Naomba ushauri juu ya huyu boss

Mimi ni mwajiliwa wa taasisi fulani inayohusika na maswala ya ununuzi, nimeajiriwa tangu mwaka juzi. Tatizo nililonalo ni huyu boss wangu amekuwa ni mtu wa hasira sana ukikosea kidogo tu lazima achukue siku nzima kukusema na yupo radhi hata wekeend akupgie simu mtoke wote ila mkifika kwanye huo mtoko lazima akuanzishie mambo ya ofisini na kukusema tena kibaya zaidi ukimjibu ndo anazidisha mara ooh mpumbavu we hutumii akili yani inshort napata wakati mgumu natamani kuacha kazi ila nashindwa kwan familia inantegemea.

Nimejiuliza kwa watu wake wakaribu wanadai sio wewe tu ndivyo alivyo kwani ni mtu anayeamini yuko sahihi kwa kila kitu na pia jeuri ya fedha inampa kiburi

Tafadhari naomba ushauri wenu nifanyeje ili niweze kuendana na huyu boss wangu.
Pole sana mkuu mungu akupe tahfif katika kipindi hiki kigumu,
kuna mambo mawili matatu ningependa kukushauri,
kila jambo katika maisha ili kuliamuwa ni lazima kupima faida na hasara ,kuliendea au kuliacha ,
Na swala la boss wako ni kiasi cha kukaa chini na kupima je Matatizo yake ni makubwa kuliko faida za uwepo wako apo kazini?
jibu utalopata utajua nini cha kufanya
maana waswahili wanasema heri kufa umesimama kuliko kuishi kwa kupiga magoti
Riziki mungu ndio anatoa na hakuna anayejua ya kesho zaidi yake mwenyewe mungu,mtumaini sana yeye katika kila jambo lako na maamuzi yake,sote inawezekana tunakosea katika maamuzi ila sio yeye

siku njema mkuu na pole tena kwa majanga
 
Mimi ni mwajiliwa wa taasisi fulani inayohusika na maswala ya s wangu.
take easy mkuu kikubwa ushamuelewa ni mtu wa aina gani mbona hayo mambo yako sana tu mkuu wala usifikirie kuacha kazi la msing tu tambua yule ni bosi wako na ww ni mfanya kazi tu wa kawaida so fuata ya kwako chukulia tu hio kama changamoto yakukufunza tu na ww utafute mkwanja ili uondokane na manyanyaso ya kishamba kama hayo
 
Mpigie Afisa unajiri nafatilia haki za mwajiriwa.. zitakulinda ila kama ni mtu binafs tafuta sehemu nyngine usiogope kwamba hutopata tena kwani hiyo kazi ulipataje? utotoni ulikuwa unajua? Naam
 
Jimbu ni moja tu ameathirika mi nimekaanao sana hawa watu. So Fanya kazi kawaida tu!
 
= mwajiriwa
= tafadhali

Kwa mwandiko huo tu unaonesha uko "bogus".

Kama unabisha wewe siyo "bogus" basi tuwekee hicho ambacho unaona hujakosea na "boss" wako akakulaumu bila yeye kuwa sahihi.

Nnauhakika hutoweza kukiweka, that's how much bogus you are.
Hahahahahaha
You made my day
 
Siku nyingine akikutoa out then akaanzisha mboyoyo mboyoyo za ofisini unamtia vitasa vya maana then kesho yake unamuomba msamaha na kumwambia ni pombe
 
= mwajiriwa
= tafadhali

Kwa mwandiko huo tu unaonesha uko "bogus".

Kama unabisha wewe siyo "bogus" basi tuwekee hicho ambacho unaona hujakosea na "boss" wako akakulaumu bila yeye kuwa sahihi.

Nnauhakika hutoweza kukiweka, that's how much bogus you are.
Faiza fox my dada leo hauko sawa huyu anaomba ushaur na wala hujataka kujua kazi yake kama ni kubeba zege inahusiana nini na kuandika anaomba ushaur msaidie
 
kumbe wotr wanaume bhn ,mchane tu mpe makavu live,wote mmeajiriwa hpo hmna mwenye kkampun hpo xo oneday anaweza toka yy au ww,izo kaz tu afu mchane akinuna achana nae,,usiogope kufukuzwa cz ndo source ya manyanyaso yotr hayo
 
Mimi ni mwajiriwa wa taasisi fulani inayohusika na maswala ya ununuzi, nimeajiriwa tangu mwaka juzi.

Tatizo nililonalo ni huyu boss wangu amekuwa ni mtu wa hasira sana ukikosea kidogo tu lazima achukue siku nzima kukusema na yupo radhi hata weekend akupgie simu mtoke wote ila mkifika kwanye huo mtoko lazima akuanzishie mambo ya ofisini na kukusema tena kibaya zaidi ukimjibu ndo anazidisha mara ooh mpumbavu we hutumii akili yani inshort napata wakati mgumu natamani kuacha kazi ila nashindwa kwan familia inantegemea.

Nimejiuliza kwa watu wake wakaribu wanadai sio wewe tu ndivyo alivyo kwani ni mtu anayeamini yuko sahihi kwa kila kitu na pia jeuri ya fedha inampa kiburi

Tafadhali naomba ushauri wenu nifanyeje ili niweze kuendana na huyu boss wangu.
mmh mtoto wa kiume OUTING HIZO angalia isije ikawa anataka 0713 aka mtandao wa kijanja zaidi
 
Kukaa na boss tupige gambe hata iweje siwez maana nnaweza nkawaka nkatoa ya moyon jumatatu nkakuta barua kwa secretary
As long as ushaambiwa ndivyo alivyo ishi nae kw namna hyo then kama vip mpe ya kwake tena huko kwenye mitoko yenu na jumatatu hawez kuleta case ofisn
 
Muwekeeni sumu afe,,,,,,,,, mambo gani ya kutiana stress. Usawa wenyewe mgumu .
 
Pole sana... Hizo tabia wanazo maboss karibia wote... hata wewe ukija kuwa boss utaona jinsi utakavyuokuwa... Vumilia kwa sasa...
 
Back
Top Bottom