Naombeni Ushauri kuna mtu amenitishia

Naombeni Ushauri kuna mtu amenitishia

Wakuu kwema.

Nimekuwa nikiishi kwa amani sana mpaka pale nilipoenda kupanga mtaani,
Kuna mpangaji mgeni ila inaonekana yeye ni mwenyeji hapa mtaani , ni mvutaji bangi mkubwa mno, utulivu hakuna.

Juzi natoka zangu kampas nakuta mtu kanisubiri akisema nimeiba kitu chake ambacho hata mimi sikijui kwakweli,
Kaukuza ugomvi anasumbua sana.
Nasasa kasema atanifanya kitu kibaya kwakweli amekuwa akinitishia sana, ukizingatia pia jamaa ana magenge ya wavuta bangi wenzake, na wala huwezi kuzungumza naye akakuelewa anapiga kelele tu.

Wakuu naombeni msaada wa kimawazo, sijawahi kutishiwa hivi, Siwezi kuhama kwasababu nimelipa kodi ya miezi nane pia sina hela. Siwezi kuishi nahofia usalama wangu hivi
Wavuta bangi huwa wanaangalia mtu. Ameona labda wewe ni mpole, laini na mwoga ndiyo maana anakutishia lengo umpe pesa hana lolote huyo.

Tuliokaa uswahilini tunawajua hao! Wanataka ukiwakuta kujiweni unawapa hai, oya washkaji vipi! Buku la fegi hilo! Ndiyo furaha yao. Hata urud saa sita usiku hawakuteki! Utawasikia! Mwanetu huyu! Sasa wewe umeenda kukaa uswahilini mtoto wa kishua! Kama hauwezi kujipendekeza kwao, basi unatakiwa uvae uso wa mbuzi mpige mkwara asikuzoee. Kakamaa! Pia, kama unaweza tafuta marafiki wa muda polisi au wajeda kadhaa, siku moja uwende nao pale kwako mjifanye kama ni marafiki ili ajue kuwa akizingua unamletea noma
 
Mpaka unazinguana na mvuta bangi,basi utakua wewe ndo una matatizo.hao wavuta bangi ni watu flani hawanaga matatizo na watu kabisa zaidi ya wao kuvuta bangi zao.
 
Mambo yasiwe mengi, hama hapo kubali hasara, wengine wanatumwa na madalali na wenye nyumba ili kuiacha kodi,

Mtafute rafiki yako wa karibu kabane kwake, tafuta kodi kapange kwingine
 
Wakuu kwema.

Nimekuwa nikiishi kwa amani sana mpaka pale nilipoenda kupanga mtaani,
Kuna mpangaji mgeni ila inaonekana yeye ni mwenyeji hapa mtaani , ni mvutaji bangi mkubwa mno, utulivu hakuna.

Juzi natoka zangu kampas nakuta mtu kanisubiri akisema nimeiba kitu chake ambacho hata mimi sikijui kwakweli,
Kaukuza ugomvi anasumbua sana.
Nasasa kasema atanifanya kitu kibaya kwakweli amekuwa akinitishia sana, ukizingatia pia jamaa ana magenge ya wavuta bangi wenzake, na wala huwezi kuzungumza naye akakuelewa anapiga kelele tu.

Wakuu naombeni msaada wa kimawazo, sijawahi kutishiwa hivi, Siwezi kuhama kwasababu nimelipa kodi ya miezi nane pia sina hela. Siwezi kuishi nahofia usalama wangu hivi
Kavute RB na umweleze kuwa umemtaja kwa lolote baya likikupata. Pia akianza kupuliza moshi ita makamanda waje wamnywe akanyee debe.
 
mh kwa mtu anaetumia visu hapana
Wewe unadhani ni jambo jepesi kudhuru..... asilimia kubwa watu wa hivyo ni wadhaifu sana ukisimama nao kiume.......

Matukio kama hayo yameshanikuta Sana kwenye safari yangu ya maisha na asilimia kubwa ni confidence na kuondoa uoga.......

Makelele ya jamaa ni defence mechanism yake....lengo ni kumjaza hofu......

Nilishawahi mpaka kushikiwa panga lenye makali na vijana waliokuwa mbele yangu mitaa ya sisi kwa sisi miaka hiyo....na nikapita kati kati yao........

UKIWA TU MWANAUME JUA KUWA HAKUNA ALIYE NYUMA YAKO..... DUNIA NI KATILI SANA KWA MWANAUME MUOGA
 
Kama taifa tunasafari ndefu sana yani wewe ni mwanafunzi wa chuo na haujui ufanye nini kwenye jambo dogo kama hilo je huko kijijini kwenu hali ikoje? Si mtahamishwa kwenye makazi yenu kwa kulambwa makofi na mtahama maana hamjui mfanyaje
 
Sasa kama hana ndugu si maana yake hata we ukimpoteza hakuna wa kuhoji?

Ningekua nakaa na wewe hiyo nyumba usingeniamkia kwakua ungeona range yetu kiumri ni moja. Ila inabidi niseme "Vijana wa siku hizi laini sana"

Mtu anakutishiaje halafu unaogopa? Tena anavuta bangi? Si umkamate umbandue? Angekua askari ungehofia atakuja na kundi lake ila mtu wa uswazi mwenzako?
 
Hataki mazungumzo ya amani, wala sio msikilzaji , huwezi kuongea naye kirafiki akakusikiliza.
Kila mtu Kuna kitu anaogopa msome vizuri utakipata na wakati huo unafanya kutafuta angle ya kuweka mguu sawa siku akikufata we iambie adrenaline Yako iwe kwa amani au kwa Shari Niko tayari pambana haswa jifunze hiki kitu bro ni heri ufe kuliko kumuogopa mwanaume mwenzako unaweza usinielewe ila huo ndio uhalisia mi mtu pekee namuogopa ni mwanamke na mtoto Hawa huwa sijui namna ya ku revenge kwao ila mwanaume kama wewe
Chukua panga Yako ya size weka kwenye begi tembea nayo achana na polisi hamna kitu watafanya
"Coward of the county by ken Rogers"
 
Huyo jamaa ni mvuta bangi na ana magenge yake sasa hapo mkuu nakaaje na amani
Nenda polisi kaandikishe maelezo kwamba ukipata janga lolote muhusika ni yeye kisha chukua RB hifadhi ndani na hakikisha mjumbe wa eneo hilo awe anajua kila kinachoendelea yeye ndio atakuwa shahidi mbeleni.
Miezi 8 ni mingi sana kuiacha kizembe ingekuwa ni miezi 2 au 3 hapo sawa ningekushauri uiache
 
Solution 2:

Mvuta bhangi ni miongoni mwa watu wanaopenda hela.

Toboka Teni tuu mambo yatakaa sawa mpe mshikaji
Hii ni kweli inawezekana wamemuona jamaa ana muonekano wa kishua wanataka awe anatoa hela sema shida akitoa hela leo kesho wakimuona wanaomba tena itakuwa ni mchezo endelevu.
 
Nunua bangi siku moja nenda kijiweni kwao vuta wakuone na wewe sio mnyonge alafu tamka kuwa muda wowote kuna mvuta bangi hapoo mtaani utammaliza huku ukiongea kwa jazba nakumbia kuwa huyo mbwiga hachukui round lazima achimbe
Hii Mikwara wanafanyaga wakina Ndaro na Steve Mweusi kwenye Comedy zao ukikutana na aliyepinda zaidi hii njia yako hutoboi.
Utasikia wanaambiana hoya majita leo disko imeingia Mmasai ngoja tumfundishe michezo.
 
Hii Mikwara wanafanyaga wakina Ndaro na Steve Mweusi kwenye Comedy zao ukikutana na aliyepinda zaidi hii njia yako hutoboi.
Utasikia wanaambiana hoya majita leo disko imeingia Mmasai ngoja tumfundishe michezo.
Ni mbinu ambayo unatakiwa ukienda kuitumia uwe umeandaa vizuri nyonga na miguu ili kikitokea chochote uweze kuchimba mzee
 
Wakuu kwema.

Nimekuwa nikiishi kwa amani sana mpaka pale nilipoenda kupanga mtaani,
Kuna mpangaji mgeni ila inaonekana yeye ni mwenyeji hapa mtaani , ni mvutaji bangi mkubwa mno, utulivu hakuna.

Juzi natoka zangu kampas nakuta mtu kanisubiri akisema nimeiba kitu chake ambacho hata mimi sikijui kwakweli,
Kaukuza ugomvi anasumbua sana.
Nasasa kasema atanifanya kitu kibaya kwakweli amekuwa akinitishia sana, ukizingatia pia jamaa ana magenge ya wavuta bangi wenzake, na wala huwezi kuzungumza naye akakuelewa anapiga kelele tu.

Wakuu naombeni msaada wa kimawazo, sijawahi kutishiwa hivi, Siwezi kuhama kwasababu nimelipa kodi ya miezi nane pia sina hela. Siwezi kuishi nahofia usalama wangu hivi
Simama naye mtu mbili tu
Acha uwoga vijana wa sahv mbona mnakuwa legelege...
Huyo amekutisha lkn hana uwezo wa kukufanya lolote kwanza

Ova
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom