Naona kama dunia nzima imeniangukia

Naona kama dunia nzima imeniangukia

Pole mkuu..
Kweli ukisema uko na shida, kuna mwenye shida zaidi... Mungu akutangulie mkuu..

Jaribu kuwasiliana na ndugu zako wa Karibu wakuwezeshe kipindi hiki kigumu
 
Huko kwao hospitali hazipo? Wapelekee wenye mtoto wao waliomzaa asije kufia mikononi mwako Na ulofa wako. Asikufie mikononi warudishie waliomzaa na ueleze wazi kuwa ana complications na wewe sio mkunga wala doctor na pesa huna
Uwezo wako wa kufikiri umeishia hapa?
Mwenzio anataka kujitegemea ww unataka umfanye tegemezi. Aende nyumban kufanya nn?
 
Pole Mkuu, pole sana...kwa kweli nimeshindwa hata kukupa like katika posti yako (nafsi inanisuta) ni kama vile nitakuwa nafurahia yaliyo/yanayo kukuta.

Najaribu kuwaza, labda pengine una ndugu ama rafiki wa karibu, jaribu kijishusha.... wafuate na uwaeleze swala zima, hususani mazingira yanayo mkabili SHEMEJI, dada, shangazi yetu, naamini unaweza kupata ama kutoka na ushauri utakao leta ufumbuzi wa tatizo.

Sijui pengine labda unapatikana MKOA gani...!

Naweza kukupa ushauri mwingine kuendana na MAZINGIRA.
 
Hawa sio wazee wa Assist? Pole mkuu ndio maisha ya mwanadamu ni mafupi nayo yamejaa tabu tu

Nitakuombea
 
Wakuu poleni na majukumu,

Nina umri wa miaka 34, mke na mtoto mmoja, nimepambana kweli kweli miaka 4 nyuma nimejenga kijijini kwetu nimenunua kiwanja pembeni kidogo ya mjini, nimemsomesha mke wangu kamaliza mwaka Jana, miaka 2 nyuma niliona mambo sio mabaya nikavuta kausafiri ka kunisaidia hapa na pale.

MATATIZO YANAANZA. Mwaka Jana nilibadilisha kituo kipya (sekta binafsi) kwa ahadi ya mshahara mkubwa. Dah mambo yakawa sio mambo mshahara ukawa hutoki mpaka miezi 3 hafu tunapewa nusunusu kumbuka hapo wife ameshakuwa mjamzito mimba inamsumbua kweli, mtoto anasoma na nadaiwa kodi ya nyumba. Ilinilazimu kuacha kazi baada ya kuvutana sana basi sikulipwa mishahara miezi mitatu katikati ya mwezi wa 5 nikapata kazi sehemu nyingine japo kwa mshahara mdogo nikalipwa mshahara nusu kwa vile nilianza katikati.

MAAJABU MENGINE HUKU. Leo in trh 4 July hatujalipwa mshahara wa June ninapoandika Uzi huu nimekaa jirani na nyumbani nafikiria nitaingiaje nyumbani kwa mke wangu, anaweza kujifungua muda wowote kuanzia sasa na ana complications, Jana ni kama vile tulilala njaa, leo mama na mtoto sijui wamekula nini, shule zimefunguliwa sina ada ya mtoto, mwenye nyumbani anadai kodi tena atakuwa ananisubiri nyumbani, nimejaribu kuuza gari na kiwanja lakini hakuna wateja. Nina mawazo sana ndugu zangu, ninachoogopa zaidi ni huyu mama mjamzito.

Ushauri wenu na sala zenu.
Pole Sana mkuu
 
Asante kwa busara zako mkuu.nianze na gari ni raumu namba DAM nikipata 7.5m saws tu.nitafanye sasa.kuhusu bima sector binafsi hazijali hivyo sina.nitajaribu kuongea na bosi wangu japo no mtata sanaaaa
Mkuu sidhan kama umepata matatizo kiasi hicho. Mwenye matatizo angekuja akiwa ameshaweka bond ama anahitaji kuuza gari ama kiwanja. Yaan wewe una assets bado unang'aa macho. Vipi kuhusu sisi wenye shida zaidi yako na hatuna asset? Mkuu una matatizo lakini wengine wanayo zaidi na hawana popote pa kushika.
 
Dah.... Una gari... Una kiwanja... na zaidi una muda wa kuja kulialia hapa JF.... Bila kumung'unya maneno... Ungekuwa Shem wangu ningekutandika makofi kisha nikaondoka na dada yangu[emoji13] [emoji13]
 
Dunia ikikuangukia unasimama unasonga nayo tu
 
Daaa pole sana, hiyo gari aina gani haiwezi kuuzika? Upo dar? Kiwanja kipo dar?
 
Daah hiyo gari hingekua ist ningekuunga mkono mdau
 
Pole bwana na MUNGU akukomboe kwenye hili.fanya hivi

1.kama nyumbani kwa wazazi wa mkeo si mbali mpeleke na muache hapo kwa muda na makubaliano na wazazi kua akijifungua na kupona utamfata.na hakika hilo halitashindikana

2.nenda bank yoyote hasa Access bank ukalikopee hilo gari lako iwapo imekua ngumu kuliuza.maana una dharula,kajieleze vizuri huku ukiwa na kadi ya gari lako na vitambulisho vyako vya kazi,tengeneza kuaminiwa ili usikwame.

3.mwenye nyumba mfate bila woga na umueleze wazi wazi kama mwanaume kua awe mvumilivu na utampa pesa yake.atakuelewa na hata akiwa mkali hatafanya jambo maana nchi hii iko kisheria.hatakufukuza ghafla na kudhalilika,kama ni kukufukuza atakupa muda wa miezi mitatu na ikiwa hivyo utakua umeshajipanga

4.nenda shuleni pia kamweleze mkuu wa shule au mkurugenzi kama shule ni binafsi akupe muda kidogo.naamini pia kwa uliyoyasema hapa ukiyasema pia shuleni utaeleweka na watakupa muda hata kama ni wiki mbili na ktk kipindi hicho MUNGU atakua keshafanya yake iwapo pia unamuomba kwa moyo na imani thabiti bila uchafu wa roho na mwili

5.nitakukuombea pia leo usiku.

JAH RASTAFARI MORNING AFRICA
 
Angekuwa ana mpango wa kujitegemea toka mwanzo angejipanga asingesambaza mikadi kibao ya kuchangiwa aoe tena yenye viwango Na kuweka vikao kibao watu wamchangie aoe yaani atongoze yeye kumbe lofa hela hana hata kuoa anategemea donations. Sasa Kama alikuwa lofa wakati wa kuoa hadi akaoa kwa michango ya ndugu na marafiki sasa Kama ni lofa hadi sasa hawezi uguza mkewe ajifungue mwanae si awarudishie tu huyo mkewe wazazi wake? Sababu inaonyesha wazi kuwa ulofa kwake toka kuoa hadi mimba hiyo ya mkewe haujamtoka. Naomba mpelekeeni Pole mkewe kwa kuolewa na lofa ambaye hata kuoa alichangiwa
Kasema vitu alivyotaka kuuza havijapata mteja.
Kwahiyo lengo la kuja hapa siyo kuomba hela ni msaada wa mawazo au kununua vitu vyake.
Ndiyo tatizo la kuwa na akil za kibashite. CCM WANASUMBULIWA NA LAANA YA RAMBI RAMBI
Unakurupuka tu kama mwenyekiti wako alivyokurupuka kweny samaki na Acacia.
Nataka nione km kweli atapewa hizo trilion 104. Asipopewa litakuwa bonge la ki...la..za
Usikurupuke tu km kadikiteta uchwara
 
Duh,mke pale mgonjwa,ada july hii hujalipa,kodi ya nyumba mtihani,na mshahara bado unauchungulia km umeingia na kila mara unakuta balance ipo under 10k,pole sana ila sababu ni mwanaume bas naamin kila kitu kitakua sawa soon.

Kwanza chukulia matatizo ni sehem ya maisha na ni ladha inayoyafanya maisha yawe kama maisha,ila tu yamekukuta wakat mambo meng yameingiliana pole

Una gar,sawa umeipark au inatembea,na kama inatembea kwenda kazin unatumia kiasi gan kwa mafuta? Kama umeipak sbu ya kukosa mafuta sawa ila kama bado unaitumia ntakulaumu,maana haiwezekan ukose hela ya kula ilihali gar inawekwa mafuta,japo hujasema ila ukwel u anaujua zaid kulko ss

Labda nikushauri kdgo cha kufanya japo sikulazimshi kufanya,angalia hapo ndan kwako kipi chepes cha kuuza,najua weng wamekushaur uuze gar au uliweke bond sawa una hiari,wengine wakashaur mrudishe mwanamke kwao sawa pia una hiari,na wengine wamesema uza kiwanja pia una hiari lakin je ukishauza utakua umesolve tatizo au umeongeza? Sawa kimfaacho mtu chake bt je ukiuza unadhan matatizo yatakwsha au yatakua umehamisha moja kwenda kushoto na lingine kwenda kulia?hapa naona utakua unapotea zaid,kwanza huna hela ya kula cha haraka kuuza ni simu yako maana saa yyte unaweza kupata hela ya kustiri siku mbili tatu au hata wiki kwa ajil ya msos nyumban,

Baada ya hapo mfate mwenye nyumba wako,kaa nae chini tena akiwa na mkewe mama mwenye nyumba mueleze A to Z tatizo linalokusibu naiman kabsa anaweza kukusaidia hasa akiona kabsa hal ya mkeo,

Then mfate muajiri wako mwambie naomba ruksa nikamuuguze mke hali yake sio nzur na mimba saa yyte anaweza jifungua,na hela hata mia sina,na wewe ndio muajiri plz najua mshahara haujatoka bt unaweza kunifanyia hata nusu nikamalize tatizo,kwa iman na ukwel huwez kosa msaada ppte,lakin umrudishe mke kwao kama wanavyokushaur kwa mtoto wa kiume sikushauri,pambana uonyeshe kwa nn wewe ni baba na usiuze cchte zaid ya simu yako halaf we tumia ya mkeo kufanya mambo yako yakutafuta cchte. Tchao
 
Back
Top Bottom