Naona kama dunia nzima imeniangukia

Naona kama dunia nzima imeniangukia

Mbona hukujibu? Upo makini kweli? Hiyo gari ni aina gani? Bei gani? Na kiwanja kipo wapi? Ukubwa gani? Bei gani? Utasaidiwaje sasa kama hutaki kujibu?
 
matatatizo tumeumbiwa binadamu hasa wanaume,pole sana kaka mungu ataonyesha njia
 
Usafiri uliuza? Mnakimbilia kununua usafiri badala ya kuwekeza sehemu uwe unaingiza pesa, huo usafiri toka umenunua umekutengenezea kiasi gani cha pesa? Hivi kwa mfano hiyo pesa uliyonunulia usafiri ungekuwa umewekeza kwa kufungua duka leo hii ungeona maisha magumu? Lkn kosa jingine ulinunua usafiri badala ya kujenga hata vyumba viwili na sebule kwenye uwanja wako uachane na maswala ya kulipa kodi ww ukaona raha kuwa na usafiri huku umepanga hela zenyewe mshahara mwisho wa mwezi, tena kampuni/taasisi/kazi za watu binafsi. Ulikosea sana tena sana. Pambana kwa hali yako, dunia haijakuangukia ila ww sio rafiki wa dunia hii kwasababu ulishindwa kusoma alama za nyakati, na kwa kipindi hiki namba lazima uisome. I'm sorry kama nimekukera ila sinaga maneno matamu kwa makosa yaliyokuwa yanaepukika kama haya. Lkn bado una nafasi ya kufika uendako, wakeup
 
Umeingia kwenye huo uzi? Kama ni kwenye app unaanza na [ B ] halafu maneno unayotaka kuandika ndio yafuate lakini hiyo B uibanishe kwenye mfumo huu [A] sio kama nilivyoacha hapo space kidogo
Ok let me try..[Mambo][Joseverest]like this
 
Wakuu poleni na majukumu,

Nina umri wa miaka 34, mke na mtoto mmoja, nimepambana kweli kweli miaka 4 nyuma nimejenga kijijini kwetu nimenunua kiwanja pembeni kidogo ya mjini, nimemsomesha mke wangu kamaliza mwaka Jana, miaka 2 nyuma niliona mambo sio mabaya nikavuta kausafiri ka kunisaidia hapa na pale.

MATATIZO YANAANZA. Mwaka Jana nilibadilisha kituo kipya (sekta binafsi) kwa ahadi ya mshahara mkubwa. Dah mambo yakawa sio mambo mshahara ukawa hutoki mpaka miezi 3 hafu tunapewa nusunusu kumbuka hapo wife ameshakuwa mjamzito mimba inamsumbua kweli, mtoto anasoma na nadaiwa kodi ya nyumba. Ilinilazimu kuacha kazi baada ya kuvutana sana basi sikulipwa mishahara miezi mitatu katikati ya mwezi wa 5 nikapata kazi sehemu nyingine japo kwa mshahara mdogo nikalipwa mshahara nusu kwa vile nilianza katikati.

MAAJABU MENGINE HUKU. Leo in trh 4 July hatujalipwa mshahara wa June ninapoandika Uzi huu nimekaa jirani na nyumbani nafikiria nitaingiaje nyumbani kwa mke wangu, anaweza kujifungua muda wowote kuanzia sasa na ana complications, Jana ni kama vile tulilala njaa, leo mama na mtoto sijui wamekula nini, shule zimefunguliwa sina ada ya mtoto, mwenye nyumbani anadai kodi tena atakuwa ananisubiri nyumbani, nimejaribu kuuza gari na kiwanja lakini hakuna wateja. Nina mawazo sana ndugu zangu, ninachoogopa zaidi ni huyu mama mjamzito.

Ushauri wenu na sala zenu.
Kwani mnashinda njaa mkuu? Hiyo pesa ya mafuta ya gari save kiasi kwa ajili ya mkeo atakapojifungua,gari paki panda public transport kwenda kazini. Ukiona mambo bado magumu uza hiyo gari kwakuwa ni likability inakamua pesa. Kiwanja usikimbilie kuuza fanya mpango wa kukijenga hata nyumba ya vyumba vitatu uishi kwako na mkeo
 
ndo maana ulifeli mtihani ya ufahamu;pitia sms yake upya utamwelewa
*mtihani ya ufahamu = mitihani ya ufahamu.

Toa ushauri sio kejeli. Ushauri wako hauna maana kama unautoa kwa kejeli kwa anaeomba ushauri.
 
Ivii we jamaaa matatizo unayajua???mtu unamiliki gari,nyumba na kiwanja alfu unalia kma ivi acha kumkufuru muumba
 
Duuh wanaume tumeumbwa matesoo! Ila mateso haya kuna mkono wa mtu sio bure
 
Bei gani hiyo gari?ni aina gani? Fanya fasta!
 
Daaah pole sana mkuu, endelea kutafuta wateja na pia washirikishe ndugu ambao unahisi watakusaidia
 
Back
Top Bottom