Naomba ushauri kwa hili wana MMU

Naomba ushauri kwa hili wana MMU

Mie nimewagawanyisha kazi, kijana bado mdogo. Nimempangia kazi ya kuandaa meza wakati wa kula, kutoa vyombo tukimaiza kula, kusuuza vyombo wengine wakiosha. Kazi za kutumwa tumwa nyiingi zote ni zake, sijui kupika chai jioni, leta maji ya kunywa, tafuta rimoti, funga mapazia jioni.

Dada kupika, usafi na kufua.

Wa boarding wakija sababu wao wakubwa, nampunguzia dada baadhi ya kazi zinakuwa zao. Ukizubaa, dada anakuwa bosi wa watoto wako. Mie kuna siku alinishangaza, nilimtumanaye akamtuma kijana wangu, kidogo nimlambue.
wadogo wana kazi zao, sheshe ni hawa mabinti....
binti wa kazi sasa anataka kuona ana msaidizi ambaye anafanya kazi zake zote, lol!
 
hongera mtoto unamfundisha kufanya kazi..ila km walivosema wadau wengine guve her more time to enjoy her life at home ,sio kila saa aende sawa na dada wa kazi...
Nakumbuka when i was little my mom was sooo strict yani kazi mwanzo mwisho ht km beki3 yupo,and i hated my home just for that..japo imenifundisha,sikupenda
 
Sidekezi mtoto wangu hata siku moja. Lazima afanye kazi kama mtumwa, hata kwa bahati mbaya Mungu akiniondoa wakati yeye bado ajaweza kujitegemea aweze kuishi maisha popote bila matatizo. Kazi afanye as well lazima atenge muda wa kujisomea. Alllllaaaa!!!!!!!
 
kabla binti hajarudi likizo dada alikuwa anafanyaje hizo kazi mpaka sasa aone ni nyingi? na mie nilikuwa napenda kumfanyia hivyo hivyo binti yangu(wa msukuma) lakini niliona dada yeye ndio anataka kumgeuza binti mfanyakazi pale ndani, unatoka kazini binti kanywea kachoshwa na makazi, nilimdadisi alivyokuja kuniambia anachoshwa na kazi za ndani aisee, nilimwita dada hapo hapo nikamwambia huyu kaja mapumziko hapa atakusaidia vikazi vidogo vidogo eg mchana mkimaliza kula aoshe vyombo vyenu sio binti pasu pasu na dada, hapana kabisa.
kazi alikuwa anafanya mwenyewe zote, na muda wa kulala mchana anaupata. ila sasa anataka kuajiri naye ili apumzike. Leo ndo kagoma kufanya lolote, tumefanya kazi zote na mwanangu...
 
Hyo ipo hz habar za kutegeana kazi jaman mmh kama hujataja jina ujue imekula kwako aidha hyo kaz icfanyke au afanye yule mwenye wito
ha haaaa, kazi ni pale ambapo mwenye wito ndo ambaye siyo mwajiriwa, lol!
 
sawa kabisa, halafu sasa mie wangu alivyoona binti anachapa kazi pasu pasu yeye muda wake ni simu simu na yeye,juzi nilimchenjia kuongea na simu za kimahaba mbele ya wanangu ni No, nilivyomchenjia hivyo akaninunia, jana asubuhi ananiambia dada nataka kwenda nyumbani leo leo, nilimuuliza tu unanidai, sikudai, haya funga funga nikupeleke stendi, simu kwao binti yenu anarudi huko, mama wa binti mkarimu kweli anabembeleza kuniuliza kulikoni, nikamwambia mama ngoja nikawafungashe na watoto niwahamishie kwa dada yangu then nikitulia ntakucal tuongee, leo mdada anani beep kuanzia asubuhi, kumcal ananiomba msamaha shetani alimpitia, anaomba kurudi na na kilio juu, nadhani mama yake alimchenjia huko, mxsiii ukiwanyenyekea hawa ni majanga.
Juzi nimenyang'anya simu, jana nimenyang'anya karata......
yaani kuna kazi kibao yeye anacheza karata na binti...... kweli jamani!
simu ndo janga la Taifa nadhani
 
mie nimeona hawa wadada wa kutukanwa tukanwa ndio wanakaa kwa heshima majumbani, nina rafiki yangu kumtwanga/tukana dada ni dk sifuri, lakini wadada wanakaa haswaaa, alienae sasa hivi wanafikisha miaka mitano, mie kuanzia dada yangu aliewalea watoto wangu wote alivyoniambia anaenda kuendeleza maisha kwao kigoma huko, nakomaje sasa, nimebadilisha huyu wa nne sasa, na ni kuanzia last sept, mie sijazoea kupigishana makelele, narudi huko na lager zangu kelele nawezea wapi, lakini hawa wananifanya nizipige aisee, mana unarudi 12 jioni mtoto mdogo hajaogeshwa, mara huku nguo za watoto walizotoka nazo shule hazijafuliwa, mara wali mbichi, khaaa namkumbukaje dada yangu yule jamani.
ha haaa, angalia wale wa kwa wahindi wanavyodumu.....
Mimi ukweli siwezi kunyanyasa dada wa kazi, napenda nikae naye kama mdogo wangu. ma hivi napenda kufanya kazi za home hasa kujipikilisha basi wadada wanaona ni haki yao mimi kuwapikia.........
wananipandaje sasa!
 
mpangie kazi za kufanya yeye peke yake(mwanafunz). Mfano sie hapa home iko hivi, mwanafunzi(mtoto wa dadangu) anaosha vyombo vya jioni basi, kwa siku anazoenda shule. Siku haendi shule atafanya usafi na kuosha vyombo usiku basi, kazi nyingine hazimuhusu. Jaribu nawe kuangalia utaratibu kama huo
 
Fixed Point usithubutu kumwambia binti yako afanye kazi chache nyingine amwachie binti wa kazi mwache afanye kazi kadri apendavyo anajijengea tabia njema ta uwajibikaji yupo likizo ni ya muda mfupi ndo wajibu anapokuwa likizo tena shukuru Mungu umepata anayependa kuwajibika .mwenyewe.
na mimi sijasema asifanye kazi kabisa. nimeona sasa anakosa kabisa muda wa kupumzika na kujisomea. akiwa likizo haimaanishi asisome hata masaa kadhaa kwa siku.
Na inaudhi zaidi pale ambapo dada anaona yeye ndo ana haki ya kukaa akamwachia kazi zote binti..... na kumtuma juu!
 
hongera mtoto unamfundisha kufanya kazi..ila km walivosema wadau wengine guve her more time to enjoy her life at home ,sio kila saa aende sawa na dada wa kazi...
Nakumbuka when i was little my mom was sooo strict yani kazi mwanzo mwisho ht km beki3 yupo,and i hated my home just for that..japo imenifundisha,sikupenda
Asante dear kwa ushauri, nitampa mapumziko ya kiaina
 
iliwahi nitokea nikiwa darasa la 6 alikuja dada wa kazi ambaye nilimchukia kwa kipindi kile ila alinifundisha kazi,ila jambo la tofauti ni kwamba miminsikuwa nazijua kazi so akipika ananiita nikae pale,akiosha viombo ananiita niangalie then ananiachia rundo la viombo,nguo alafu nilikua mdogo,mama siku moja akapanga kazi kwamba mimi nitakua naosha vyombo yva mchana na kutenga msosi lakini kwa sharti moja muda wa kupika niwe jikoni mweeee mpaka leo mambo ya jikon hayanishindi ila mama asingeingilia kati nyumbank nilishapachukia So wewe ndo maza haus hilo jambo dogo sana kuamua
 
mpangie kazi za kufanya yeye peke yake(mwanafunz). Mfano sie hapa home iko hivi, mwanafunzi(mtoto wa dadangu) anaosha vyombo vya jioni basi, kwa siku anazoenda shule. Siku haendi shule atafanya usafi na kuosha vyombo usiku basi, kazi nyingine hazimuhusu. Jaribu nawe kuangalia utaratibu kama huo
nimeipenda hii ratiba......
wangu yupo boarding, kwa hiyo likizo ndo anakuwa home, haendi shule.
 
ha haaa, angalia wale wa kwa wahindi wanavyodumu.....
Mimi ukweli siwezi kunyanyasa dada wa kazi, napenda nikae naye kama mdogo wangu. ma hivi napenda kufanya kazi za home hasa kujipikilisha basi wadada wanaona ni haki yao mimi kuwapikia.........
wananipandaje sasa!


tatizo lao ndio hilo wakipendwa hawapendeki sasa, mpaka mturutane, hahaha huyu wangu ikipikwa nyama, kuku/ng'ombe ndio atatuliza kichwa kwenye mapishi mana utakuta mapaja hayapo, sijui mgongo haupo, mie nasemaga atazoea tu ataona vya kawaida, ngoja wali maharage sasa, utakuta wali/maharage mbichi.
 
kazi alikuwa anafanya mwenyewe zote, na muda wa kulala mchana anaupata. ila sasa anataka kuajiri naye ili apumzike. Leo ndo kagoma kufanya lolote, tumefanya kazi zote na mwanangu...

Hapana kwa kweli! usilifumbie macho kabisa hili,je umemuuliza kisa cha mgomo baridi???
 
tatizo lao ndio hilo wakipendwa hawapendeki sasa, mpaka mturutane, hahaha huyu wangu ikipikwa nyama, kuku/ng'ombe ndio atatuliza kichwa kwenye mapishi mana utakuta mapaja hayapo, sijui mgongo haupo, mie nasemaga atazoea tu ataona vya kawaida, ngoja wali maharage sasa, utakuta wali/maharage mbichi.
ha haaaa, umenikumbusha kitu hapa rafiki, lol!
hawa watu ni wa kuishi nao kwa akili sana yaani
 
Yaani hawa ma housegirl wa siku hizi mnawadekeza hadi basi.....fukuza huyo housegirl first
 
Kwa hiyo unasema mwepesi unapenda afanye kazi za ndani. Umemshusha dhamani mbelezxunategemea nini?

Shule umlipie child labour umfanyishe na inaelekea haujali masomo yake wewe mwanamke bila hivyo usingekaa chini hadi leo eti unalalama kuhusu masomo.

Haumlipi pesa, hg unamlipa so endelea kusevu pesa zako za kutokuwa na hg 2 unaowahitaji hapo kwako.
 
tatizo lao ndio hilo wakipendwa hawapendeki sasa, mpaka mturutane, hahaha huyu wangu ikipikwa nyama, kuku/ng'ombe ndio atatuliza kichwa kwenye mapishi mana utakuta mapaja hayapo, sijui mgongo haupo, mie nasemaga atazoea tu ataona vya kawaida, ngoja wali maharage sasa, utakuta wali/maharage mbichi.

Loh! umenichekeshaje? ukanikumbusha na mie visa vyangu, hawa wasichana basi!!!
 
Tupe kwanza maendeleo ya mwanao huko shule ndipo tuweze kushauri vzr.
Pengine binti yako anajua kutenga vizuri muda wake wa kujisomea na hapendi kumuona househelp akifanya kazi pekeyake. Watoto wa kike/wengine hawapendi kuona matabaka yanayoashiria utumwa ndani ya nyumba.
Kuingilia uhuru wa binti yako anaweza akuchukulie tofauti na kukuona ww kama Mama ndani ya nyumba u mbaguzi wakati hapo awali ulimjenga vizuri kushiriki kazi za nyumbani.
Jingine zuri, unaweza kumtenganisha huyo binti ktk ushiriki wa kazi kwa muda mrefu hapo nyumbani kwa kumtaftia tuition ili apate ulazima wa kujisomea yale atakayofundishwa huko tuition. Hii ni njia nzuri ambayo haitaleta sononeko kwake na kwa dada wa kazi.
Nafikiri umenisoma mkuu!
 
Back
Top Bottom