Nape hajaelewa vema hoja ya Zitto

Nape hajaelewa vema hoja ya Zitto

mafinga kwetu

Member
Joined
Nov 21, 2010
Posts
35
Reaction score
3
Kutokana na maelezo aliyoyatoa Nape kuhusiana na issue ya posho nadhani kuna kitu hakuelewa vema kutokana na posho zinazidaiwa zifutwe, kwa jinsi nilivyomuelewa zito anataka pesa wanazolipwa wabunge kwa kukaa vikao(sitting allowance) si sahihi kwani wabunge ndio kazi zao na wanalipwa salary na posho(travel compensations) kwa kazi hiyo.Pia hoja ya zito na chadema kwa jinsi nilivyomuelewa lengo hii kitu iendelee si kwa wabunge pekee bali mpaka taasisi zingine za serikali.

Nape alizungumzia kuwa wabunge na watumishi wengine wataishi vipi bila posho.kwa jinsi nilivyoelewa ndio maana nahisi kuwa nape hakuelewa nini zito anamaanisha ...Nami binafsi nadhani si sahihi kwani vikao vya bunge ni sehemu ya majukumu yao na wnalipwa kwa kazi hiyo.

Thanks
 
Kutokana na maelezo aliyoyatoa Nape kuhusiana na issue ya posho nadhani kuna kitu hakuelewa vema kutokana na posho zinazidaiwa zifutwe, kwa jinsi nilivyomuelewa zito anataka pesa wanazolipwa wabunge kwa kukaa vikao(sitting allowance) si sahihi kwani wabunge ndio kazi zao na wanalipwa salary na posho(travel compensations) kwa kazi hiyo.Pia hoja ya zito na chadema kwa jinsi nilivyomuelewa lengo hii kitu iendelee si kwa wabunge pekee bali mpaka taasisi zingine za serikali.

Nape alizungumzia kuwa wabunge na watumishi wengine wataishi vipi bila posho.kwa jinsi nilivyoelewa ndio maana nahisi kuwa nape hakuelewa nini zito anamaanisha ...Nami binafsi nadhani si sahihi kwani vikao vya bunge ni sehemu ya majukumu yao na wnalipwa kwa kazi hiyo.

Thanks

Siyo kwamba Nepi hajamwelewa Zitto bali anafanya upotoshaji wa makusudi. Upotoshaji huo anaufanya kwa watu wasioelewa na wasioweza kuhoji anachowaambia
 
Usimlaumu Nape ndio uwezo wake wa kuelewa. Nilishawahi kumsikia siku moja akihojiwa na Clouds FM, kweli jamaa anauwezo mdogo wa kuelewa mpaka ikabidi wakati mwingine wale akina Kayanda wanamsaidia kumkumbusha baadhi ya majibu ambayo yeye alikuwa anakwenda chaka!

Lakini kumbuka kuwa Posho anazolipwa na CCM ndicho kitu ambacho hata yeye kinamsaidia sasa hivi katika kupeleka matumizi kwa mke na mtoto aliokuwa amewatelekeza pamoja na kwa matumizi yake binafsi.

Je unategemea ukisema posho zifutwe atakuelewa huyu!
 
Nape anafanya makusudi,ni dharau dhidi yetu walipa kopi. Nlimsikia anasema tukifuta posho za polisi je wakiamishwa wasilipwe?nape kwani ma polisi uhamishwa kila mwaka?je uhamishwa wote?je Zitto kuna sehemu kawataja ma polisi? Ujue hata ile 'sheria za ajira' haziwabani polisi na wanajeshi,sasa nape anaongea vitu gani? Sasa wameamua hata icho walichojipa hawataka kodi,ivi wana akili timamu au wanataka kuiacha serikali ijayo imekonda? Nape ueleweki!
 
Wafute za wabunge sio sie watumishi,mshahara 300,000 TGSD,alafu nisimamie mradi kijijini miezi sita kwa kutegemea mshahara hapa zito sipo na wewe.am CDM damu damu,lakn kwa hili mtanisamehe,DSA zangu naomba nipewe haraka tafadhari la sivyo pandisha mshahara hadi 3Mil
 
Zitto mbabaishaji, Mohamed Shosi alielezea vizuri "couldn't do it any better".

Hiyo ni kama muislaam kusema, msinipe urithi siutaki, wakati anajuwa hiyo ni sharia na haifutiki atapewa akitaka asitake.
 
Zitto mbabaishaji, Mohamed Shosi alielezea vizuri "couldn't do it any better".

Hiyo ni kama muislaam kusema, msinipe urithi siutaki, wakati anajuwa hiyo ni sharia na haifutiki atapewa akitaka asitake.
Mambo ya urithi ya Kiislamu yanatoka wapi?????????? Haya sasa na NCCR wamekataa hizo posho, unasemaje aua bado unamwangalia Mhs Zito tuu!!!!!!!!
 
Wafute za wabunge sio sie watumishi,mshahara 300,000 TGSD,alafu nisimamie mradi kijijini miezi sita kwa kutegemea mshahara hapa zito sipo na wewe.am CDM damu damu,lakn kwa hili mtanisamehe,DSA zangu naomba nipewe haraka tafadhari la sivyo pandisha mshahara hadi 3Mil

Mimi mara nyingine ninaachwa mdomo wazi na uelewa wa watu wengine? Labda ni kupotoshaji wa makusudi. Zitto hajasema POSHO zote zifutwe. Anachopendekezwa kufutwa ni sitting allowance, kwa kiswahili posho za vikao na hili sio kwa wabunge tu bali pia viongozi wengine wakubwa serikalini na taasisi zake. Kitu gani kigumu kueleweka hapa hata kama umemaliza STD VII??

Wabunge wakiwa Dodoma hulipwa posho za aina mbili 1. subsistance allowance (posho ya kujikimu). Hii Zitto anasema iendelee kuwepo. 2. Lakini wakati huo huo hulipwa sitting allowance simply kwa kuhudhulia vikaovya bunge ambavyo kimsingi ni majukumu yao. Hii ndiyo Zitto anapendekeza ifutwe. Lakini watu wameanza kupotesha mantiki ya suala hili wakidai eti Zitto anapendekeza Posho zote zifutwe kama anavyoseme Nape Nnaye kwa mapolisi eti wakihamishwa wasipewa posho!

Halafu wanadai suala la posho ni la kisera na lipo kwa mjibu wa sheria, kwamba CDM hawapaswi kulipinga wafuate utaratibu kama wanataka kuzitoa wakati wanafahamu kwamba Wabunge wa Magamba wako wengi na ni wachumia tumbo wata vote against! Sasa Anne Makinda amesema atawalipa kwa nguvu hizo posho CDM na NCCR. Kama mlifikiri wana beep wameshaandika barua ya kuzikataa kwanini mnawashinikiza, si mchukue nyinyi mafisadi (CCM) tu.
 
Zitto mbabaishaji, Mohamed Shosi alielezea vizuri "couldn't do it any better".


Hiyo ni kama muislaam kusema, msinipe urithi siutaki, wakati anajuwa hiyo ni sharia na haifutiki atapewa akitaka asitake.
wewe na hafcaste akili zenu zinzfanana.vikao vinavyolipa siting alowance mtu mwenye mshahara wa laki tatu hawezi ingia.
na wewe na akili yako mbovu unalinganisha sheria kandamizi na onezi za serkali ya kifisdi na sheria za mwenyezi mungu?
ona ulivyo na laana ya kiccm na utaendelea na mawazo yako mgando mpaka sheria hiyo itakapofutwa ndipo utabaki na aibu na ushabiki wako usiokuwa na maana.
 
Nape na ccm vilaza tuu, kama wangekua watu makini, wangezingatia baadhi ya hoja zitolewazo na wapinzani, siyo kwamba hoja zote za wapinzani zinalengo la kuikomoa serikali, nyingine ni za msingi, na zina umuhimu katika kuleta maendeleo, instead ya kukaa na kupembua mchele na makapi wao wanachukulia yote ni makapi. buree kabisa.
 
Zitto mbabaishaji, Mohamed Shosi alielezea vizuri "couldn't do it any better".

Hiyo ni kama muislaam kusema, msinipe urithi siutaki, wakati anajuwa hiyo ni sharia na haifutiki atapewa akitaka asitake.

...halafu miss judisi ako wapi eti?
 
Zitto anazunggumzia sitting allowance, Nape analeta ishu ya posho za safari, Kiazi kwelilikweli
 
Wachumia matumbo wa CCM matumbo moto, maana wengi wameende bungeni kuganga njaa, ulaji unapungua.

Faizafoxy, kwa hiyo unataka kusema Zitto si muisilamu safi mmana haelewi sharia inasemaje, eeh?:crazy:
 
Wachumia matumbo wa CCM matumbo moto, maana wengi wameende bungeni kuganga njaa, ulaji unapungua.

Faizafoxy, kwa hiyo unataka kusema Zitto si muisilamu safi mmana haelewi sharia inasemaje, eeh?:crazy:

Hayo unasema wewe, rejea post yangu uisome vizuri kama hujaielewa kausha. Mwenye kujuwa maana haulizi maana.
 
wewe na hafcaste akili zenu zinzfanana.vikao vinavyolipa siting alowance mtu mwenye mshahara wa laki tatu hawezi ingia.
na wewe na akili yako mbovu unalinganisha sheria kandamizi na onezi za serkali ya kifisdi na sheria za mwenyezi mungu?
ona ulivyo na laana ya kiccm na utaendelea na mawazo yako mgando mpaka sheria hiyo itakapofutwa ndipo utabaki na aibu na ushabiki wako usiokuwa na maana.

Ngoja ifutwe ndio useme. Kwa sasa bunge limemstukkia janaja yake na likamwabia NO> Chukuwa mwenyewe halafu zipeleke unapotaka.
 
[QUOTE Hiyo ni kama muislaam kusema, msinipe urithi siutaki, wakati anajuwa hiyo ni sharia na haifutiki atapewa akitaka asitake.[/QUOTE]

Hapo na wewe umepotoka mama ushungi kama Nape
 
Back
Top Bottom