Mkereketwa_Huyu
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 10,590
- 7,951
Wasalaam wana JF, mimi binti Nina tarajia kuwa tabibu hivi karibuni. Ila Nina tatizo Fulani, Nina mchumba muislam na mimi ni mlokole, tunapendana sana lakini wachungaji wangu hawamtaki kabisaaa. Nachanganyikiwa wanadai nimuache, tutafanya maombi nitapata mlokole mwenzangu. Wananiambia biblia inasema "msifungiwe NIRA na MTU asiyeamini" na MTU asiyeamini ni yule ambaye hajampokea YESU kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yake na haamini kifo cha msalaba, ila wazazi wetu wote hawanashida. Sasa nifanyeje Niko njia panda. Kama nimekosea undishi mnisamehe sana naombeni mchango wenu
Sent from my Vodafone Smart Tab 3G using JamiiForums mobile app
NB. Huyu MTU nimeanza mahusiano nae kabla sijaokoka na nimeokoka ukubwani
Acha ujinga wewe, ukiendekeza dini hata kula utashindwa. Penzi alibaguwi na wala halina rangi, dini, mfupi, mrefu, mwembamba, mnene, na wala kabila japo hili lina utata kidogo. Kama umempenda huyo jamaa yako fuata moyo wako, hao wachungaji wako watakulostisha na kukupatia mwanamme si chaguo lako mwisho wa siku utakuja kujishitukia unatafuta mchepuko. Walokole si watu wa kuwafuatilia, wanajipa matumaini ya hajabu na yasiyo na maana wala msingi. Penzi ni chaguo lako wewe si la wengine.