuatiwa na kamati kuu na Mkuutano mkuu wa chama. Kingunge ni mwanachama siyo chombo cha maamuzi. Kama ingalikuwa mahakama, mahakama ya rufani ndiyo chombo cha juu cha kutafsiri sheria haiwezekani mahakama ya mwanzo iikosoe mahakama ya rufani?
Nape na wewe una adabu,kwani mtu akitoa mawazi ambayo ni tofauti na mtazamo wenu ndio umjibu namnahiyo.AAcha na yeye atumie demokrasia yake kama mtanzania.Si msapoti Lowasa but naye anaweza kutoa mtazqmo wake
 
Umesahau ni mwenyewe alisema kuwa kikao kimoja sio mwisho wa maamuzi, unaweza kukata rufaa kikao cha juu. Je alitumia nafasi hiyo? Kama hakutumia anamtishia nani sasa? Tangu MTU wake akatwe anaona aibu hata kuonana na viongozi wa chama ambao amewalea yeye. Mwalimu Jk aliwakemea viongozi kwenye vikao ikibidi aliwaita kwake.

Hivi kwa ule mchakato ulivyoendeshwa unadhani Kingunge na hata yeyote yule asieridhika anaweza kupata haki yake kweli kwa watu wale wale?kwanza unaambiwa Mwenyekiti alitoa majina mfuko wa tako licha ya yale aliyopewa na kamati ya maadili,sasa kwa muktadha huo unadhani kimebaki nini hapo kama sio ubabe,umafia na bora tukose wote?
 
Nape kakata mpaka jina la Mwandosya? Huyu kijana hatariii sana
Ndio demokresia. Kama hafai hafai hata kama ni mzazi wako. Sio wale wanaong'ng'ania maiti zinazotembea kuwa zinafaa wkt wanaona kabisa kuwa hakuna kitu. Labda uwezo wa kuganga njaa za watu
 
mzeeee kingungeeeeee ccm imejaa vijana siku hizi nakuomba upumzike hatuwezi kumpitisha mgombea anayetembea na daktari kumcheki afya yake kila sekunde wakati tunajua afya yake mgogoro anatafuta wadhamini kuonyesha kampeni anaweza jamani
 
Utatangulia wewe. Na atahudhuria mazishi yako. Ukienda kamuulize Holace Kolimba, alimuombea kifo Mtikila
 
Kingunge ameongea kwa uchungu sana na msipoangalia wana ccm hiyo laana itawatafuna hadi mifupa jifanyeni mnajua sana
 
Kamwe haiwezekani kumridhisha kila mtu matakwa yake

Watu walikua wanapiga kelele humu kila siku Lowassa hafai, wakaenda mbali na kumshambulia Kingunge kumuunga mkono Lowassa

Leo chama kimefanya yake lakini wale wale waliokua wanamlaani Lowassa wamegeuka watetezi wake ili mradi kuonyesha kuna mpasuko ndani ya ccm

Ccm ina misingi yake na haijawahi kuyumbisha umoja wao
Ninacho wahakikishia ni kwamba Lowassa atapita kwenye kampeni kumnadi Magufuli kama kawaida iwe hapendi au anapenda......... Ndio misingi ya chama

Chama kikisha fanya maamuzi yake kama hujaridhika misingi ya chama ni kutoa madukuduku ndani ya chama na si kwenye media
Ukilalamika kwenye media utajibiwa ki media media hivyo hivyo na ukilalamika ndani ya chama utajibiwa kichama kwa heshima
 
Hakuna mpasuko. Si mara moja au mbili kumekuwa na mawazo pinganifu na hatukusema mpasuko. Lowassa na Kingunge ni wanachama tu kama wengine if hawajaridhika wanaweza kuhamia vyama vingine au kuanzisha chao

ni kweli kabisa..chama si cha mtu mmoja,kulazimisha kujenga hoja za kitoto eti chama kitasambaratika ni uvivu wa kufikiri..chama kwanza mtu baadae!
 
Nape waheshimu wazee wako.

Kwani kamtukana jamani? Kamwambia afanye atakavyo yeye (Kingunge) anayemtetea huyu fisadi Lowasa. Mbona wanalazimisha hivyo? Lowasa alitaka kwenda kufanya biashara gani pale ikulu? MUNGU amemkataa asiwe mfalme wa nchi yetu basi na hakuna jinsi. Maana MUNGU alijua nia yake. Hata Nabii TB Joshua alipoenda kule Nigeria alimwambia mikono yake inanuka damu maana amewaibia sana waTZ. Sasa alitakiwa kujipima na kuacha kuchukua hata fomu ya kugombea lakini kwa tamaa na uchu wa mali uliopitiliza aliamua kutumia nguvu ya pesa ili apate hayo madaraka. MUNGU akishasema NO basi hata ufanyeje na yeye (Lowasa) amejidhihirishia hili.
 
Kueneza propaganda kwamba kuondoka kwa Lowasa kutaleta mpasuko ndani ya chama si kweli..kama kungekuwa na mgawanyiko tungeona pale zilipopigwa kura na mmoja wa wagombea kuibuka kidedea kwa ushindi wa 82%..unaanzaje kusema Kuna mpasuko hapo!?#kwa mara ya kwanza ccm wamempata mgombea katika duru moja tu ya uchaguzi!!#unawezaje kusema Kuna mpasuko hapo!??
 
Wacha viumane ......yalioandikwa yatatimia tu!! kama siyo Dodoma Basi hata kabla ya Oct. 2015:A S-rap:
 
Back
Top Bottom