Naomba ushauri wenu

Naomba ushauri wenu

Nilimchukuwa kwa nia ya kumsaidia ila dah ni vigumu mno tena sana nilitaka aje ni mtafutie kazi kwasababu nilikuwa tayari nina connexion ya kazi na baada ya hapo ni mtafutie nyumba ila mipango yote hii imekwamishwa kwasababu ya kutokuelewa kwake tu

Nilikuwa naishi hapa mambo yalikuwa ivi kikawaida yeye anafanyaga kikiwa kipindi cha baridi ndo anatafutaga sehemu ya kukaa na sehemu zote ambazo alikuwa anakaa kote alifukuzwa kwasababu ya tabia yake ya uongo tu sasa kipindi iki nikamwambia mke wangu kuwa tumkaribishe baba hapa kwasababu ili nipate kumsaidia kupata kazi na sehemu ya kulala mke wangu akubali kumpokea baba nyumbani lengo langu lilikuwa akija tu nimtafutie kazi na akiwa na kazi ni mtafutie chumba cha mda miezi 6 kuendelea ila cha hajabu sasa mtu ambaye nilimpokea ili nije kumsaidia hasaidiki hata kidogo kwanza alikuwa hana document yeyote nimejaribu kumbembeleza vipi alete document ili ni msaidie kumpata kazi ana nidanganya kuwa ana kazi na kila siku anaendaga uko ambako anaitaka kazini kwake ila ukweli ni kwamba ana shinda ndani ya station za bus tu na yote haya anafanya kwasababu moja ya tatizo lake ni kukubali kuwa ameshindwa asaidie au kukubali kuwa hana
APatiwe atakudanganya mpaka utachoka
Vizeee vyetu vya keko sio vya kuvibeba kuvipeleka mambele vitakutoa roho .
Hapa hapa bongo ukimbeba mzee sijui uishi naye nyumbani haki nakuambia lazima avunje ndoa yako kama sio kwa kukutongozea mkeo basi ni kuwafutinisha wazee wa keko hao ..

Anyway kwa maisha ya mzee wako fanya chap umrudishe uliko mtoa kama msaada msaidie akiwa huko huko ili tatizo usiishi nalo mpaka mwakani atakuuwa huyo
 
Ulimchukua kutoka wapi?,inakuwaje qnakuwa mdwanzi hivyo mbona umri wa miaja 46 ni mtu ambae ana nguvu za kupambana
 
Nahitaji ushauri wa watu wenu ndugu zangu wenye busara.

Ninaishi Canada kwenye nyumba ya serikali (HLM) pamoja na mke wangu na watoto wangu wawili. Baba yangu ana miaka 46. Nilimchukua aishi kwangu kwa sababu alikuwa ana maisha magumu, lakini tangu ameingia kwangu maisha yamekuwa magumu sana.

Tabia zake zimekuwa changamoto kubwa:

Ni muongo kupita kiasi, hasemagi ukweli hata nikimwomba nimsaidie kupata kazi.
Ni mvivu wa kazi, hajawahi kuendelea na kazi yoyote. Wiki 3 sasa hana kazi wala kipato.
Anadanganya kuwa anaenda kazini kumbe anazurura tu mitaani.
Ni mlalamikaji, mbishi, na anakasirika haraka.
Ni mbeya na ana historia ya kuleta migogoro ndani ya familia. Kwasababu ya uongo wake
ALimkataa mama yangu 2017 tena kwa talaka cha ajabu yeye ndo anateseka zaidi na wakati aliaminisha jamii kuwa mama yangu ndo mbaya
Ana tabia ya kutumia watu, akishapata mahali pa kula na kulala, anajisahau kabisa.
Anapenda kula sana, na gharama za chakula zimepanda sana. Zamani nilikuwa natumia $200–$300 kwa mwezi, sasa tunatumia $700+.
Hatoi chochote kwenye matumizi, mimi ndiye nabeba kila kitu.

Kwenye nyumba ya serikali (HLM) siruhusiwi kuishi na mtu mwingine yeyote ambaye hajatajwa kwenye mkataba. Hii inaniweka kwenye hatari ya kufukuzwa na kupoteza makazi yangu pamoja na familia yangu.

Ukweli mwingine mgumu ni kwamba baba yangu amezoea kufukuzwa kila mahali anapokwenda kwa sababu ya tabia zake. Akiachiwa aishi kwa watu, harudi tena kwao mpaka apate shida. Baridi ikianza ndipo anarudi kuomba msaada.

Nimejaribu kila njia za kumwonya, kumueleza, kumsaidia, kumuelekeza, lakini haelewi kabisa. Kila siku ni uongo, visingizio, lawama na kuonyesha ubabe. Ukimwambia jambo analalamika au kuchukia.

Sasa nimefika mwisho nataka kumfukuza ila kuna wakati huruma unanijaa moyoni tu

Ila Nina hofu kwa watoto wangu, mke wangu, ikiwa tutapoteza nyumba yetu kwa kuvunjiwa mkataba na serekali sisi ndo tutaangaika zaidi . Lakini pia ninajua huyu ni baba yangu mzazi, na akitoka kwangu atakuwa hana pa kwenda

Swali

Nifanye nini katika hali kama hii?
Nimfukuze kwangu kwa ajili ya usalama wa familia yangu, au niendelea kumvumilia huku familia yangu ikiteseka?

Naomba ushauri wenu
Una umri gani mkuu
 
Tatizo naishi kwenye nyumba ya serekali na wakijua anaishi hapa nitakuwa nimepoteza nyumba yangu ya kwasababu mkataba utavunjwa kwa kutoheshimu mkataba pili hajishauriagi yeye ni uongo tu ata nikimwambia mambo ya kujenga maisha yake anakuona kama adui yake vile
Sasa kama baba yako ana 46 years wewe una miaka mingapi
 
Ukishakuwa na familia yako,kukaa na mzazi wako ni changamoto
Huruma isipite uwezo wako,mrudishe nyumbani akigoma fukuza!
Harafu umri wake ni 46 yrs? Huyu bado ni kijana anaweza kufanyakazi na kujitunza!
Imetosha kwa muda wote uliomsaidia.
Aisee ujue nimeshangaa age hiyo mbona anajilemaza sana,huyo ni my age mate kabisa, umri huu sisi ni watu wazima angekuwa 60 ningeelewa
 
Dah ila mara nyingi downfall zetu zinaletwa na ndugu siku zote..kuliko mtu Baki . .
 
Kumbe cost of living ni chini sana huko,yani chakula unatumia USD 700 tu-ndogo sana.
 
Huyo ni BABA YAKO MZAZI
au baba yako mlezi?

KAMA NI BABA YAKO MZAZI, BASI KATI YAKO WEWE NA UBONGO WAKO KUNA KIMOJA HAKIPO SAWA!

Sina ushauri mwingi kwa umakolo wako zaidi ya kukuambia GHARAMA ALIZOTUMIA BABAKO KUKUTUNZA NI ZAIDI YA HIVYO VIDOLA!

1. maisha ni magumu kwa sababu umelifunga lango la baraka (kwa kumuona babako kero)

2. hakuna aliye mnanga babake mzazi akabaki salama.

3. MHESHIMU BABAKO NA MAMAKO SIKU ZAKO ZIWE NYINGI DUNIANI.

4. Mrudie muumba wako kwa imani yako ili ubaki salama!

5. MTUNZE BABAKO, MAANA WAKATI ANAKUTUNZA HAKUKUAMBIA UENDE KUTAFUTA KAZI.

6. Yeye kutalakiana na mamako haikuhusu maana huwezi jua tatzo liko wapi. ACHA UJINGA MTUNZE BABAKO.
 
Ikiwa Ulishajaribu: Kumwambia, Kumweka karibu na Kumshauri bila kumdhalilisha mbele za watu/ familia yako.
Na bado: ni muongo, mbishi n.k
, basi mtafutie malazi(shelters) yaani sehemu za msaada wa wahamiaji / wanaume wasio na makazi/ nyumba za wazee. Baada ya kumpeleka mpatie kwa kiasi kidogo cha pesa ya kwanza ya kujikimu.

Unaweza kumwambia kwamba sababu ya yeye kuhitajika kutoka hapo ni kwamba "sheria ya HLM hairuhusu mtu ambaye hajatajwa kwenye mkataba wa kupangisha nyumba hii, kuendelea kuishi hapo zaidi ya siku kadhaa... "

Ila bado unajukumu kubwa la kumnasihi kwa hekima, muwe wawili tu na kuona kama atajirudi, kumfukuza BABA ni hatua nzito sana.
Usichokijua ww ni kwamba, hayo ni maagizo kutoka kwa mkewe.
 
Nahitaji ushauri wa watu wenu ndugu zangu wenye busara.

Ninaishi Canada kwenye nyumba ya serikali (HLM) pamoja na mke wangu na watoto wangu wawili. Baba yangu ana miaka 46. Nilimchukua aishi kwangu kwa sababu alikuwa ana maisha magumu, lakini tangu ameingia kwangu maisha yamekuwa magumu sana.

Tabia zake zimekuwa changamoto kubwa:

Ni muongo kupita kiasi, hasemagi ukweli hata nikimwomba nimsaidie kupata kazi.
Ni mvivu wa kazi, hajawahi kuendelea na kazi yoyote. Wiki 3 sasa hana kazi wala kipato.
Anadanganya kuwa anaenda kazini kumbe anazurura tu mitaani.
Ni mlalamikaji, mbishi, na anakasirika haraka.
Ni mbeya na ana historia ya kuleta migogoro ndani ya familia. Kwasababu ya uongo wake
ALimkataa mama yangu 2017 tena kwa talaka cha ajabu yeye ndo anateseka zaidi na wakati aliaminisha jamii kuwa mama yangu ndo mbaya
Ana tabia ya kutumia watu, akishapata mahali pa kula na kulala, anajisahau kabisa.
Anapenda kula sana, na gharama za chakula zimepanda sana. Zamani nilikuwa natumia $200–$300 kwa mwezi, sasa tunatumia $700+.
Hatoi chochote kwenye matumizi, mimi ndiye nabeba kila kitu.

Kwenye nyumba ya serikali (HLM) siruhusiwi kuishi na mtu mwingine yeyote ambaye hajatajwa kwenye mkataba. Hii inaniweka kwenye hatari ya kufukuzwa na kupoteza makazi yangu pamoja na familia yangu.

Ukweli mwingine mgumu ni kwamba baba yangu amezoea kufukuzwa kila mahali anapokwenda kwa sababu ya tabia zake. Akiachiwa aishi kwa watu, harudi tena kwao mpaka apate shida. Baridi ikianza ndipo anarudi kuomba msaada.

Nimejaribu kila njia za kumwonya, kumueleza, kumsaidia, kumuelekeza, lakini haelewi kabisa. Kila siku ni uongo, visingizio, lawama na kuonyesha ubabe. Ukimwambia jambo analalamika au kuchukia.

Sasa nimefika mwisho nataka kumfukuza ila kuna wakati huruma unanijaa moyoni tu

Ila Nina hofu kwa watoto wangu, mke wangu, ikiwa tutapoteza nyumba yetu kwa kuvunjiwa mkataba na serekali sisi ndo tutaangaika zaidi . Lakini pia ninajua huyu ni baba yangu mzazi, na akitoka kwangu atakuwa hana pa kwenda

Swali

Nifanye nini katika hali kama hii?
Nimfukuze kwangu kwa ajili ya usalama wa familia yangu, au niendelea kumvumilia huku familia yangu ikiteseka?

Naomba ushauri wenu
Tuanze kwanza, mama aliyetalikiwa na baba mwaka 2017 yuko wapi kwa sasa?,kingine una uhakika huyo ndio baba yako kweli?
 
WEwe ni andazi unajitengenezea chai
Huyu andazi ni andazi kweli😁. Inakuwaje mzee anakula zaidi ya share nzima ya familia yake kutoka $200 - $700?.

Binadamu unakuwaje na nguvu ya kumsemea negatively binadamu mwenzako kuhusu chakula? Kitu ambacho baada ya dakika kadhaa kinageuka jina ambalo hautaki hata kuliona/ kulisikia hadharani? Hata kwenye uongo hii haitakiwi.

Kuwa mchoyo maeneo mengine siyo chakula
 
Duuh huyu stori zake na jamaa mmoja alikuwa anaitwa nipo online unafikiri wanaandikia wageni wa Facebook
 
Back
Top Bottom