Naona kabisa Depression na stress zinakwenda kuniua

Naona kabisa Depression na stress zinakwenda kuniua

Nadhani hiki kitu kipo Dunia nzima yaani Mwanaume aliefanikiwa atakwambia sio rahisi kiivyo, usinione hivi nimeteseka na kupitia changamoto nyingi hadi kufika hapa nilipo kwa hiyo ni "ujiko"vilevile.
Mbona wanawake wanatoboa kirahisi bila maumivu. Nikuulize kipi bora kufanikiwa kirahisi au kufanikiwa Kwa misukosuko
 
Huyu tangu post yake ya kwanza alivyopunyuliwa na Arlteza nilimsoma anatakiwa amshukuru yeye alitoka salama na bajaji ndio ikaharibika je vipi angetenguliwa kiuno akawa yupo kitandani! Sasa hivi anatakiwa ahangaikie marejesho yake na sio kupiga ukunga kila wakati ebooh!
Nisamehe mimi.
Nimekuelewa.
 
Mbona wanawake wanatoboa kirahisi bila maumivu. Nikuulize kipi bora kufanikiwa kirahisi au kufanikiwa Kwa misukosuko
Asili ya jinsia hizi hazipo hivyo

Kiasili mwanaume ni provider wa food shelter na security while wanawake ni home animals,breast feeders na home warmers

Na ndiyo hata Sheria ya ndoa inamtambua mwanaume kama diyo sole breadwinner
 
Hellow JF

Naomba hata kama kuna Mtaalamu wa masuala ya psychology anisaidie kuniweka sawa.

nimepata ajali na bajaj yangu sijui itachukua muda gani kurudi barabarani..

Lakini sijui marejesho YANGU yatasimama au vipi, na sijui ikipona ntarudi tena au ndio wataichukua moja kwa moja.
Ntakuwa nimekosa vyote yani niko hopeless

Yani Daaah sina ABC wala D
Msaada wa mawazo please.
Pole sana, changamoto yako ni ndogo sana, jiambie nafsini mwako kwamba "hii ni issue nyepesi sana"
Marejesho sio jambo la kukuumiza kichwa Kwa linazungumzika,na sababu ya kushindwa kupeleka marejesho ni genuine!
Na traffic case inaisha bila tatizo, Kwa kuwa hiyo si jinai (labda iwe na jinai ndani yake, mf.iwe ilibeba bangi, silaha n.k)

Ikifaa elezea vizuri, ajali imetokea wapi, na mazingira ya ajali yalikuwaje, ili kama kuna mtu aliye karibu na ulipo aweze angalau kukupa hiyo psychological treatment.

Pole sana!
 
Kuvuja kwa pakacha nafuu kwa mchukuzi.
Huenda alikosea na ndo maana akasema sijui kama niko sawa,
Wabongo kwa kukuza mambo nawakubali.
Mwandishi atakuwa aliegesha tu hakuelewa, elimu bure yaani elimu bila usimamizi rasimi na endelevu, imeua vipaji vya vijana wengi
 
Sidhani kama hawa vijana wa sasa wana hata methali 1000 kwa kichwa.
Ndio maana hata hawakumbuki vizuri.
 
Uza iyo bajaji rudisha mikopo ya watu chenji inayobakia fungua biashara ingine Bob
Utakuja kunishukuru badae
 
Ndio hizo bajaji mnazokopeshwa kifisadi?

Pole sana mkuu. Kwani mkataba unasemaje kwenye scenario kama hii yako?

Endelea kufuatilia bima, ila pia usikae tu ndani endelea kujishughulisha na chochote halali kinachowezekana kwa sasa.
 
Asili ya jinsia hizi hazipo hivyo

Kiasili mwanaume ni provider wa food shelter na security while wanawake ni home animals,breast feeders na home warmers

Na ndiyo hata Sheria ya ndoa inamtambua mwanaume kama diyo sole breadwinner
Basi wenzetu wanapata raha sisi tunahangaika. Mahangaiko sio sifa hakuna kitu kizuri kama kula Kwa kustarehe bila jasho
 
Hellow JF

Naomba hata kama kuna Mtaalamu wa masuala ya psychology anisaidie kuniweka sawa.

Nimepata ajali na bajaj yangu sijui itachukua muda gani kurudi barabarani..

Lakini sijui marejesho YANGU yatasimama au vipi, na sijui ikipona ntarudi tena au ndio wataichukua moja kwa moja.
Ntakuwa nimekosa vyote yani niko hopeless

Yani Daaah sina ABC wala D
Msaada wa mawazo please.
Pole

1: Usiishi kwa kufikirika, kuwa proactive. Fanyia kazi yaliyopo kwenye mikono yako/usibaki kuyafikiria. Hapo muda unakuwa unakwenda, hivyo tumia muda wako vizuri bila panick.

2: Timiza wajibu wako kwa uaminifu, yaliyokutokea yaweza kumtokea yeyote na kwa madhira magumu zaidi.

3: Usijaribu kumtolea majibu yule ambaye haujamfikishia ujumbe, fikisha ujumbe kamilifu kwa kadri ya hali halisi na uwe chanya/be positive. Pata maoni halisi ya mhusika na uyafanyie kazi kikamilifu.

4: Amini aliyekufikisha hapo ulipo bado anaweza kukupitisha kwenye hilo na kukupeleka kwenye mafanikio zaidi.

5: Amini maisha ni kama barabara, huwezi kukosa kona na kona zenyewe ndo hizi ulizopo. Kata kona kwa uangalifu na spidi nzuri utafika.

6: Amini katika utaratibu wa maisha, usifikiri na kuamini katika kumaliza tatizo ghafla/kwa mkato hii inaweza kugharimu zaidi na kukuchanganya.

7: Pata wasaa na wenzako kijiweni ili kuangalia jinsi ya kutatua changamoto ndogo ndogo za kimaisha na michongo mipya. Kama umekuwa ukiishi ndani ya misingi ya kiutu basi usihofu.

8: Chukulia kila changamoto kama daraja la kupambana zaid, kuongeza juhudi wala changamoto isikunyong'onyeshe.

Nakutakia mafanikio mema.
 
Mzee wape taarifa wenye iko chomba fatilia taratibu halafu uckae kibwege tafuta Day day piga mzigo mambo yaendee


Unakata tamaa uko vema hata ujalazwa hospital mkuu
 
Back
Top Bottom