Nape asusia kikao cha CCM

CCM ya sasa kila mtu ni msemaji wa mwisho chamani.

Ugonjwa wa saratani ya rushwa ikishapenya kwenye uongozi wa juu chamani ndio kama hivo heshima kutoweka kabisa na kila mtu kuenenda tu na lwake. Nasema mwenyekiti asiyejiheshimu kabisaaa hana tofauti hata kidogo na baba mtu mzima mwenye mji wake lakini bado ni LIKOJOZI KITANDANI.

Hata hivyo, mambo ya mafisadi tuwaachie magamba wenyewe watajiju ila ndio kama hivo wananchi tumeshaelewa wote hadi mwenyekiti wao wa taifa na unafiki wake unavyokua ni zaidi ya mzigo wa misumari ya moto kwa sehemu kubwa ya wanachama wake na uvundo huo huo sasa kusambaa nchi nzima.

Kiongozi yeyote akiwa ni kigeugeu mbaya sana, ila akiongezea na tabia wizi na uporaji wa mali ya umma kama hivi sasa hadi hapo havumiliki tena!!


 

Kaka unaweza kusema Nape ni kijana aliye jitahidi na labda wapenda mabadiliko ndani ya CCM wangempongeza. lakini uthubutu wake ulikuwa ni dhaifu na wa kukurupuka ninasema hivi kutokana na maelezo yafuatayo

EL alituhumiwa na tume ya akina mwakyembe, na hata baadae akajiuzulu kutoka ktkt nafasi yake. tangu kujiuzulu kwa EL, zaidi ya uchunguzi wa akina mwakyembe, hakuna chombo cha maadili ndani ya CCM kiliwai kumchunguza au kumhoji EL kuhusiana na utendaji wake mbovu kuhusiana na richmond, kumbuka ushahidi wa kwanza wa sababu za kumhoji ingekuwa ni ripoti ya richmond ambayo ipo bungeni. EL alijaribu kukanusha juu ya ushiriki wake wa moja kwa moja ktk richmond. lakini watendaji wa kuu wa CCM walikaa kimya. mpaka pale wapinzani walipoendelea kuzomea hayo maovu ya richmond wakitaka serikali iwaadhibu viongozi waliohusika na richmond, ndipo serikali ikaona iwa "fool" wananchi kwa kuhamisha hii kitu na kupeleka kwenye chama but this deliberately with "surface actions". kwakuwa ilikuwa ni "surface" ndiyo maana chama hakikutaka kuchunguza tuhuma zilizo mkabili EL, badala yake chama kikawa kinaongea na EL na wenzake kupitia media.kwasababu kilichokuwa kinafanyika kilifanyika kwa makusudi, na Nape ametumiwa kwenda kuongea mtaani juu ya kuvua gamba-yeye akidhani amepewa heshima kumbe anadhalilika. hata ungekuwa wewe kaka Mwanakijiji, usingejivua madaraka ndani ya chama , pasipo kusomewa mashtaka na hatimaye hukumu. El hajawai somewa mashtaka na chama, kwanini ajidhalilishe kwa kuachia ngazi?. nae Nape leo akiambiwa atoe ushaidi wa makosa ya EL, na adhabu anayostahili ndani ya chama kwa mujibu wa taratibu za chama anaweza kutoa?.
ninamwona Nape ni kijana dhaifu na asiye makini, huwezi kujenga maadili ya chama kwa kuzungumza kwenye media eti kisa wewe katibu mwenezi, haiwezekani . tuwe wakweli, Kaka Mwana kijiji unafahamu mgogoro wa ndani ya Chadema wakati ule wa uchaguzi, wakati Mh. Kabwe anataka kugombea uenyekiti, si uliwaona walivyo handle mambo yao?walikuwa wanalopoka ovyo kama hiki chama chetu CCM?. nape hana tofauti kubwa na yule katibu wa CCM aliye staafu juzi hajui anachokifanya. I would expect a creative and innovative Nape, one whose thinking is based on logic and not intuition!. nasema hivi kwasababu ktk mahubiri ya magamba , Nape alikuwa anatumia hisia na siyo logic. EL aliyafahamu mapungufu yote yaliyopo ktkt kushughulikia tuhuma zake. na sasa EL anatumia u mbumbumbu wa Nape kutafuta kufuta ukweli wa tuhuma zake.
kwenye NEC kusingepatikana mtu wa kumpongeza Nape kwakuwa wanajua Nape anatolewa sadaka, aidha walishafahamu hilo siku nyingi. lakini lililo kubwa ni kuwa hawana nia ya mabadiliko, CCM inalelewa na vyombo vya dola na siyo mission yake kwa wananchi.

kumbuka nilikwambia pasipo na kiongozi makini , hali haiwezi tulia. Jambo laweza kuibuliwa na yoyote, lakini kiongozi lazima awe na uwezo wa kulimaliza na kulifunga, hatimaye kuendelea na mengine. mpaka sasa mgogoro wa makundi na magamba una gharimu CCM, kumbuka migogoro hii inatumia pesa,inatumia muda, wanakaa vikao kujadili yasiyoisha, hawana muda wa kujenga chama, hawana muda wa kupanga maendeleo, na wao ndo "wameshika hatamu" – na nchi yetu haiwezi kuendelea
 
Nape amekumbana na tatizo lile lile ambalo wengine tumeliona muda mrefu uliopita - CCM haibebeki, haikoleki na mtu yeyote anayejaribu kuiokoa anaweza kujikuta kwenye matatizo makubwa zaidi. Kwa sababu tazizo la CCM ndani ni zaidi ya watu (personalities) na ni zaidi ya maslahi (interests) na kwa kweli kabisa ni zaidi ya matamanio (ambitions). Tatizo lake limefungamana moja kwa moja na tunu, mitazamo, na itikadi ya Chama. Haiwezekani kuisafisha CCM bila kugusa huku. Ndio maana mwisho wa siku naamini kama Nape aliyoyoasema aliamini yalikuwa sahihi na kuwa alikuwa anasimamia maamuzi sahihi ya Chama na dhamira yake ikimthibitisha anabakiwa na uchaguzi mmoja tu - kutoka kwa heshima.
 



Mkuu,
Naheshimu sana mawazo yako. Hasa pale uliposema kuwa hukuwahi kuzungumzia kuhusu Nape.

Ukweli upo wazi. Ccm haiwezi kubadilika na haiwezi kubadilika kabisa pale anayeongoza mabadiliko anapokuwa ni kijana. Nape alieelezwa hayo tangu awali. Akaishia kujibu wanaomtahadharisha kwa mipasho na taarab. Leo yamemkuta. Alikuwa anahubiri mafisadi wajivue gamba (kitu ambacho wapenda mabadiliko/maendeleo tunakikubali) leo yeye ndiye anatakiwa kuvuliwa gamba. Laiti angesikia sauti zilizokuwa zinamshauri, leo yasingemkuta!

Sasa anatakiwa kufanya maamuzi magumu. Aondoke kabisa kwenye hicho chama maana imedhihirika kwamba wana mtazamo tofauti. Hiyo ndio njia pekee itakayomrudishia hesima yake kisiasa. Otherwise atapotea kabisa kwenye ulingo wa siasa na anayoyaamini yatakuwa yamekufa nae!
 
Nilishawahi kusema humu ndani ya JF kuwa watanzania bado hawajawa huru na bado tunapigania demokrasia. Ukiisaliti demokrasia ya Tanzania especially kwa miaka hii, na yenyewe pia itakusaliti. It's just a matter of time Nape atadai kuwa ni victim...watch.
I'm prepared to be corrected.
 
Hamu sina wana jf kumbe wengi wenu Nape alikuwa akiwaboa sana hasa anapomtaja EL?
 

Mi nna ushauri mmoja tu kwako..jifunze kuandika!!manake ulichokiandika hapo juu hakika hakieleweki..loh!
 
sifa mojawapo ya wana ccm unatakiwa ufanane na huyu kiumbe nape kesho utamusikia
 
Hamu sina wana jf kumbe wengi wenu Nape alikuwa akiwaboa sana hasa anapomtaja EL?

Binafisi sikuwa nakwazika bali nilikuwa ninamuona Nape kama mmoja wa wasanii na waganga njaa ambao wakishapewa ulaji wanatulia na kuanza kuimba mapambio ya kusifia mfumo kwamba ni mzuri sana.

Kila siku huwa ninasema kwamba huwezi ku-isolate ufisadi wa individuals ndani ya CCM kwa kuwa viongozi wengi kama sio wote ni wanufaika wa ufisadi, wameshiriki kwa njia moja au nyingine, ama individually au kama Chama. Ndo maana kesi za EPA zimebaki kuwa ni masimulizi tu na haswa kwa wanufaika waliozipeleka kwenye chama.

Nape alitaka kupata umaarufu kwa "Operation Vua Magamba" sasa naona imegoma. Ili kumuonyesha kwamba uongozi wa CCM ni Gamba Kuu, alipigwa stop na CC asiende Igunga kwenye kampeni na ilihali yule aliyejivua gamba akipewa nafasi ya kushiriki kwenye kampeni. Hilo lilikuwa ni tusi kubwa sana kwa Nape na baada ya hapo alitakiwa kuwa makini.

JK baada ya kuona chati ya CCM imepanda ghafla, alitamka kwamba, "kile anachosema Nape, ni maelekezo yenye baraka kutoka kwenye uongozi wa juu wa CCM". Nape alikuja hapa na kujitapa kwamba tumemsikia Mwenyekiti kwa kinywa chake.

Ili kuonyesha kwamba alikuwa na dhamira ya kweli ya kupambana na mfumo huo aachie ngazi kwa kuwa kile alichokuwa akiwaahidi vijana kwamba amedhamiria kukishughulikia kimemshinda na sasa kibao kinamgeukia. Yeye alikuwa anawatuhumu mafisadi na sasa nao wamemgeuzia kibao kwamba anawapaka matope na kuwatukana.

Nape na akina Samweli Sitta, Mwakyembe, Kilango, Sendeka, Lembeli, Manyanya na wengineo wanaotumia kete ya kupambana na ufisadi, ni wanafiki tu. Hakuna mpambanaji wa kweli ndani ya CCM, wengi wao ni waganga njaa tu na wachumia matumbo.
 

Namsikitikia ila hayo ndiyo malipo anayopata kwa kutokuwa na akili za kutosha.
 
Kijana alifanya kile alichoamini, na ambacho watanzania wengi wakiongozwa na wapinzani pia waliamini kuwa ndicho kilichoiangusha CCM katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2010. Kijana aliongea kwa moyo kwa kuamini, na wengi waliamini kuwa ukombozi pekee wa CCM ni kuwaondoa watu ambao wamekuwa wakitumia madaraka waliyonayo kwa manufaa yao binafsi. Kuondoka kwa akina Makamba ilikuwa kama changamoto na ufunuo mpya kwa watu wote walioamini kama ambavyo Nape alikuwa akiamini. Nguvu ya chama na kukubalika kwa chama kwa wananchi na kupunguza nguvu ya upinzani ni kusafisha chama kwa kuwaondoa watu wote waliokipaka chama matope, watu waliosababisha CDM ikawa na nguvu katika uchaguzi wa mwaka 2010, na watu waliosababisha mgawanyiko mkubwa katika kura za maoni mwaka 2010. Kwa wanaoelewa na hata uongozi wa juu wa CCM unakiri kabisa kwamba matatizo yanayokikabili CCM yanatokana kwa kiasi kikubwa na mambo hayo. Sasa kijana alisahau watanzania wengi ni Njaa tu. Nilikuwa nikisoma magazeti kuwa pesa ilitembea, pesa ilitumika, na CCM ni pesa na kwa mwenye nazo CCM ndio mtawala wa Chama. Nape na wenzake walikuwa wanatumia pesa za chama, na hawa wengine wanatumia pesa za nani? Mzee MMJ naafiki na ushauri wako wa mwisho kuwa ndugu huyu ananjia moja tu iliyobakia, je anaweza kuifuata njia hiyo? Ni njia ngumu sana kwa mtu mwenye ndoto za kisiasa. Kuna ndugu zetu waliwahi kufukuzwa CCM sasa ndio hao, they came back, how did they do that? and what do they stand for now? Hata hivyo haki wakati wote huwa inashinda siku za mwisho, tutacheza sana libeneke sasa hivi lakini Chama chochote cha siasa kitashinda kama kitakonga nyoyo za wananchi. Madhumuni ya chama cha Siasa ni kushika dola, na sio rahisi kila wakati yatumike mabavu, ulaghai au njama ili kufikia adhima hiyo, itafikia kipindi CCM wataona umuhimu wa wananchi, hope this will happen before it is too late.
 
Ndio maana mwisho wa siku naamini kama Nape aliyoyoasema aliamini yalikuwa sahihi na kuwa alikuwa anasimamia maamuzi sahihi ya Chama na dhamira yake ikimthibitisha anabakiwa na uchaguzi mmoja tu - kutoka kwa heshima.
Mwanakijiji kutoka CCM kunahitaji uaminifu sifa ambayo sidhani kama Nape anayo, kutoka CCM kunahitaji kuwa jasiri sifa nyingine ambayo sidhani kama Nape anayo, kutoka CCM kunahitaji utulivu wa mawazo sifa ambayo mtu mkurupukaji kama Nape nina hakika hana na kutoka CCM kunahitaji uwajibikaji ambao Nape ameonyesha si mara moja kuwa hata dalili yake hana.

Ndani ya CCM hivi sasa naamini hakuna mtu hata moja mwenye sifa hizo na kama alikuwapo ameshaathirika kiasi cha kupoteza hata kile kiduchu alichokuwa nacho awe kiongozi wa chama, kiongozi wa serikali au mwanachama wa kawaida. Mtu yeyote ambaye anaamini kuwa wakifukuzwa watu wawili watatu, CCM itatakasika hawezi kuwa na hekima ya kutoka CCM kwa heshima.
 

Tatizo atoke aende wapi? Shida wengi bongo hatuna option B. Namshauri akomae humohumo apigane kiume na apambane nao kisawasawa vinginevyo atasahaulika kwenye medani za siasa za bongo.
 
Elimu + utashi ni vitu muhimu katika maisha ya leo ya binadam.Hivi ummpa fursa ya kujitambua na kutenda kulingana na hali iliyopo.CC na NEC waliomo wengi aidha wanakosa elimu ama utashi hivyo kutizama matumbo yao pamoja na ombwe la uongozi.

Siamini katika usafi wa Lowassa hata kidogo.Ni nini mtu huyu anachotaka kwetu sisi? Kuwa RAIS? Hapana tunapaswa kumuogopa kama ukoma maake tamaa aliyonayo si dhahiri kwamba ana nia ya dhati kuwatumikia watanzania.Huu ni uchu uliopita kiasi,kwani ali-resign ili atokee mlango wa nyuma? If that is the case hapa kuna tatizo tena kubwa.

Hakuna anayethubutu kuprove kuwa Lowassa ni msafi zaidi ya kudai samaki mmoja akioza uoza wote!Taarifa ya tume ya Mwakyembe ni ushahidi tosha na iwapo anabisha/kupinga juu ya hayo alete utetezi wake against Mwakyembe tume na si bla blaa za kisiasa ili kupata huruma toka kwetu.Typical agenda ili kuwa juu ya hali ya kisiasa nchini,ghafla akaibuka na mambo yake binafsi hundred percent na kusahau juu ya Taifa kwanza huu si ubinafsi ni nini? Eti anajisafisha na kuungwa mkono na wezi wenzake kama Sumaye.

Binafsi naitizama CCM,CC na NEC yake kama wanacheza ngoma wasio ijua.Nadhani ni wakati wa kufa kwake kwani sikio sasa halisikii dawa.Huwezi kutoa maamuzi rahisi rahisi kwa gamba la Lowassa etal.Kamati ya Maadili inauwezo wa kuchunguza madhambi ya Lowassa zaidi ya kamati ya akina Mwakyembe? Au ni njia za kutafuta huruma za kisiasa na kuwapumbaza watanzania.

Hapa sijaafiki juu ya yaliyotokea ndani ya CC na NEC ya CCM, to me its a biggest disappointment i had ever seen na ni fedhea kwa wenye nia njema na chama pamoja na nchi kwa ujumla.Kikwete tuambie juu ya hiyo hidden agenda yako na Lowassa na wala si ''ukigeu geu'' wa huku Nape tuko pamoja (diamond jubilee) upande mwingine Lowassa hatukukutana barabarani.Msingi wa maamuzi magumu si ''kucheka cheka'' kwani body language means a lot.

Ilikuwa muhimu kushughulikia matatizo haya sasa ili kama ni kuvurugana kuonekane mapema na kudhibitiwa before 2015.Ushauri wa jaji Bomani kuwa CCM isubiri uchaguzi wa mwakani ili iweze kujisafisha ni sawa na kutokipa kidonda dawa na kuacha kiendelee kuoza.

Ni dhahiri uchaguzi mwakani ndani ya chama ni timu ya ushindi, hivyo hapa ndipo mafisadi watatumia fedha zao kupanga safu ya kutimiza matakwa yao.Hili ni pigo kwa Chama pamoja na wazalendo wa nchi hii.

Nape simlaumu sana ila nae kajisahau kupita kiasi hasa baada ya kupanda juu.Siku moja nimezungumza nae na nilichokibaini ni kuwa si kiongozi bora na ni kijana tu kwenye upepo wa siasa.Madaraka aliyopewa anayaona ni makubwa kiasi cha kujitenga na vijana wenzake ''eti aliniambia ,kama ni ushauri nataka kumpa nimpe kupitia facebook ama ani assign mtu wa chini yake kwani yeye yuko busy sana''.Huyu ni kijana anayejiita mpambanaji katika dunia ya changamoto kama hii anayedhani ukosoaji ni upinzani tu.

Majibu yake hata humu Jf ni ya kejeli na yasiyoendana na hadhi yake kwa maana ya nafasi aliyonayo.Real ni ya mtaani kabisa.Huyu sina comment sana nae, ngoja asonge kwa silaha aliyonayo uwenda akashinda vita hiyo isiyo na maono.
 


Taaaaaaaaaaarrrrrrrrrrrrrrrrraaaaaaaaaaaaaaaaatttttttttttttttttiiiiiiiiiiiiiiiibbbbbbbbbbbbbbbbbuuuuuuuuuuu?

Kwa wenye ufahamu huu ndio mwanzoooooooooooo.!!!!!!!!!!!!!1
 

Uko sahihi kaka,option ni yake sisi wengine ni kumuunga mkono tu ila sio yeye tu yupo mzee wangu chiligati huyu ana heshima sana sasa leo kuvunjiwa heshima ndani ya kikao ni aibu kwake.Nilichosikia kama ni kweli mkiti amekubali kuwachukulia hatua za kinidhamu wakina chiligati basi watoke mapema tena kwa heshima zao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…