Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,243
- 44,520
Hold on a minute; hii ni hoja ambayo hata mimi nimeitoa nyuma hata nilipotoa pendekezo la kuundwa Kanda za chama. Nilipendekeza kuwa Kanda ziundwe baada ya Mabadiliko ya Katiba ambayo yangeainisha mahusiano kati ya Kanda na Mikoa, Kanda na Taifa n.k. Lakini ni la muhimu kwa sababu Kanda zinatakiwa kuwa na madaraka na madaraka yanakuja kutoka kwenye Katiba.
Baraza Kuu ni kweli linaweza kuwa liliagiza kuundwa kwa Kanda lakini zikiwa na mamlaka gani? Uongozi wake unapatikana vipi? Kilichotokea kuwa baadhi ya viongozi wale wale wa kitaifa - wengine ni wabunge - wamekuwa tena viongozi wa Kanda ina defeat the whole pupose of relegating or delegating authority kwenda kwenye kanda.
Lakini kubwa zaidi ni kuwa CDM itajikuta kwenye matatizo litakapokuja suala la nidhamu (discipline); Je Kanda inaweza kusimaia nidhamu kwa viongozi wa mikoa na wilaya katika kanda hizo? Kanda zinapata wapi madaraka hayo? Madaraka hayaji kwa kuwa chombo kipo bali kwa kuanishwa mahsusi nini kinawezekana.
Nni kweli mfumo wa Kanda za CDM ni tishio kubwa zaidi la mfumo wa CCM kwani kwa wanaojua historia mara baada ya kuundwa kwa TANU kazi mojawapo ilikuwa ni kuunda Kanda za chama kwa hiyo mfumo huu si mgeni Tanzania ni CCM waliuacha. Ni mfumo unaokisogeza chama karibu zaidi na wananchi lakini siyo alama za chama tu bali pia uhuru na mamlaka ya chama.
Badala ya kumkejeli Nape kisiasa ni vizuri tujibu hoja yake kuhusu Mamlaka ya Kanda - uundwaji wake na utendaji kazi wake - yanapatikana wapi katika Katiba ya CHADEMA? Kwanini CDM na Baraza Kuu hawakufanyia maabdiliko katiba ili kuunda vyombo hivi vya kanda?
Sasa hoja hii wala haikutakiwa kutolewa na watu wa CCM kabisa; ilikuwa ni hoja iliyotakiwa kuibuliwa na wana CDM wenyewe.
Baraza Kuu ni kweli linaweza kuwa liliagiza kuundwa kwa Kanda lakini zikiwa na mamlaka gani? Uongozi wake unapatikana vipi? Kilichotokea kuwa baadhi ya viongozi wale wale wa kitaifa - wengine ni wabunge - wamekuwa tena viongozi wa Kanda ina defeat the whole pupose of relegating or delegating authority kwenda kwenye kanda.
Lakini kubwa zaidi ni kuwa CDM itajikuta kwenye matatizo litakapokuja suala la nidhamu (discipline); Je Kanda inaweza kusimaia nidhamu kwa viongozi wa mikoa na wilaya katika kanda hizo? Kanda zinapata wapi madaraka hayo? Madaraka hayaji kwa kuwa chombo kipo bali kwa kuanishwa mahsusi nini kinawezekana.
Nni kweli mfumo wa Kanda za CDM ni tishio kubwa zaidi la mfumo wa CCM kwani kwa wanaojua historia mara baada ya kuundwa kwa TANU kazi mojawapo ilikuwa ni kuunda Kanda za chama kwa hiyo mfumo huu si mgeni Tanzania ni CCM waliuacha. Ni mfumo unaokisogeza chama karibu zaidi na wananchi lakini siyo alama za chama tu bali pia uhuru na mamlaka ya chama.
Badala ya kumkejeli Nape kisiasa ni vizuri tujibu hoja yake kuhusu Mamlaka ya Kanda - uundwaji wake na utendaji kazi wake - yanapatikana wapi katika Katiba ya CHADEMA? Kwanini CDM na Baraza Kuu hawakufanyia maabdiliko katiba ili kuunda vyombo hivi vya kanda?
Sasa hoja hii wala haikutakiwa kutolewa na watu wa CCM kabisa; ilikuwa ni hoja iliyotakiwa kuibuliwa na wana CDM wenyewe.