Sekta ya Huduma kama hiyo mara nyingi watu huambizana kuwa kituo au Doctor fulani wako vizuri sana through word of mouth
Hivyo basi the best way kupata wateja wengi ni kuwahudumia hao wachache kwa huduma iliyotukuka.
Feedback, lazimisheni kwa staff wenu mechanism ambayo itawafanya mpate feedback toka kwa wagonjwa wenu. Kumbukeni tunaishi ktk dunia ambayo customer feedback ni mtaji mkubwa mno ili muweze kubadilisha WEAKNESS zenu ziwe STRENGTH (isije ikawa nimekuacha)
Ikiwezekana una hire hata "mysterious shoppers" ambao watawapa feedback jinsi gani wateja wanahudumiwa hapo
TAT, Turn Around Time ktk huduma yoyote muda wa kupata huduma ni kitu muhimu sana, nadhani kwenye suala la Afya umuhimu wake utakuwa maradufu. Hivyo ni lazima muweke standard ya muda tangu mteja anaingia, anajiandikisha mpaka anamaliza huduma itachukua muda gani ? Jee mteja kaletwa yuko hoi anatweta kwanini asipelekwe kwanza kwa Daktari wakati kujiandikisha kunafuatia.
Na mkishaweka hiyo TAT mnahakikisha mna system ambayo inaenda sawa na muda mlioweka
Tofauti, lazima mjitofautishe na watoa huduma wengine kwa mfano wateja wengi wanajuwa nikienda Marie Stoppes wako competent kwa tiba za aina fulani, nikienda Furaha Clinics pale Morocco ni kwa ajili ya watoto. Hivyo na nyie lazima muwe na utambulisho ktk specialisation zenu ingawa hawa wa Malaria, UTI na Typhoid nao mnawahudumia
Ubunifu, wekeni utamaduni wa ubunifu katika kuwahudumia wateja. Mnaweza mkawa na digital database ya customers wenu mkawa na tarehe za kuzaliwa za wateja, ambapo mnaweza mkawa mnawawish happy birthday wateja wenu kila wakati ikifika au hata kuwatakia Sikukuu njema zifikapo nyakati za Sikukuu
Usafi wa Mandhari, Wafanyakazi, Vifaa Tiba na Kauli za Watoa huduma nazo ni muhimu sana
Ciao