Naomba ushauri Ninunue Bajaji au IST Nifanye Uber/Bolt

Hyrax

JF-Expert Member
May 20, 2023
604
1,534
Wakuu salaam, Naomba ushauri wenu aisee maana ni wiki sasa najaribu kudadavua kipi ninunue kati ya Bajari au Gari aina ya IST kwaajili ya biashara ya huduma ya usafiri hapa mjini kupitia Bolt na Uber, mbali na hilo ntakuwa nafanya mishe zingine kupitia chombo nitakachonunua sasa naomba wenye uzoefu wa hizi mishe kipi nianze nacho na kitakachonipa faida endelevu, uzuri nitakuwa naendesha mwenyewe maana sina mishe nyingine hapa town kwasasa. ushauri wenu ntaupokea na kuwashukuru. asanteni
 
Wakuu salaam, Naomba ushauri wenu aisee maana ni wiki sasa najaribu kudadavua kipi ninunue kati ya Bajari au Gari aina ya IST kwaajili ya biashara ya huduma ya usafiri hapa mjini kupitia Bolt na Uber, mbali na hilo ntakuwa nafanya mishe zingine kupitia chombo nitakachonunua sasa naomba wenye uzoefu wa hizi mishe kipi nianze nacho na kitakachonipa faida endelevu, uzuri nitakuwa naendesha mwenyewe maana sina mishe nyingine hapa town kwasasa. ushauri wenu ntaupokea na kuwashukuru. asanteni
Kama upo DSM ist is better utapata michongo plus uber na utapata wateja wa Uber plus ambao sio Uber maana bajaji Kuna Muda Mtu atahitaji mwende mbali then chombo kitashindwa kupiga Kazi lakini Kama upo mikoani bajaji inaweza kuwa sahihi but I'm not sure
 
Guta lipeleke shamba na usimamie mwenyewe.

Tafuta eneo wanapovuna hasa mahindi ama mpunga hutojutia japokuwa ni lazima ukubaliane na mazingira ya kuishi shamba.
 
Bora ununue ist sabu kwanza inadumu zaidi ya bajaji lakin pia Ist ina hazi zaid ya bajaji kwaiyo wigo wa wateja utaongezeka na pia ist unaweza ata ikodisha kwwnye sherehe, harusi na ata misiba
Lamwisho IST ni gar unaweza ata itumia kwa shuguli zako binafsi mara moja moja,
Ist in air condition, inavioo uwezi nyeshewa mvua wala kupigwa jua
Kwa wale tunaokaa majijini IST inaingia mtaa na sehemu yyte ila bajaji hairuhusiwi kuingia mjini kati
 
Guta lipeleke shamba na usimamie mwenyewe.

Tafuta eneo wanapovuna hasa mahindi ama mpunga hutojutia japokuwa ni lazima ukubaliane na mazingira ya kuishi shamba.

Wewe nae umetoka usingizini et, jamaa anamaanisha bajaj ya abiria kwaajiri ya kufanya Uber wewe unaongelea bajaj ya mizigo, madafakary
 
Back
Top Bottom