Fixed Point
JF-Expert Member
- Sep 30, 2009
- 11,304
- 12,753
- Thread starter
- #121
Asante sana......una bahati kupata huyo binti. mi alikuja mtt wa wifi akiwa teenager, alikaa kwangu muda wa kutosha tu, mbona nilijuta. akiamka asubuhi anawasha TV miguu juu ya sofa anasubiri dada apike chai. Hata akikuona mama mwenye nyumba unachakalika yeye hajali. kumuuliza mbona humsaidii dada hata kupika chai, akanijibu yeye dada ndio msaidizi wa kazi, ndio majukumu yake.
ila pia kuna wtt wanapenda kumsaidia dada kazi za ndani kuliko kusoma. hakikisha binti anapata muda mzuri wa kujisomea, na aelewe umuhimu wa shule pia
Mimi pia hapa kwangu huwa wanakuja mabinti watoto wa ndugu zangu au wa upande wa pili huwa ni majanga.
Na mimi ukweli huwa silazimishi mtoto wa watu afanye kazi, kama kwao hawafanyi basi hawezi anzia kwangu, after all, ni mpita njia tu.