Naombeni Ushauri kuna mtu amenitishia

Naombeni Ushauri kuna mtu amenitishia

Huyo jamaa ni mvuta bangi na ana magenge yake sasa hapo mkuu nakaaje na amani
Huyo jamaa hana hiyo back up anakutishia tu....... mwanaume wa kweli hana vita ya maneno ikiwa ana uwezo wa kufanya tukio......

Huyo amekuona wewe ni mdhaifu na unatetemeka kila akikoroma ndio maana anakunyanyasa.......

Narudia tena....

Stand your ground as a man.......

Ilishawahi kunitokea mitaa ya manzese miaka mingi nyuma na nilipewa ushauri kama huu na baadae yule jamaa akawa rafiki yangu........

DUNIA NI KATILI KWA WANAUME WAOGA NA WENYE HOFU.........

ONLY THE STRONG CAN SURVIVE
 
Anayefanya jambo hasemi.......

Stand your ground as man......

Hivyo ndivyo dunia ilivyo....utashtaki wangapi.......

Huyo jamaa amekuleta kwenye dunia ya wanamume.....na ili uwe mwanaume lazima uivuke mitihani ya kiume......

Kaa kiume kaa tayari kwa mapambano....usiruhusu nafsi ya woga kujenga mizizi kwenye kifua chako.....

Dunia ni katili sana kwa wanaume waoga na wazembe.......
Mtoto wa single mother huyu kakulia kwa kudekezwa kimama ngoja anyooshwe kwanza
 
Nataka amani tu
Ukiitaka amani huwezi kuipata,dawa ya moto ni moto,ni bora usiogope chochote,maana kama jamaa ana nia ovu kwako hofu,wasiwasi na kuhangaika kwako hakubadilishi kitu, cha muhimu usiogope chochote ikiwa unajuwa hukumfanya ubaya wowote.
 
Wakuu kwema.

Nimekuwa nikiishi kwa amani sana mpaka pale nilipoenda kupanga mtaani,
Kuna mpangaji mgeni ila inaonekana yeye ni mwenyeji hapa mtaani , ni mvutaji bangi mkubwa mno, utulivu hakuna.

Juzi natoka zangu kampas nakuta mtu kanisubiri akisema nimeiba kitu chake ambacho hata mimi sikijui kwakweli,
Kaukuza ugomvi anasumbua sana.
Nasasa kasema atanifanya kitu kibaya kwakweli amekuwa akinitishia sana, ukizingatia pia jamaa ana magenge ya wavuta bangi wenzake, na wala huwezi kuzungumza naye akakuelewa anapiga kelele tu.

Wakuu naombeni msaada wa kimawazo, sijawahi kutishiwa hivi, Siwezi kuhama kwasababu nimelipa kodi ya miezi nane pia sina hela. Siwezi kuishi nahofia usalama wangu hivi
Acha kulia Lia wewe....nenda nunua bastola ya plastic...mwambie mkutane mkikutana iweke kiunoni...mwambie nimekuja tuongee ulichokuwa unasema kama wanaume kisha nyanyua mabega kidogo aione. Hata kusumbua tena.

Kuwa mwanaume...yakikushinda tafuta elfu 50 Lipa vijana ashughulikiwe.
 
Ungekuwa wewe ungefanyaje mkuu, maana nikianza ugomvi nitatoka kwenye focus namimi nahitaji suluhu ya kudumu.
Usitishike na maneno yake wewe endelea na mambo yako.....usimjibu wala kujibizana naye.....ukikutana naye muache aongee na usiondoke mpaka amalize kuongea lakini usioneshe hofu wala woga........

Tembea kwa kujiamini lakini uwe na tahadhari.....lakini uwe na uwezo wa kujitetea physically iwapo atakuvamia(naamini hawezi kufanya hivyo)......

Umeruhusu hofu kukubomoa na kuonekana mdhaifu.....
 
Kwani upo mkoa gani Mkuu?

Kwa maelezo yako ni kama unasoma chuo. Sasa nawaza mmepishania wapi na huyo jamaa ila labda anahisi unambania kufanya jambo fulani hapo mnapoishi.

Sasa wewe toa taarifa kwenye vyombo vya kiserikali, ila pia naweza kushauri jambo tofauti kidogo. Kuna muda ishu za mtaani zinamalizwa mtaani.

Wewe cheku wadau kutokea mbali na hapo wapange vizuri, muibukieni huyo jamaa anyooshe maelezo vizuri. Asipigwe ila aonywe kimtaa akiwa nunda aguswe kidogo.

Usiwe mnyonge sana, utaonewa na kila mtu Mkuu.


IGP Sirro alishangaa mtanzania unalalaje ndani huna hata panga.

Jiongeze Mkuu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom