Naombeni ushauri wenu, nahitaji nunua iphone 6s+

Naombeni ushauri wenu, nahitaji nunua iphone 6s+

Kama umezoea kutumia Android phones mwanzo itakupa wakati mgumu sana, mpaka pale utakapoamua kuachana na vitabia vya simu za Android au utakapoanza kujua baadhi ya tweaks za kuifanya ilingane na matumizi yako awali, kama ulishazoea kurushiana nyimbo kupitia Bluetooth kwenye iPhone hayo masuala hayapo, kuweka miziki ni mpaka uwe na Software ya iTunes, kama ukizoea kutumia third-party app kuwa mbadala wa system app, huko kwenye iPhone nyingi zipo restricted kwa ajili ya security, kwa ufupi kama ulizoea mambo yako ya ajabu ajabu kwenye Android basi huko kwenye iPhone utayakosa mpaka baadae sana utakaonza kuijua vizuri eco-system ya iOS na tweaks zake kama jailbreak na nyinginezo

Nilipata shida sana kipindi cha mwanzo kuzoea ios, android ni ugonjwa mbaya sana asee[emoji23]
 
wewe bwana nunua tu tecno yaishe,nakufuatilia maswali yako hapa,najisikia kichefuchefu,tuache wa iOs tuendelee na maisha yetu na nyie wa Android hali kadhalika,acha kumchosha@ WAHEED SUDAY

Nashukuru kama umeshtukia hilo, jamaa inaonekana hana hata huo mpango wa kununua hiyo  anachofanya ni kumpumzikia mwenzake tu[emoji23][emoji23]
 
usifananishe iphone na vitu vya kijinga... me natumia android na ios lakin ukihifahamu vizuri system ya ios inavo operate utokaa kutaman kutumia android... android is the cheapest os to ever built
 
Wabongo Mna Matatzo sana..
mnajifanya Mnajua mambo wakat hata kutengeneza Calculator hamuwezi..

Sasa Eti 'qhd inatakiwa iwe kwenye Tv sio Simu' kwahyo wao walioweka kwenye simu ni wajinga,.?

Hapo juu umezungumzia Suala La customization eti ni Ujinga,kwako ni ujinga kwa wengine ni Raha,ulitaka zote ziwe na sifa 1 sasa kungekuwa na haja gani ya kuwa na Os Tofauti Tofauti.???

Nimetumia Iphone 6+ sitakaa nirudi tena kwenye Apple..Yani Bila Internet Apple ni sawa tu Na Tecno Ya Tochi Yenye Mp3 player..

Ndiyo maana mpaka leo Trump Anatumia Galaxy S3 na akishauriwa Na CiA abadilishe anakataa..

Viongozi wa juu wa US wanatumia Blackberry na ni lazima sio hiyari.
 
Trump Mpaka Leo Hii anatumia S3 galaxy..
na kagoma kubadilisha despite of ushauri wa CIA.?

Tu Bet Mkuu Tutafute Ushahidi.???

CIA hawashughuliki na mambo ya Rais,Secret Service ndio wanashughulika na hayo mambo.
 
Ngoja niendelee kukaa pembeni tu nisikilizie.

LAKINI
ukiwa na IPHONE sahau yafuatayo: kubadilisha mlio, kubadili launcher, kutumia bluetooth na vifaa visivyo vya apple, double line, rooting.
Mlio unabidil lakin ni process sana kweny itune
 
Nionavyo, Android wataendelea kutawala Dunia kwa muda mrefu zaidi.
Kwakua waba utajiri wa Apps, customize nyingi, nk

Japo binafsi navutiwa zaidi na iPhone.
 
Nionavyo, Android wataendelea kutawala Dunia kwa muda mrefu zaidi.
Kwakua waba utajiri wa Apps, customize nyingi, nk

Japo binafsi navutiwa zaidi na iPhone.

Android watengenezaji wapo wengi,kuanzi Samsung hadi akina Tecno zipo hadi za bei chee kabisa wakati Apple product zake anatoa za juu kabisa, sio wote wanaweza kumudu

Kwa msingi huo simu zinazotumia Android lazima zitakua nyingi sana mtaani sababu ya urahisi wake ingawa pia zipo za hali ya juu
 
Back
Top Bottom