Naomba ushauri kuhusu dini

Sito kwamba yeye alikuwa mkweli bali alikuwa mkweli na muaminifu na hili pia walilishuhudia maadui zake. Sasa utaona lipi zito halo kati ya kujishuhudia mwenyewe au wale walio kupiga vita wakakiri ya kuwa weww ni mkweli na muaminifu.

Naanzia hapa :

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipapanda juu ya jabali Swafaa akawaita watu wake na kuwaambia: "Enyi Maquraysh (na riwaayah nyingine enyi Banuu Manaaf, Enyi Banuu fulani na fulani). Je, ikiwa nitawaambieni kuwa wapanda farasi wapo nyuma ya jabali hili wakijitayarisha kukushambulieni, mtanisadiki?" Wote kwa pamoja wakamjibu:

"Bila shaka tutakusadiki, kwa sababu hatujapata kusikia kutoka kwako isipokuwa maneno ya kweli." Akasema: "Basi mimi ni mwonyaji kwenu juu ya adhabu kali iliyo mbele yenu. Okoeni nafsi zenu kutokana na moto…" [Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo kwa riwaayah tofauti]

Kisha naendela na hapa :

Hii ni kauli ya Abu Jahl, huyu alikuwa akimpinga Mtume, lakini alikiri juu ya ukweli na uaminifu wa Mtume.

“Wa-Allaahi mimi najua vilivyo kuwa yeye ni Mkweli….Tulikuwa tukimwita katika ujana wake Asw-Swaadiq Al-Amiyn.” (Mkweli Mwaminifu). [Tafsiyr Al-Qurtwubiy]

Kisha narudi hapa :

Na yule aliyekuja na ukweli na wakausadikisha - hao ndio wenye taqwa. [Az-Zumar: 33]

Amesema Mujaahid na Qataadah na wengineo kuhusu: “Na yule aliyekuja na ukweli” “Huyo ni Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)” [Tafsiyr Ibn Kathiyr]

Misho wa kunukuu.

Nakukumbusha maswali yangu :

1. Yesu ni njia, je ni njia ya kuelekea wapi ?

2. Mwanga wa Yesu ni upi ?

3. Kwanimi Yesukila jambo alikuwa analielekeza kwa Mola muumba ?
 
Kwenye Qur'aan hilo liko wazi. Nakuiliza wewe ambaye unalazimisha mfanano wa Yesu na Allah, ndiyo utuambie Yesu huo mwanga wake ni upi ?

Sababu kila andiko Yesu analirudisha kwa Mola wake aliye mtuma. Sasa tuambie Yesu alimaanisha nini kusema yeye ni mwanga na yeye ni uzima ? Nataka utupe maana aliyo itoa Yesu mwenyewe.
 
Aya umeweka kwamba muhammad yale aliyoleta ndio kweli tofautisha na Yesu kasema yeye ndio kweli yenyewe , Yesu ndio njia ya Kwenda mbinguni lazima umfuate yeye na kweli ilikuwa sifa yake ya kiungu

Allah anasema Koran 22:62. Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Wa Kweli,....

Yesu anatoa jibu John 14: 6Yesu akamjibu, “Mimi ni njia, na ukweli na uhai.
 
Allah anamtaja Mwenyezi Mungu ni mwanga , jibu ndio hili na lipo wazi
Koran 24:35. Mwenyezi Mungu ni Mwanga wa Mbingu na Ardhi....

Yesu anajitaja yeye ni mwanga
John 8:12 Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, “Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu.
 
Kijana hivi mfano Yesu aliposema yeye ni Njia ina maana alimaanisha yeye ni mungu ?

Kijana usikate andiko alisema hivi kwa ukamilifu :

, “Mimi ndiye Njia na Kweli na Uzima; mtu hawezi kufika kwa Baba bila kupitia kwangu. "

Hapo mitume wote huwa hawesemi uongo, na kweli ni ile aliyo tumwa na Mola. Sasa vipi mtume aseme ukweli halafu asiwe mkweli ? Aliitwa mkweli na muaminifu sababu alikuja na ile kweli toka kwa Allah.
 
Allah anamtaja Mwenyezi Mungu ni mwanga , jibu ndio hili na lipo wazi
Koran 24:35. Mwenyezi Mungu ni Mwanga wa Mbingu na Ardhi....

Yesu anajitaja yeye ni mwanga
John 8:12 Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, “Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu.
Allah anamtaja Mwenyezi mungu ndiyo nini ?

Nimekuuliza swali rahisi, maana ya Yesu kuwa ni mwanga ni nini kwa mujibu wake Ywsu yeye mwenyewe. Nasubiri jibu hapa.
 
Kama ulivyo sema umri ...naamini kwa umri uliyo nao ni dhahiri unafanya kitu ukiwa na utimamu wa akili nakushauri amani ya moyo ni kila kitu kama moyoni una amani fanya kile unacho jiskia usiwaze watu watakuchukuliaje
 
Allah ankujibu
Allah anasema Koran 22:62. Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Wa Kweli,....

Yesu anatoa jibu John 14: 6Yesu akamjibu, “Mimi ni njia, na ukweli na uhai.
 
Allah anamtaja Mwenyezi Mungu ni mwanga , jibu ndio hili na lipo wazi
Koran 24:35. Mwenyezi Mungu ni Mwanga wa Mbingu na Ardhi....

Yesu anajitaja yeye ni mwanga
John 8:12 Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, “Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu.
Kingine nilikuuliza kwanini Yesu kila analosema analorudisha kwa yule aliye mtuma ? Yeye kama ni mungu kwanini asinge sema tu mimi nimesema hivi, akamaliza.
 
Kajishusha??? Tuhuma hizi ni world wide. World wide ndugu na ni kama mila pale katoliki. Kuhusu maustazi hawa wa mwendokasi ni ujinga tu uliopo hapa bongo lakini sio world wide issue
Upo serious ama? Unataka kusema maustazi wanaobaka wapo limited kwa Tanzania pekee?
 
Allah ankujibu
Allah anasema Koran 22:62. Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Wa Kweli,....

Yesu anatoa jibu John 14: 6Yesu akamjibu, “Mimi ni njia, na ukweli na uhai.
Kisha Yesu akamaliziaje kwenye hilo andiko ? Jiulize kwanini kwanini hakuishia hapo ulipoishia wewe ?
 
Allah anamtaja Mwenyezi mungu ndiyo nini ?

Nimekuuliza swali rahisi, maana ya Yesu kuwa ni mwanga ni nini kwa mujibu wake Ywsu yeye mwenyewe. Nasubiri jibu hapa.
Kwa hiyo hutaki tena majibu ya Allah
Allah anasema Mung ni mwanga Koran 24:35. Mwenyezi Mungu ni Mwanga wa Mbingu na Ardhi....

Yesu anajitaja yeye ni mwanga
John 8:12 Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, “Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu.
 
Wewe haujasoma dini yani upo upo tu unafuata upepe

Quran inasema : Na anaetaka dini isiyokuwa ya kiislam haitakubaliwa kwake
 
Allah ankujibu
Allah anasema Koran 22:62. Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Wa Kweli,....

Yesu anatoa jibu John 14: 6Yesu akamjibu, “Mimi ni njia, na ukweli na uhai.
Kisha katika hiyo aya ya 62, Allah akasema haya :

22 : 62. Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Wa Kweli, na kwamba wale wanao waomba badala yake, ni baat'ili, na hakika Mwenyezi Mungu ndiye Aliye Juu na ndiye Mkubwa.

Mbona hujatuonyesha wapi Yesu akisema aabudiwe ? Hii ni maana ya kuwa Yesu si Mungu.

Sasa uwe unalinganisha maneno kwa ukamilifu.
 
Mimi sina dini kwa hiyo sijui nimekaririshwa nini!!! Anyways kuna mahala kwenye hii thread nimesoma ya kwamba mleta mada hata kiarabu hajui ndio maana nikauliza sala zenu zinasikika kwa Mungu kupitia lugha ipi.

Kama sala yako inasikika kwa lugha yoyote ile kuna ulazima upi wa kujua kiarabu? Pia hujajibu swali langu kuhusu kitabu chenu kitakatifu, kipo kwenye lugha ipi?
 
Kisha Yesu akamaliziaje kwenye hilo andiko ? Jiulize kwanini kwanini hakuishia hapo ulipoishia wewe ?
Nimeweka point ya Yesu Kuwa kweli na Imani Yetu ni Kwamba Kuna Mungu Baba , Mwana na Roho mtakatifu zote ni divine
Allah anasema Koran 22:62. Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Wa Kweli,....

Yesu anatoa jibu John 14: 6Yesu akamjibu, “Mimi ni njia, na ukweli na uhai.

Yesu raha sana anajitaja kabisa , ila allah ana refer kwa Mungu yani ni yeye allah anaongea alafu anasema "Mwenyezi Mungu ndiye Wa Kweli"
 
22 : 62. Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Wa Kweli, na kwamba wale wanao waomba badala yake, ni baat'ili, na hakika Mwenyezi Mungu ndiye Aliye Juu na ndiye Mkubwa.
Safi kabisa Allah anasema Mungu ndiye kweli

Yesu natoa jibu Yeye ndie kweli
John 14: 6Yesu akamjibu, “Mimi ni njia, na ukweli na uhai.
 
Kwa hiyo hutaki tena majibu ya Allah
Allah anasema Mung ni mwanga Koran 24:35. Mwenyezi Mungu ni Mwanga wa Mbingu na Ardhi....

Yesu anajitaja yeye ni mwanga
John 8:12 Yesu alipozungumza nao tena, aliwaambia, “Mimi ndimi mwanga wa ulimwengu.
Kwa ukamilifu wa aya hiyo uko hivi :

35. Mwenyezi Mungu ni Nuru ya Mbingu na Ardhi. Mfano wa Nuru yake ni kama shubaka lenye kuwekwa ndani yake taa. Taa ile imo katika tungi. Tungi lile ni kama nyota inayo meremeta, inayo washwa kwa mafuta yanayo toka katika mti ulio barikiwa, mzaituni. Si wa mashariki wala magharibi. Yanakaribia mafuta yake kung'aa wenyewe ingawa moto haujayagusa - Nuru juu ya Nuru. Mwenyezi Mungu humwongoa kwenye Nuru yake amtakaye. Na Mwenyezi Mungu huwapigia watu mifano. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye kujua kila kitu. (an-Nur : 35)

Nakataa vipi hali toka kwa Mola wangu, na huo Allah alitumia kama mfano. Ndiyo maana nataka uniambie maana ya Mwanga wa Yesu ni nini ? Sababu hiyo lugha ni ya mfano, sasa tuambie Yesu alimaanisha nini aliposema yeye ni Mwanga wa ardhini, nataka utuwekee andiko alilosema yeye mwenyewe akilitolea ufafanuzi.
 
Haya ya mungu baba mnayasema nyinyi hajasema Yesu haya. Kwahiyo achana nalo hamuwezi kulitetea.

Nataka umalize andiko usilete dibaji za mungu baba wala mwana wala roho mtakatifu huu mlango unaoingia kaa ukijua huwezi kutoka.

Qur'aan ni muujiza kuanzia uandishi wake na maana zake, Mtume ndiyo ananukuu Qur'aan kwahiyo lazima aisome kama ilivyo kuja ndiyo maana kuna sehemu Qur'aan inamuweka sawa mtume na mfano wa hayo, kwahiyo inaonyesha wazi huijui Qur'aan.
 
Allah anaongea alafu ana refer kwa Mungu kweli ni muujiza ,

Allah anasema Koran 22:62. Hayo ni kwa kuwa Mwenyezi Mungu ndiye Wa Kweli,....

Yesu anatoa jibu John 14: 6Yesu akamjibu, “Mimi ni njia, na ukweli na uhai.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…