Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
Awali ya yote, nikiwa kama Mwana CCM, naongozwa na kanuni muhimu sana ya chama inayosema:
Kukosoa na Kukosoana Ndio Silaha ya Mapinduzi.
Vile vile tuna kanuni nyingine muhimu sana ndani ya Chama chetu inayosema:
Nitasema Ukweli Daima, Fitina Kwangu Mwiko.
Moja ya mambo ambayo yamekuwa yanakivuruga chama chetu ni tabia ya viongozi na wanachama kuwa na unafsi, ambao ni ugonjwa mbaya sana. Hata Mwalimu Nyerere aliwahi kulizungumzia tatizo hili ndani ya kitabu chake cha TANU na Rais (1962) ambapo alikemea sana tabia za unafiki, fitina, uwoga na unafsi miongoni mwa viongozi na wanachama wa TANU.
Kwa mfano, Mwalimu anatamka kwamba:
"Makosa yetu mengine hutokana na woga; woga unaotuzuia kumlaumu mkubwa japo tunajua kuwa kakosa, au kumtetea mdogo anayelaumiwa na wakubwa japo tunajua hana makosa. Na msingi wa woga pia ni unafsi. Pengine huwa tunaogopa sisi wenyewe kulaumiwa au kupata hasara fulani. Pengine twaweza kuwa hatuna cheo chochote ambacho tunaogopa kupoteza; pengine hatuna wala tamaa yoyote ya kupata cheo fulani. Lakini woga unaweza kutokana na tamaa ya kila binadamu kupendwa na binadamu wenzake. Sisi wote tunayo tamaa hii, au sivyo tusingekuwa binadamu. Woga huu huweza ukamfanya mtu kuvumilia maovu, hasa kama maovu yale yanatendwa na walio wengi kwa walio wachache, au yanatendwa na wakubwa kwa wadogo. Kwa kuogopa kuwaudhi wengi tunaacha watende makosa bila kuwasahihisha, wasije wakatuchukia. Huu ni unafsi mbaya sana. Ni kweli kwamba demokrasia haiwezi kudumu ikiwa wachache hawatakubali matakwa ya wengi. Lakini matakwa ya wengi hujulikana katika majadiliano au mazungumzo ya wazi wazi."
J.K Nyerere, TANU na Raia (1962, pp2-3).
----------------------------------------------------
Katika siku za hivi karibuni, Nape kama kiongozi wa chama chetu amekuwa anatuchanganya sana sisi vijana wenzake ambao bado tuna mapenzi na CCM, na maoni haya sio yangu tu bali ya vijana wengi tuliopo site. Tumekuwa tunamtetea kwa nguvu zetu zote kwenye mijadala yetu vijiweni lakini kila siku zinavyozidi kwenda mbele, tunazidi kuishiwa na ammunition za kutumia kupambana kwa hoja. Kwa mfano, karibia mwezi mmoja uliopita, Nape alitoa tamko kwenye vyombo vya habari kwamba yeye haoni tatizo lolote Mzee Mustapha Sobodo kuchangia fedha Chadema. Lakini jambo la kushangaza na linalotufanya sasa tukimbie vijiwe ili kuficha nyuso zetu ni hili:
Mzee Sobodo ni mtanzania kama watanzania waliokusanyika Serena Hotel na kuichangia Chadema milioni 70 hapo kwa papo (huku nyingine zikiwa ni ahadi/pledges). Kitendo hiki hakikumfurahisha Nape, ingawa ukweli ni kwamba ni kiwango kidogo kuliko kile alichotoa mtanzania mwingine – Mzee Sobodo ambacho nadhani ilikuwa ni fedha taslimu shilling milioni 100. Sasa iweje suala la Mzee Sobodo (mtanzania kutoa fedha taslimu milioni 100 kwa Chadema) lisiwe tatizo lakini watanzania wengine pale Serena kutoa fedha taslimu milioni 70 iwe tatizo? Yupo kijana mmoja wa chama cha upinzani ambae huwa tupo pamoja kijiweni kwetu alitoa kauli moja ambayo kidogo iliharibu hali ya hewa, na binafsi nisingependa kuamini kwamba yupo sahihi. Kijana huyu alitamka kwamba:
----
"huyo Nape wenu anawachanganya tu, ‘inawezekana' (akasisitiza tena ‘inawezekana') suala la mzee Sobodo analiunga mkono kwa nia ya kujijenga na Mzee huyu mzalendo ili aje kumsaidia apate jimbo moja la ubunge mwaka 2015 huko kusini kwani Mzee Sobodo na Nape wote wanatokea mkoa wa Lindi. Isitoshe, ndoto za Nape ubungo zimemalizwa na John Mnyika."
----
Maneno haya yalinishtua sana na nisingependa kuamini kwamba hii ndio dhamira kuu ya Nape kuwa na msimamo tofauti na suala la harambee ya chadema pale serena (milioni 70 fedha taslimu) vis a vis suala la Mzee Sobodo (milioni 100 fedha taslimu). Isitoshe, sina uhakika kama kweli mzee Sabodo anatokea Kusini.
Haya ndio maoni yangu kama mwana CCM bila ya unafiki, fitina wala woga, na napata ujasiri wa kunena haya kwani hata Mwalimu Nyerere kama tulivyokwisha ona anahimiza kwamba kufanya hivyo ndio kukijenga chama, na kinyume chake ni kukibomoa chama. Hii ndio dhana nzima kanuni ya "Kukosoa na Kukosoana Ndio Silaha ya Mapinduzi."
Vijana wengi waliopo ‘site' hawana access yoyote kwa Nape, na pia hawamjui in person, hivyo ni vigumu kwao kumpatia mawazo yao yenye lengo la kujenga chama ndani ya misingi niliyokwisha ijadili. Mitandao kama JamiiForums ndio huwa tegemeo la wengi towards that end. Isitoshe, Nape ni mtumiaji mzuri wa mtandao huu kwani tumemuona mara kwa mara akijibu hoja mbali mbali kwa uvumilivu wa hali ya juu. Vinginevyo, katika kipindi cha miezi ya hivi karibuni, Nape amekuwa anatoa kauli ambazo sisi watetezi wake huku vijiweni mara nyingine inabidi tukimbie ili kuficha nyuso zetu – kwa mfano kauli dhidi ya wanachama wa CCM wanaohamia upinzani n.k. Kila kukicha, vijana wengi ambao bado wana mapenzi na CCM licha ya Chama chetu kukosa (au pengine niseme kukoseshwa) mwelekeo, huwa wanasali sana Nape arudie katika hali yake ya zamani alipokuwa UVCCM kwani vijana wengi walikuwa wanajidai na kujivunia sana kuwa na kiongozi wa aina yake, na kijana mwenzao ndani ya Chama ambae hakika alikuwa makini sana kwa kila jambo.
Nawakilisha.
Kukosoa na Kukosoana Ndio Silaha ya Mapinduzi.
Vile vile tuna kanuni nyingine muhimu sana ndani ya Chama chetu inayosema:
Nitasema Ukweli Daima, Fitina Kwangu Mwiko.
Moja ya mambo ambayo yamekuwa yanakivuruga chama chetu ni tabia ya viongozi na wanachama kuwa na unafsi, ambao ni ugonjwa mbaya sana. Hata Mwalimu Nyerere aliwahi kulizungumzia tatizo hili ndani ya kitabu chake cha TANU na Rais (1962) ambapo alikemea sana tabia za unafiki, fitina, uwoga na unafsi miongoni mwa viongozi na wanachama wa TANU.
Kwa mfano, Mwalimu anatamka kwamba:
"Makosa yetu mengine hutokana na woga; woga unaotuzuia kumlaumu mkubwa japo tunajua kuwa kakosa, au kumtetea mdogo anayelaumiwa na wakubwa japo tunajua hana makosa. Na msingi wa woga pia ni unafsi. Pengine huwa tunaogopa sisi wenyewe kulaumiwa au kupata hasara fulani. Pengine twaweza kuwa hatuna cheo chochote ambacho tunaogopa kupoteza; pengine hatuna wala tamaa yoyote ya kupata cheo fulani. Lakini woga unaweza kutokana na tamaa ya kila binadamu kupendwa na binadamu wenzake. Sisi wote tunayo tamaa hii, au sivyo tusingekuwa binadamu. Woga huu huweza ukamfanya mtu kuvumilia maovu, hasa kama maovu yale yanatendwa na walio wengi kwa walio wachache, au yanatendwa na wakubwa kwa wadogo. Kwa kuogopa kuwaudhi wengi tunaacha watende makosa bila kuwasahihisha, wasije wakatuchukia. Huu ni unafsi mbaya sana. Ni kweli kwamba demokrasia haiwezi kudumu ikiwa wachache hawatakubali matakwa ya wengi. Lakini matakwa ya wengi hujulikana katika majadiliano au mazungumzo ya wazi wazi."
J.K Nyerere, TANU na Raia (1962, pp2-3).
----------------------------------------------------
Katika siku za hivi karibuni, Nape kama kiongozi wa chama chetu amekuwa anatuchanganya sana sisi vijana wenzake ambao bado tuna mapenzi na CCM, na maoni haya sio yangu tu bali ya vijana wengi tuliopo site. Tumekuwa tunamtetea kwa nguvu zetu zote kwenye mijadala yetu vijiweni lakini kila siku zinavyozidi kwenda mbele, tunazidi kuishiwa na ammunition za kutumia kupambana kwa hoja. Kwa mfano, karibia mwezi mmoja uliopita, Nape alitoa tamko kwenye vyombo vya habari kwamba yeye haoni tatizo lolote Mzee Mustapha Sobodo kuchangia fedha Chadema. Lakini jambo la kushangaza na linalotufanya sasa tukimbie vijiwe ili kuficha nyuso zetu ni hili:
Mzee Sobodo ni mtanzania kama watanzania waliokusanyika Serena Hotel na kuichangia Chadema milioni 70 hapo kwa papo (huku nyingine zikiwa ni ahadi/pledges). Kitendo hiki hakikumfurahisha Nape, ingawa ukweli ni kwamba ni kiwango kidogo kuliko kile alichotoa mtanzania mwingine – Mzee Sobodo ambacho nadhani ilikuwa ni fedha taslimu shilling milioni 100. Sasa iweje suala la Mzee Sobodo (mtanzania kutoa fedha taslimu milioni 100 kwa Chadema) lisiwe tatizo lakini watanzania wengine pale Serena kutoa fedha taslimu milioni 70 iwe tatizo? Yupo kijana mmoja wa chama cha upinzani ambae huwa tupo pamoja kijiweni kwetu alitoa kauli moja ambayo kidogo iliharibu hali ya hewa, na binafsi nisingependa kuamini kwamba yupo sahihi. Kijana huyu alitamka kwamba:
----
"huyo Nape wenu anawachanganya tu, ‘inawezekana' (akasisitiza tena ‘inawezekana') suala la mzee Sobodo analiunga mkono kwa nia ya kujijenga na Mzee huyu mzalendo ili aje kumsaidia apate jimbo moja la ubunge mwaka 2015 huko kusini kwani Mzee Sobodo na Nape wote wanatokea mkoa wa Lindi. Isitoshe, ndoto za Nape ubungo zimemalizwa na John Mnyika."
----
Maneno haya yalinishtua sana na nisingependa kuamini kwamba hii ndio dhamira kuu ya Nape kuwa na msimamo tofauti na suala la harambee ya chadema pale serena (milioni 70 fedha taslimu) vis a vis suala la Mzee Sobodo (milioni 100 fedha taslimu). Isitoshe, sina uhakika kama kweli mzee Sabodo anatokea Kusini.
Haya ndio maoni yangu kama mwana CCM bila ya unafiki, fitina wala woga, na napata ujasiri wa kunena haya kwani hata Mwalimu Nyerere kama tulivyokwisha ona anahimiza kwamba kufanya hivyo ndio kukijenga chama, na kinyume chake ni kukibomoa chama. Hii ndio dhana nzima kanuni ya "Kukosoa na Kukosoana Ndio Silaha ya Mapinduzi."
Vijana wengi waliopo ‘site' hawana access yoyote kwa Nape, na pia hawamjui in person, hivyo ni vigumu kwao kumpatia mawazo yao yenye lengo la kujenga chama ndani ya misingi niliyokwisha ijadili. Mitandao kama JamiiForums ndio huwa tegemeo la wengi towards that end. Isitoshe, Nape ni mtumiaji mzuri wa mtandao huu kwani tumemuona mara kwa mara akijibu hoja mbali mbali kwa uvumilivu wa hali ya juu. Vinginevyo, katika kipindi cha miezi ya hivi karibuni, Nape amekuwa anatoa kauli ambazo sisi watetezi wake huku vijiweni mara nyingine inabidi tukimbie ili kuficha nyuso zetu – kwa mfano kauli dhidi ya wanachama wa CCM wanaohamia upinzani n.k. Kila kukicha, vijana wengi ambao bado wana mapenzi na CCM licha ya Chama chetu kukosa (au pengine niseme kukoseshwa) mwelekeo, huwa wanasali sana Nape arudie katika hali yake ya zamani alipokuwa UVCCM kwani vijana wengi walikuwa wanajidai na kujivunia sana kuwa na kiongozi wa aina yake, na kijana mwenzao ndani ya Chama ambae hakika alikuwa makini sana kwa kila jambo.
Nawakilisha.