MSAGA SUMU
JF-Expert Member
- May 25, 2015
- 6,478
- 20,390
Wakati wakina Lema na Chadema wakishinda mitandaoni kusaini petition kadhaa wakitaka Diamond afungiwe, Profesa Jay yeye anapiga show na vijana waCCM (Nandy, Diamond , Weusi nk). Wasanii ambao kwa mujibu wa Chadema ni moja ya watu waliotumika kuingiza mamlakani utwala dharimu wa CCM.
Wakati makamu mwenyekiti anatuma kwenye magrupu ya whatsapp watu washare katiba mpya, prof anaweka pembeni hizo post kisha anapost kwanza show zake, na kudharau maamuzi ya chama ya kuhusu suala la katiba mpya. Huu ukosefu mkubwa wa nidhamu wa Prof kkwa chama bila shaka unaashiria profesa anataka kwenda CCM kusimamimsha uchumi kwanza maana katiba mpya inaweza kusubiri.
Mimi binafsi naona Profesa Jay ni moja ya mfano mkubwa wa kuigwa kwa vijana. Maisha ya Profesa yanatufundisha kuwekeza sehemu nyingine pale tunapokuwa na nyadhifa za kisiasa ili siku unapozipoteza maisha yaendelee, Leo hii tofauti na Msigwa na Heche yeye maisha yake yanaendelea kama kawaida.
Unapokuwa umewekeza nje ya siasa maisha yanaendelea hata unapokuwa nje ya mfumo, yaani unalipa bili zako bila shida.
Karibu sana nyumbani Jay