Mimi ni mwajiliwa wa taasisi fulani inayohusika na maswala ya ununuzi, nimeajiriwa tangu mwaka juzi. Tatizo nililonalo ni huyu boss wangu amekuwa ni mtu wa hasira sana ukikosea kidogo tu lazima achukue siku nzima kukusema na yupo radhi hata wekeend akupgie simu mtoke wote ila mkifika kwanye huo mtoko lazima akuanzishie mambo ya ofisini na kukusema tena kibaya zaidi ukimjibu ndo anazidisha mara ooh mpumbavu we hutumii akili yani inshort napata wakati mgumu natamani kuacha kazi ila nashindwa kwan familia inantegemea.
Nimejiuliza kwa watu wake wakaribu wanadai sio wewe tu ndivyo alivyo kwani ni mtu anayeamini yuko sahihi kwa kila kitu na pia jeuri ya fedha inampa kiburi
Tafadhari naomba ushauri wenu nifanyeje ili niweze kuendana na huyu boss wangu.