Naona kama dunia nzima imeniangukia

Naona kama dunia nzima imeniangukia

ungekuwa Mbeya ningekutafutia mteja Wa gari,viwanja siku hizi havitoki kiivo!!!!gari inaweza toka japo kwa bei mbovu!
 
Mkuu inabidi uza hata hiyo gari. Na hiyo ni wake up call unahitaji kuwa na income ya ziada nje ya kazi.Uzuri imekuja wakati ambapo majukumu hayajawa mazito. Mkuu itabidi hata ufikirie mradi wa kama genge la nyanya na uanze kuweka akiba ya fedha pale utapopota kazi isiyozingua. Wanashauri inatakiwa uwe atleast na mishahara ya miezi sita mpaka mwaka. Pole sana kwa matatizo ila ni wakati wa kujiongeza. Sasa hivi ni vyema ukaiweka tu hii gari sokoni hata kwa bei ya hasara, nusu ya hela fungua ka mradi hata ka genge, inayobaki jitahidi kuihudumia familia katika miezi hii ambayo wife ni mjamzito. Punguza matumizi ambayo ni unnecessary. Hakikisha una chakula ndani hilo ndo jambo la msingi kuliko yote. Suala la kodi kama ukiongea na mwenye nyumba ukalipa hata miezi mitatu itakuwa vyema. Sijui nyumba unayokaa ni ya gharama gani. Ila cha msingi ni kutatua tatizo ulilo nalo mkononi wakati ukifikiria suluhisho la kudumu,. We ni mwanaume komaa tu.. Wanaume tunakomaaga hata mambo yawe magumu vipi..Utatoka tu kwenye hili.
 
Life is hard but bot impossible keep working mzee mengine ni majaribu tunayapitia ili kuona uwepo wa Mungu hapa duniani
 
Ukiona hivyo ujue mafanikio makubwa zaidi yako hapo jirani. Usikate tamaa, muombe Mungu thrn songa mbele
 
Dah sometimes mtu unawezajiona unashida kuliko kiumbe chochote hapa duniani,lakini ukikutana na mwenye shida unajiona huna shida.

Hapa ndio unapo aply rule msemo usemao''Ukitaks kumshukuru Mungu wako basi muangalie aliechini yako" ...Pole sana mkuu yatakwisha.
 
Toka zamani ukioa Kama huyajui au uwezo huna mke alikuwa akijifungulia kwa wazazi wake kuna wakunga wa jadi kwenye koo waweza handle complications zingine kuliko madaktari bingwa waliosoma marekani kwa Trump. Huyo mwanamke asije kufia mikononi wapelekee waliomzaa
Yani ww!!
 
Dah sometimes mtu unawezajiona unashida kuliko kiumbe chochote hapa duniani,lakini ukikutana na mwenye shida unajiona huna shida.

Hapa ndio unapo aply rule msemo usemao''Ukitaks kumshukuru Mungu wako basi muangalie aliechini yako" ...Pole sana mkuu yatakwisha.
Amina
 
Ukiona magumu yanazidi tambua kuwa neema ndio inakaribIa.
 
Wakuu poleni na majukumu,

Nina umri wa miaka 34, mke na mtoto mmoja, nimepambana kweli kweli miaka 4 nyuma nimejenga kijijini kwetu nimenunua kiwanja pembeni kidogo ya mjini, nimemsomesha mke wangu kamaliza mwaka Jana, miaka 2 nyuma niliona mambo sio mabaya nikavuta kausafiri ka kunisaidia hapa na pale.

MATATIZO YANAANZA. Mwaka Jana nilibadilisha kituo kipya (sekta binafsi) kwa ahadi ya mshahara mkubwa. Dah mambo yakawa sio mambo mshahara ukawa hutoki mpaka miezi 3 hafu tunapewa nusunusu kumbuka hapo wife ameshakuwa mjamzito mimba inamsumbua kweli, mtoto anasoma na nadaiwa kodi ya nyumba. Ilinilazimu kuacha kazi baada ya kuvutana sana basi sikulipwa mishahara miezi mitatu katikati ya mwezi wa 5 nikapata kazi sehemu nyingine japo kwa mshahara mdogo nikalipwa mshahara nusu kwa vile nilianza katikati.

MAAJABU MENGINE HUKU. Leo in trh 4 July hatujalipwa mshahara wa June ninapoandika Uzi huu nimekaa jirani na nyumbani nafikiria nitaingiaje nyumbani kwa mke wangu, anaweza kujifungua muda wowote kuanzia sasa na ana complications, Jana ni kama vile tulilala njaa, leo mama na mtoto sijui wamekula nini, shule zimefunguliwa sina ada ya mtoto, mwenye nyumbani anadai kodi tena atakuwa ananisubiri nyumbani, nimejaribu kuuza gari na kiwanja lakini hakuna wateja. Nina mawazo sana ndugu zangu, ninachoogopa zaidi ni huyu mama mjamzito.

Ushauri wenu na sala zenu.
Gari lako ni aina gani na unaliuza shilingi ngapi?
 
Pole sana mkuu, ugumu wa maisha umetuangukia watanzania wengi sana japo yanazidiana hatupaswi kukata tamaa!! Rudi nyumbani huwezi kukimbia kwako rudi ukashauriane na mkeo,naamini yeye atakupa Mawazo mazuri zaidi na faraja
 
Mkuu huyo jamaa tunajua akili zake mpuuzie!!

Kwa sababu una gari na kiwanja kwanin usitangaze humu jf ili uuze??

Pia kama unaweza waambie wafanyakaz wenzako na kama ikiwezekana m-face boss wako mwambie hali halisi ili akiweza akupe pesa mkatane kwenye mshahara!!

Labda nikuulize...kazini hamna bima ya afya?? Kwanin usiitumie kwa ajili ya matibabu ya wife??

Pole sana mkuu!! Mungu akupe wepesi!!
Mkuu inamaana haukusoma kuwa kampuni yake mpaka Jana tarehe 4 ilikuwa haijalipa wafanyakazi mishahara ya june? Sasa unahisi wanaweza kumkopesha fedha nyingi?
 
Pole sana Samjom kwa changamoto unazopitia....
Nakubaliana na wanaosema, kama kuna ndugu/rafiki anaweza kukushika mkono, tafadhali usiache kumwambia.
Mazingira kama hayo ndipo unapomjua ndugu / rafiki akufaaye. Pole sana, Mungu afanye njia.
 
Mtu anataka ushauri/mawazo yetu mnakazana kumpa pole watanzania bhana.Ushauri wangu kama una nyumba na gari basi nenda kachukuwe mkpo haraka benki ili uweze kutatuwa matatizo hayo kwa haraka alafu badaye you will pay kidogo kidogo
 
  • Pole sana kaka pole mnoo nakuonea huruma. Fanya maarifa yoyote mkuu. Kwanza ongea na mwenye nyumba maana akirusha mizigo unaweza kuchanganyikiwa usiweze cha kufanya. Mwenye nyumba ni binadamu atakusikiliza ili usikose sehemu ya kuja kupumzika dili zikikwama huko juani.
 
Mkuu inamaana haukusoma kuwa kampuni yake mpaka Jana tarehe 4 ilikuwa haijalipa wafanyakazi mishahara ya june? Sasa unahisi wanaweza kumkopesha fedha nyingi?
Nimesoma mkuu!! Sio kampun...na hata kama kampun haina pesa boss anaweza msaidia!! Sizan kama ana uwezo atashindwa mkuu!
 
Pole sana jamaa, mimi navyoona usiuze Gari. Uza Kiwanja. Kitangaze Fb. Tungekuwa tunaaminiana humu tungepeana namba, lakini kwakweli huwa hatuaminiani.

Nimeshauri uuze kiwanja badala ya Gari. Hii ni kwasababu Gari itakusaidia mizunguko ikiwemo kumpeleka mkeo hospitali. Kiwanja utanunua Kingine bali ikitengemaa.
 
Back
Top Bottom