Maombi ya vita siyo maombi rahisi ni vyema upate muongozo sahihi kutoka kwa mtumishi/ mchungaji au muombaji anayejua maombi hayo. Nakushauri hiyo hali ikianza kemea ita damu ya Yesu kwa kumaanisha ukiwa katika hali hiyo, narudia tena ita "DAMU YA YESU"Amini hiyo hali itatoweka na kila siku itakapokuwa inaanza Fanya vivyo hivyo na hatimaye itapotea kabisa.......naongea haya nikiwa km shuhuda nakushuhudia niliwahi kupatwa na hali hyo ila hadi leo haijawahi kunirudia tena!
Muhimu kabisa usilale kama mpagani Fanya maombi kabla ya kulala kila siku. Mungu ni mwaminifu atakuponya na hiyo shida- pole sana