Nawasalimu kwa Upendo wanaMMU.
Kuna hili jambo naomba unishauri maana sina uhakika na ninayoyafanya niyafanye vipi.
Nina binti ambaye yupo sekondari, boarding school.
Wadada wa kazi ambao nimeshakaa nao mpaka sasa wote ni wana umri mkubwa kwa binti yangu.
Huyu binti yangu ukweli tangu akiwa primary school huwa napenda sana anapokuwa home asaidie kazi za nyumbani kama ambavyo wadada wanafanya. na imetokea kawa mfanya kazi mzuri sana, kuanzia kupika, kufanya usafi na kazi zote za nyumbani.
Tatizo sasa linakuja, dada wa kazi niliyenaye sasa anataka kazi zooteee za nyumbani wafanye sawa na binti yangu. binti yupo nyumbani kwa likizo ya wiki 2, lakini ukweli hapati hata muda wa kupumzika au kufanya kazi zake za shule maana muda wote anafanya kazi za nyumbani.
Ni kweli napenda binti asaidie kazi za nyumbani, lakini kama leo nimejisikia vibaya sana sababu binti hapati muda wa kupumzika kama watoto wengine wa nyumba nyingine, dada wa kazi anataka kila kazi wafanye wote. Na mimi naona haipendezi kumwambia binti yangu apumzike wakati dada wa kazi anafanya kazi, hata kama ni kuosha vyombo.
Nimekuja hapa kuuliza wenzangu mnisaidie, nipangaje kazi ili dada ajue kuwa kazi za nyumbani ni wajibu wake yeye na siyo binti ambaye yupo hapa kwa muda tu?
Au wenzangu mnafanyaje?
NB: najua kuna wengine pia wanaishi na ndugu, wadogo zenu, mawifi, ambao ni wanafunzi, hao pia nawaweka kwenye kundi kama hili tu la binti. Mnapangaje hapo?
Natanguliza shukurani