Naombeni msaada nimechanganyikiwa

Naombeni msaada nimechanganyikiwa

kuokoka ndo nini? mbona utampa sana shida kaka wa watu .mi naona hata humfai wanawake waliokoka kama mnavojiita ni shida tupu
 
ajipime katika hayo maswali niliyomuuliza halafu afanye maamuzi
Tatzo linapokuja ni kwamba bint kapenda sana hata anavyosema ulokole imekuwa kichaka tu..
Kwahyo yawezekana hata hayo maswali akaona hayana umuhimu kwasasa
 
Wasalaam wana JF, mimi binti Nina tarajia kuwa tabibu hivi karibuni. Ila Nina tatizo Fulani, nina mchumba muislam na mimi ni mlokole, tunapendana sana lakini wachungaji wangu hawamtaki kabisaaa.

Nachanganyikiwa wanadai nimuache, tutafanya maombi nitapata mlokole mwenzangu wananiambia biblia inasema "msifungiwe NIRA na MTU asiyeamini" na MTU asiyeamini ni yule ambaye hajampokea YESU kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake na haamini kifo cha msalaba, ila wazazi wetu wote hawanashida sasa nifanyeje niko njia panda.

Kama nimekosea undishi mnisamehe sana naombeni mchango wenu

Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app
NB. Huyu mtu nimeanza mahusiano nae kabla sijaokoka na nimeokoka ukubwani
Mungu Mmoja tu kwani shida ipo wapi.

Sent from my TRENDY using JamiiForums mobile app
 
Tatzo linapokuja ni kwamba bint kapenda sana hata anavyosema ulokole imekuwa kichaka tu..
Kwahyo yawezekana hata hayo maswali akaona hayana umuhimu kwasasa
basi na ajiandae tu badae sababu ndoa si shela japo najua akili yake kwa sasa inawaza ile siku ya chereko chereko yale masaa matatu yale na kusahahu maisha baada ya masaa matatu
 
Sasa mlokole mzima jambo Dogo kama hilo linakusumbua!!?umeokoka lini?
 
wewe unahitaji approval ya wachungaji au wazazi?
 
Pole kwa kuchanganyikiwa.

Tatizo umesema "umeambiwa na wachungaji kuwa BIBLIA inasema hivi"

Ila ungekuwa msomaji mzuri wa Biblia nadhani ilikuwa hata ufiki hali hiyo ya kuchanganyikiwa ungepata majibu mwanzo kabisa.
 
Utaanguka kiroho take care sio kila mtu anayekufaa tafuta mtu atakaye ijenga imani yako zaidi ndoa sio bora kuliko usalama wa imani yako take care.
Muombe Mungu sana

Sent from my TECNO-J8 using JamiiForums mobile app
 
Halafu Mimi huwa nashangaaa sana hasa tunaojiita walokole ivi iweje wewe misingi ya imani yako ijengwe kwa Mchungaji ebo!

Yani wewe kung'amua kitu kidogo hiki unashwindwaje sikiliza dada kaa chini soma Biblia kwa msaada wa Mungu utakuwa mbali sana msaidizi wako wa karibu ni 'holy spirit' achana na mambo ya wachungaji.

Kifupi sio healthy sana kuolewa na mtu wa imani hiyo kama ni Mungu amekupangia umuokoe through you labda otherwise tafuta mtu atakaye kuinua kiroho.

Sent from my TECNO-J8 using JamiiForums mobile app
 
Nachelea kuseme ww sio MLOKOLE kabisa ila unasali na sisi.

~Dada Mungu hadhihakiwi hata kidogo na sisemi umemdhihaki hapana maana biblia inasema viache ngano na magugu vikue pamoja ndio km hivi.

~Narudia hujaokoka huijui kweli ww!! tena ungeijua gharama ya msalaba na damu ya YESU y ungetubu mapema sana dhambii haianzii nje huanzia ndani.

~Natamani km nikuhubirie yani kuna kitu kinachemka ndani yangu si cha kawaida.najiuliza una ROHO MTAKATIFU kweli?

~Mimi ni mlokole tena kwa chimbuko dada Mungu anajibu,usisingizie wachungaji ww biblia husomi au zipo tofauti yakwako inaruhusu??

Yeremia 17:5 inajieleza wazi.panda mlimani,hata siku 3 kavu,lia kwa Mungu majibu hayapo Jf yapo magotini mama.Ita jina lipitalo majina yote.

~dada iambie damu inenayo mema kuliko damu ya habiri inene mema juu ya hilo,ingia patakatifu pa patakatifu,kisogelee kiti cha rehema kwa ujasiri.amuru mbingu iachie majibu,fungua madirisha ya hazina iliyo sitirika ohooo jamani kwa YESU raha saaana.

~Nb;MUNGU HAWI RADHI NA WAPUMBAVU.

Sent from my SHV-E250S using JamiiForums mobile app
 
kuokoka ndo nini? mbona utampa sana shida kaka wa watu .mi naona hata humfai wanawake waliokoka kama mnavojiita ni shida tupu
Dada ulokole si shida,shida ni watu kwanza mm kumkiri YESU kuwa bwana na mwokozi wa maisha yangu naona faharii mnoo tena najivunia kuwa mlokole.kama ww unaona ni shida basi ni kwako na si kwawote.

~Sikushangai walikuwepo wakina Kora,Sauli,Farao lkn muda ulipo fika walisalenda.ninacho furahia umeumbwa kwa mfano wa Mungu subir wakati wa Bwana

Sent from my SHV-E250S using JamiiForums mobile app
 
Ulokole siku hizi umekuwa kichaka cha mabinti wasaka waume.....hivi mlokole aliyeiva katika imani anaanzaje mahusiano iwe na mtu wa imani yake au hata wa imani nyingine?...huyu binti kaamua kutuuzia chai tuu na kuchafua imani za watu.

Mkuu;
Ubarikiwe saana. tu kwa kuliona hilo. Nimemshauri akimbilie huko kwa muisilamu leo leo kwani wazazi weshakubaliana. Aachane na hao wachungaji wanaompotezea muda
 
Wasalaam wana JF, mimi binti Nina tarajia kuwa tabibu hivi karibuni. Ila Nina tatizo Fulani, nina mchumba muislam na mimi ni mlokole, tunapendana sana lakini wachungaji wangu hawamtaki kabisaaa.

Nachanganyikiwa wanadai nimuache, tutafanya maombi nitapata mlokole mwenzangu wananiambia biblia inasema "msifungiwe NIRA na MTU asiyeamini" na MTU asiyeamini ni yule ambaye hajampokea YESU kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake na haamini kifo cha msalaba, ila wazazi wetu wote hawanashida sasa nifanyeje niko njia panda.

Kama nimekosea undishi mnisamehe sana naombeni mchango wenu

Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app
NB. Huyu mtu nimeanza mahusiano nae kabla sijaokoka na nimeokoka ukubwani
Binti tafadhali. Mpenzi ni upofu lakini nakuhakikishia baada ya mwaka mmoja kama utang'ang'aniza hiyo ndio.

Hutapata wa kukusaidia hata Wahenga hautawapata waliopata kusema hapo mwanzo kuwa majuto ni mjukuu.

Acha huo mchezo.
 
  • Thanks
Reactions: THT

Similar Discussions

Back
Top Bottom