Naomba ushauri kwa hili wana MMU

Naomba ushauri kwa hili wana MMU

mpangie binti yako muda wa kufanya kazi za shule mfano baada ya chakula cha jioni au mchana na umwambie dada wa kazi kuwa wakati huo ni wa binti yako kujisomea!so kama kuna kazi za ziada dada achukue jukumu la kuzifanya wakati huo!
Asante rafiki, nitafanya hivyo
 
Mpangie binti yako majukumu yake tena ambayo yatamfanya aweze kumaliza mapema na hivyo kupata muda wa kusoma na kupumzika pia na kuhusu huyo dada wa kazi mweleze kuwa hatakiwi kutaka usawa na binti yako kwani yeye unampa pesa kila mwisho wa mwezi kwa ajili ya kazi za ndani,muulize binti yako unamlipa shilingi ngapi?kama ni mwelewa na hana gubu atakaa chini na kutafakari na kisha kuchukua hatua nzuri.

na wala hutakiwi kuwa na hofu kuwa unamharibu bnitiyo kwa kumpa muda wa kupumzika na kujisomea nadhani mpaka hapo ulishamkunja angali mbichi na ndio maana umeona matunda yake kuwa ni mchapa kazi so naamini kamwe hatobadilika kwa huo msingi mzuri uliomwekea,ila kwa situation aliyonayo sasa hana budi kupitwa na baaadhi ya kazi ili ajisomee ni haki yake dada Fixed Point.
 
Last edited by a moderator:
Mpangie binti yako majukumu yake tena ambayo yatamfanya aweze kumaliza mapema na hivyo kupata muda wa kusoma na kupumzika pia na kuhusu huyo dada wa kazi mweleze kuwa hatakiwi kutaka usawa na binti yako kwani yeye unampa pesa kila mwisho wa mwezi kwa ajili ya kazi za ndani,muulize binti yako unamlipa shilingi ngapi?kama ni mwelewa na hana gubu atakaa chini na kutafakari na kisha kuchukua hatua nzuri.

na wala hutakiwi kuwa na hofu kuwa unamharibu bnitiyo kwa kumpa muda wa kupumzika na kujisomea nadhani mpaka hapo ulishamkunja angali mbichi na ndio maana umeona matunda yake kuwa ni mchapa kazi so naamini kamwe hatobadilika kwa huo msingi mzuri uliomwekea,ila kwa situation aliyonayo sasa hana budi kupitwa na baaadhi ya kazi ili ajisomee ni haki yake dada Fixed Point.
najionaje mwepesi sasa mdogo wangu! asante sana kwa huu ushauri.
 
Usiwaze sana best ni simple sana , Fixed Point wewe ni mama mzuri unayejua malezi na ninategemea wewe ni rafiki

kwao si adui,ongea nao wote wawili wakiwepo na panga majukumu as mama kwa upendo kabisa as family talk,mueleweshe

binti yako kwamba anahitaji kuwa na muda mzuri wa kusoma yupo likizo lakini masomo hayako likizo,akishamaliza

yale majukumu yake apumzishe mwili then asome na anaposoma haitajiki mtu yeyote kumsumbua hii iwe ni Strict to

all family members. Muelimishe dada pia umuhimu wa kufanya kazi kwa wakati na kumaliza mapema ili awe na muda wa

kupumzika. ALL THE BEST.
 
Last edited by a moderator:
Usiwaze sana best ni simple sana , Fixed Point wewe ni mama mzuri unayejua malezi na ninategemea wewe ni rafiki

kwao si adui,ongea nao wote wawili wakiwepo na panga majukumu as mama kwa upendo kabisa as family talk,mueleweshe

binti yako kwamba anahitaji kuwa na muda mzuri wa kusoma yupo likizo lakini masomo hayako likizo,akishamaliza

yale majukumu yake apumzishe mwili then asome na anaposoma haitajiki mtu yeyote kumsumbua hii iwe ni Strict to

all family members. Muelimishe dada pia umuhimu wa kufanya kazi kwa wakati na kumaliza mapema ili awe na muda wa

kupumzika. ALL THE BEST.
kumbe jambo ukilitoa kwa watu inakuwa kitu rahisi tu.....
nimewaza sana nifanyaje ili kutatua hili.
Asante sana rafiki kwa ushauri
 
Mueleze uyo dada wa kazi wala usione aibu,mm pia nina mtt ww dada angu,ilikua kama ww,dada wa kazi anataka waende sawa,juzi ninemuita,kwa upendo nikamwambia flani ni mwanafunzi,kazi zake nampangia mm,na akumbuke namlipa yy na c huyo mtt wa dada,so afanye kazi zake!na imekua hivyo,mueleze kwa upendo bila ukali!
 
Kwani huyo mtoto wako analalamika pindi afanyapo kazi pasu na huyo dada wa kazi??? Kama hanung'uniki mwache amsaidie dada kazi inaonekana kwanza wanaelewana vizur pili mwanao anajua wajibu wake kama mtoto wa kike sijaona ubaya wowote mdada!!
 
Samahani Fixed Point wewe ni baba au mama?
Nivizuri watoto wanapokua likizo wakafanya pia majukumu ya nyumbani wakishirikiana na wasaidizi wetu....na pia ni muhimu kwa mzazi kujua kwamba watoto wana JUKUMU KUBWA pia la Kujisomea na kufanya marudio ya masomo wawapo nyumbani.

Hapohapo ni muhimu wasaidizi wetu watambue kwamba wapo hapo kwa ajili ya kazi inayowapa kipato nikimaanisha kwamba wanatakiwa wayajue majukumu yao na kuyafanya ipasavyo

Binti yako anaweza kufanya kazi ambazo hazichukui muda mwingi kama kufanya usafi na kuendelea na kujisomea wakati msaidizi ataendelea na hizo nyingine - ikizingatiwa umesema hakuna kazi nyingi
 
Inakuaje binti yako afanye kazi sawa au zaidi ya msichana wa kazi? manake kaja hapo kwaajili ya kazi na mshahara analipwa, mimi kwetu tulikuwa na msichana wa kazi lakini pia mama yetu hakutaka kutulea malezi ya kutokufanya kazi kabisa alijitahidi tujue kazi, na tulijua lakini si kwa kufanya kazi sawa na mfanyakazi wetu, sana sana ilikuwa nguo zetu tunafua wenyewe, chumba chetu tunasafisha wenyewe, na kupika ilikuwa ni kumsaidia usiku tu tena yeye akipika mboga tutamsaidia kupika wali au chochote kile ambacho kinalika usiku huo au yeye akipika wali tutasaidia mboga lakini asilimia 90 ya kazi alikuwa anazifanya yye manake ndo zilizomleta
 
kumbe jambo ukilitoa kwa watu inakuwa kitu rahisi tu.....
nimewaza sana nifanyaje ili kutatua hili.
Asante sana rafiki kwa ushauri
karibu,asante nawe pia kwa kufunguka maana kupitia uzi huu wengi wataelimika.

Ila nimefurahi sana na ninakupongeza kwa kuuona umuhimu wa mtoto wa kike kujua kaz za nyumban,maana malezi ya siku hizi......??? Binti anakuja kuolewa hajui hata kudeki kisa masomo.

Big up mamaa na endelea kuwa mama mzuri!
 
hongera kwa kumfundisha binti yako kazi. suala simple tu, muite dada wa kazi, mwambie anatakiwa ajue majukumu yake vema hata kama binti atamsaidia. mwambie lipi atasaidiwa na lipi atatkiwa kulifanya mwenyewe. mwambie ukweli unataka binti yako nae apate muda wa kupumzika.
 
ha haaaa, ngoja nitengeneze work permit, lol!

binti yako si ni educated kiasi mamii??

kwani akiandika work report ni vibaya? lols..

ila seriously, mpe limit za aina gani za kazi afanye ili apate muda wa kupumzika,

usimfanye mrembo wetu akose amani ya kuwa likizo!..

btw, mwambie excel anamsalimia!,,.. lols!
 
Kukaa na dada muda mrefu hapo nyumbani kusimfanye asahau position yake kwakuwa likizo ni fupi mwambie dada mwanao aoshe kama ni vyombo asubuhi na vya mchana na kazi nyingine azihandle dada wa kazi
 
Mueleze uyo dada wa kazi wala usione aibu,mm pia nina mtt ww dada angu,ilikua kama ww,dada wa kazi anataka waende sawa,juzi ninemuita,kwa upendo nikamwambia flani ni mwanafunzi,kazi zake nampangia mm,na akumbuke namlipa yy na c huyo mtt wa dada,so afanye kazi zake!na imekua hivyo,mueleze kwa upendo bila ukali!
tatizo ni hilo la kuonea aibu dada wa kazi....
nataka naye ajione kama ni mmoja wa wanangu, ila sasa imekuwa too much
 
Kwani huyo mtoto wako analalamika pindi afanyapo kazi pasu na huyo dada wa kazi??? Kama hanung'uniki mwache amsaidie dada kazi inaonekana kwanza wanaelewana vizur pili mwanao anajua wajibu wake kama mtoto wa kike sijaona ubaya wowote mdada!!
mwanangu halalamiki, na wapo marafiki tu.
lakini sasa binti hapati muda wa kujisomea nyumbani, labda usiku wakati dada kalala.
sasa hapo kweli namtendea vema binti?
 
Samahani Fixed Point wewe ni baba au mama?
Nivizuri watoto wanapokua likizo wakafanya pia majukumu ya nyumbani wakishirikiana na wasaidizi wetu....na pia ni muhimu kwa mzazi kujua kwamba watoto wana JUKUMU KUBWA pia la Kujisomea na kufanya marudio ya masomo wawapo nyumbani.

Hapohapo ni muhimu wasaidizi wetu watambue kwamba wapo hapo kwa ajili ya kazi inayowapa kipato nikimaanisha kwamba wanatakiwa wayajue majukumu yao na kuyafanya ipasavyo

Binti yako anaweza kufanya kazi ambazo hazichukui muda mwingi kama kufanya usafi na kuendelea na kujisomea wakati msaidizi ataendelea na hizo nyingine - ikizingatiwa umesema hakuna kazi nyingi
Jamani, mimi ni mama..... ndo maana naongelea mambo ya kazi za nyumbani......
Binti anajua kazi zooote za home. kuna kipindi tunakuwaga peke yetu bila dada na tunajiweza tu.
Nitazingatia ushauri wako rafiki
 
Inakuaje binti yako afanye kazi sawa au zaidi ya msichana wa kazi? manake kaja hapo kwaajili ya kazi na mshahara analipwa, mimi kwetu tulikuwa na msichana wa kazi lakini pia mama yetu hakutaka kutulea malezi ya kutokufanya kazi kabisa alijitahidi tujue kazi, na tulijua lakini si kwa kufanya kazi sawa na mfanyakazi wetu, sana sana ilikuwa nguo zetu tunafua wenyewe, chumba chetu tunasafisha wenyewe, na kupika ilikuwa ni kumsaidia usiku tu tena yeye akipika mboga tutamsaidia kupika wali au chochote kile ambacho kinalika usiku huo au yeye akipika wali tutasaidia mboga lakini asilimia 90 ya kazi alikuwa anazifanya yye manake ndo zilizomleta
unajua napenda dada naye ajione yupo nyumbani....
sasa inakera kuona yeye ndo anajibweteka na kutaka kazi zote zifanywe na binti wakati yeye ndo anapata mshahara kwa hizo kazi.
 
karibu,asante nawe pia kwa kufunguka maana kupitia uzi huu wengi wataelimika.

Ila nimefurahi sana na ninakupongeza kwa kuuona umuhimu wa mtoto wa kike kujua kaz za nyumban,maana malezi ya siku hizi......??? Binti anakuja kuolewa hajui hata kudeki kisa masomo.

Big up mamaa na endelea kuwa mama mzuri!
Asante mamii....
niliamua nichukue style ya mamangu.....
sisi pia tulikuwa tunafanya kazi ingawa tulikuwa na dada, ukweli inalipa sana maana nafanya kila kitu mwenyewe.
tatizo wadada wa siku hizi ni wavivu, kwa hiyo anakwepa sana majukumu yake
 
hongera kwa kumfundisha binti yako kazi. suala simple tu, muite dada wa kazi, mwambie anatakiwa ajue majukumu yake vema hata kama binti atamsaidia. mwambie lipi atasaidiwa na lipi atatkiwa kulifanya mwenyewe. mwambie ukweli unataka binti yako nae apate muda wa kupumzika.
Asante rafiki, nitajitahidi........
leo usiku nitakaa nao kikao cha urafiki
 
Back
Top Bottom