Naombeni ushauri kwa hili lililonikuta

G8M8

JF-Expert Member
Jan 24, 2019
432
389
Mimi ni kijana niliyekulia ktk familia ya kipato cha kawaida Sana.. Nilianza safari yangu ya kusoma kwa kujituma toka shule ya msingi na kuvuka hadi advance nikiwa na imani iliyo kwenye mind yangu nije kuwa na maisha mazuri lkn pia nilikuwa nikiwaza Sana maisha yatakuwaje baadae kwani nimesomeshwa na mama na mama yangu ana amini mwanaye nitakuwa na maisha mazuri baadaye nikija kuajiriwa.

Sasa baada ya kumaliza kidato cha Sita mwaka 2018 nilijiamini nitatoboa kabisa sikuwa na hofu nilichukua combination ya pcm lkn mambo yakawa tofauti kabisa nikashindwa kukizi vigezo vya kwenda chuo..

Baada ya kurudi toka jeshi sikuwa vizuri nikifikiria nimekosea wapi mbona mtihani nilifanya vizuri nikifikiria mengi mpaka nikahisi kuchanganyikiwa kwa sababu matarajio yamekuwa tofauti na mama yangu naye na mawazo kibao akiamini maisha kwangu ndio basi kwa kweli nilikuwa na wakati mgumu weak Zapata 3 au 2..

Ndani ya hizo siku nilijawa na wazo nirudie mtihani lkn nilishaomba ushauri Sana kwa watu hadi wazazi wa wenzangu nakumbuka niliambiwa achana na hayo mawazo kubaliana na yaliyo tokea chukua uamuzi mwengine lkn nilitaka kufanya kumridhisha mama nikalipiwa gharama za mtihani lkn baadae nikawa na wazo la kufanya biashara nitoke kimaisha Kwan kusoma lengo litakuwa ni kuajiriwa na hilo jambo halitafanya nifike ndoto zangu kwani nina malengo mengi sana hivyo huu uamuzi wa kurudia mtihani nilijutia sikuwa najishughulisha kabisa na kusoma zaidi kutumia mda wangu kufanya tafiti za biashara mbali mbali..

Imefikia mda sasa nataka kufanya vitendo ili nifike lengo kuu.. sasa mama aliniuliza mbona sikuoni ukisoma itabidi nimwambie kitu ambacho nalenga kufanya na mtihani sitofanya kwani nimeona maisha yamebadilika ni wakati wa kubadili fikra zetu kujiajiri siyo kuajiriwa..

Mama yangu hataki kabisa wazo langu na ameongea Sana anaamini siwezi kuwa na maisha mazuri kama sitofika chuo kikuu.. yeye na mzee wameongea Sana na nimeambiwa kama nina mawazo hayo basi niondoke nyumbani nikatafute mama aliyenizaa

Nipo na mawazo mengi sana mama yangu amekasirika na hataki kuniona nimesikitika Sana wazazi wetu kuwa na mawazo haya... Ameongea Sana kiasi hata mm mwenyewe nina mawazo Sana sijamvunjia heshima mama yangu lkn yamekuwa haya..

Naombeni ushauri nifanye nini kijana wenu...


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kitu kimoja ambacho watu wengi wanajuta kwenye maisha Ni kufanya mambo kuwapendeza watu.

Fanya unachopenda kwa juhudi zote wazazi wako watakuelewa baadae..


Kitu kimoja ambacho Ni chako na unamiliki wewe Moja kwa Moja Ni maisha yako sasa wewe una uamuzi uwe jambazi,uwe padri use mfanyabiashara, uwe mwalimu uwe mvuta bangi ...ishi kama una hati miliki ya maisha yako... wazazi wako walishakuleta duniani inatosha waheshimu ila sio kupangiana maisha...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dah pole sana,fanya unachokipenda wewe na unachoona kitakutoa katika maisha.

tatizo lugha
 
Dah ndugu yangu.. wazazi wabadilike
Kahustle tu mtaani..hii mentality ya 'mwanangu soma ufike hadi chuo kikuu upate kazi uwe na maisha mazuri'
Imemteka mamako...na wazazi wengi wa siku hizi wanayo..mi siipendi kwakweli

Sent using Jamii Forums mobile app
wabadilike kwani Kuna ambao wanapoteza vipaji vya watoto wao kisa kukariri haya mambo.. Mama angu dah ataki kusikia kabisa hivi ameniambia atak kuniona kisa kusema nataka kujiajiri mwenyewe..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kitu kimoja ambacho watu wengi wanajuta kwenye maisha Ni kufanya mambo kuwapendeza watu.

Fanya unachopenda kwa juhudi zote wazazi wako watakuelewa baadae..


Kitu kimoja ambacho Ni chako na unamiliki wewe Moja kwa Moja Ni maisha yako sasa wewe una uamuzi uwe jambazi,uwe padri use mfanyabiashara, uwe mwalimu uwe mvuta bangi ...ishi kama una hati miliki ya maisha yako... wazazi wako walishakuleta duniani inatosha waheshimu ila sio kupangiana maisha...

Sent using Jamii Forums mobile app
Asante kwa ushauri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwweleze ukweli soko la ajira sio la uhakika Tanzania..unaweza pata degree ukasota miaka mitano unatafuta ajira..
Dah ndugu yangu.. wazazi wabadilikewabadilike kwani Kuna ambao wanapoteza vipaji vya watoto wao kisa kukariri haya mambo.. Mama angu dah ataki kusikia kabisa hivi ameniambia atak kuniona kisa kusema nataka kujiajiri mwenyewe..

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole Mdogo wangu
Najua unachopitia si kwasababu Mimi ni muhanga lakini ni kwasababu wazazi Wetu wengi wamebebwa na hiyo dhana ya kutaka status.
Cha kufanya
1. Amini kwamba ulipaswa upitie hayo na Mungu ana makusudi Wewe kupitia hapo
2. Maisha ni ya kwako, sisemi udharau wazazi maana at the end of the day wazazi watataka kusaidiwa na Wewe
3. Amini ndoto zako, tumia jitihada zako na muombe sana Mungu.
4. Ajira ni ngumu kwa kipindi hiki na hata biashara pia lakini biashara Ina uafadhali wa kuingiza hata 500
5. Tafuta mtu ( mentor) naamini mtu aliyefanikiwa ukikutana nae ukamuelewesha lengo lako atakuelewa na kukusaidia kimawazo na zaidi ya hapo
Naamini Mungu ana kusudi na Wewe
Usikate tamaa...simama endelea na safari..Amini njia unayotaka kupitia
 
Pole Mdogo wangu
Najua unachopitia si kwasababu Mimi ni muhanga lakini ni kwasababu wazazi Wetu wengi wamebebwa na hiyo dhana ya kutaka status.
Cha kufanya
1. Amini kwamba ulipaswa upitie hayo na Mungu ana makusudi Wewe kupitia hapo
2. Maisha ni ya kwako, sisemi udharau wazazi maana at the end of the day wazazi watataka kusaidiwa na Wewe
3. Amini ndoto zako, tumia jitihada zako na muombe sana Mungu.
4. Ajira ni ngumu kwa kipindi hiki na hata biashara pia lakini biashara Ina uafadhali wa kuingiza hata 500
5. Tafuta mtu ( mentor) naamini mtu aliyefanikiwa ukikutana nae ukamuelewesha lengo lako atakuelewa na kukusaidia kimawazo na zaidi ya hapo
Naamini Mungu ana kusudi na Wewe
Usikate tamaa...simama endelea na safari..Amini njia unayotaka kupitia
Asante Sana kaka.. Mungu akubariki

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulipokosea ni kuomba hela ukarudie mitihani halafu ukafanyia mambo mengine. Sasa nenda google upate data za WaTz ambao hawajaajiriwa pamoja na kuwa na degree zao. Halafu, google pia kuhusu maisha ya JackMa (mwenye kampuni ya Ali Baba), na ya Bill Gates (ambao wote wawili hawajamaliza elimu ya chuo kikuu). Ukiwa na data hizo, uende kwa wazazi wako, uwaombe radhi kwa "kuwadanganya" kwamba unaenda kuendelea na masomo. Kisha uwape hizo data za kina Jack Ma. Tafuta na majina ya matajiri wengine hapa Tanzania ambao hawana elimu kubwa. Uwaeleze wazazi wako kwamba kuwa na degree sio kigezo cha mafanikio. Ukiwaeleza kwa unyenyekevu watakuelewa tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fanya kilicho ndani ya moyo wako, ushakuwa mtu mzima sasa hutakiwi kuyumbishwa na mawazo ya wazazi/ndugu hatma ya maisha yako iko mikononi mwa Mungu na wewe mwenyewe.
Nafasi waliyo nayo wazazi/ndugu zako ni kukushauri tu na kukuonyesha njia sahihi katika maisha.

Muombe sana Mungu yeye ndiye ajuaye ukweli wewe ni nani hakuna mwingine.
 
hapo kweli mtihani unao mdogo wangu, ni hivi ili uweze kuwa na amani na ufanye vitu kwa uhakika ni lazma utengeneze amani na wazazi wako mana mwisho wa yote wao watabaki wazazi na ndio kimbilio lako la mwisho na wewe bado mdogo sana kuanza maisha huku wazazi wako wakiwa na kinyongo na wewe, sasa fanya hivi wewe kubaliana nao, resit mtihani lakini huku mambo yako mengine unayotaka kufanya yakiendelea, mana kusoma hakumzuii mtu kufanya biashara kama kweli ana moyo wa kufanya hivyo, na hata ikitokea umefaulu vzr ukachaguliwa kwenda chuo we nenda mana hiyo degree itakuwa faida kwako pia, mbona wako vijana wengi wanasoma chuo lakini pia wanajishugulisha na biashara kiasi kwamba wakimaliza wala hawahangaiki na ajira na hata wakitafuta inakuwa sio kwa presha, na kingine kuwa na elimu ya chuo ni kama ngao kwenye maisha yako kesho na kesho kutwa biashara zimegoma kabisa utatafuta ajira ikusaidie kimaisha wakati unatafuta namna ya kutatua changamoto zilizojitokeza kibiashara au kimaisha kiujumla
 
Back
Top Bottom