kwa madini sasa hivi Tanzania yawe na madhara yasiwe nayo hayatusaidii chochote sana sana tunazidi kukaribisha waibaji aka wawekezaji ili waje watuudhi zaidi! madini mengine yametusaidia nini? wezi,utapeli na ubinafsi wa viongozi, tena kwa hilo bora tukatae tu maana hata kama hayana madhara maadamu kuna wasiwasi na wala madini hayatusaidii chochote tumebaki kuwa maskini wa kutupwa bora tupinge labda kweli kuna madhara! dhahabu watu wanachimba wanabeba wanapeleka ulaya sisi tunaishia kuwa manamba tu kwenye migodi,hata historia ya kina chifu mangunga haitusaidii chochote kujifunza tunafanya yaleyale tu.
Mara gesi nyingi imegunduliwa mimi binafsi nilishakata tamaa wala hata sifuatilii tena maana najua haitusaidii kitu watanzania tulio wengi sana sana tutaishia kufukuzwa maeneo tunayo kaa kupisha miradi ya wizi tu. Kilichobaki sasa ni kupigania uhuru upya ili kuikomboa nchi yetu maana hatuko huru tena na hata police nao maskini wenzetu ndiyo wanaotumiwa kutugandamiza wamelewa sifa za kuitwa vyombo vya dola huku maisha yao na wao ya hovyo kama nini,ila hao ndiyo number moja kuwamaliza maskini wenzao!
Mara gesi nyingi imegunduliwa mimi binafsi nilishakata tamaa wala hata sifuatilii tena maana najua haitusaidii kitu watanzania tulio wengi sana sana tutaishia kufukuzwa maeneo tunayo kaa kupisha miradi ya wizi tu. Kilichobaki sasa ni kupigania uhuru upya ili kuikomboa nchi yetu maana hatuko huru tena na hata police nao maskini wenzetu ndiyo wanaotumiwa kutugandamiza wamelewa sifa za kuitwa vyombo vya dola huku maisha yao na wao ya hovyo kama nini,ila hao ndiyo number moja kuwamaliza maskini wenzao!