Naombeni msaada kwenye hili

Hziyech22

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2019
Posts
18,302
Reaction score
26,151
Jana ndugu yangu alienda kupima Corona baada ya kupimwa akataka aondoke baada ya kumaliza kupimwa akaambiwa akae kwanza karantini mpaka kesho yake na majibu atapewa hiyo kesho.

Na Mungu mkubwa matokeo amepata negative ila wamemzuia kuondoka leo bila kutoa gharama ya kuwepo karantini ambayo kaambiwa ni laki 3.5 wakampunguzia mpaka laki 2, wakati anaenda kupima Corona alizani ni bure na pia yeye akutaka kubaki hapo karantini ila alilazimishwa na daktari je mwenye kujua kuhusu hili imekaaje? atuambie
 
Alipimiwa wapi?

Amandla..
 
Hao siyo matapeli kweli? Kipimo kilichukuwa siku moja? Mhn! Sounds fishy
 
Elezea vizuri watu waelewe ndugu. Alikuwa nje ya nchi? Alienda kupima wapi? Alikuwa anaumwa ndiyo akaenda? Karantini aliwekwa wapi?
 
Mkuu Usio na Hatia Mtegemea, jibu maswali haya usaidiwe
Elezea vizuri watu waelewe ndugu. Alikuwa nje ya nchi? Alienda kupima wapi? Alikuwa anaumwa ndiyo akaenda? Karantini aliwekwa wapi?
P
 
Elezea vizuri watu waelewe ndugu. Alikuwa nje ya nchi? Alienda kupima wapi? Alikuwa anaumwa ndiyo akaenda? Karantini aliwekwa wapi?
Yupo hapa hapa bongo na kapima hapa hapa bongo alikuwa amehisi ana dalili za Corona ndo akaenda kupima ila kapatikana negative.
 
Mleta mada wewe hukwenda kule kwenye isolation ya ofisi?
 
Karantini ni aina mpya ya kupiga pesa hapa nchini
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…