Story yako inafanana kabisa na watu fulani hivi hapo nyuma kidogo:
Ilikuwa hivi;
Walikutana wakati wamemaliza advance wakaanza kudate, kisha ukafika wakat wa kuanza michakato ya ku apply vyuo, mwanaume akamuomba msichana asiapply kwanza asubirie mwanaume apply kisha aone atapangiwa chuo gani na mambo yataendaje!
Basi mwanaume akafanikiwa kuchaguliwa chuo kimojawapo hapa Tz na akafanikiwa kuanza masomo.
Wakat akiwa shule mwanzoni mapenzi yao yalikuwa moto moto sana simu kila mara iko sikion watu wanalonga mahuba yao.
Ikakata miezi 3 had 6 mbele, jamaa akaanza kuona ni ushamba kuwa na demu huko kijijini ilihal wapo pale arround wanaojua kuvaa mini sket, headphone masikion nk,
Akaanza ku approach dada mmoja hivi, yule dada akamkubalia akalamba asali sasa ili aoneshe yuko serious ikabidi adrop mawasiliano na yule wa kwanza, si unajua tena ukipata kipya unachunguzwa na kuvhunguzana, sema bahat nzuri yule dada wa chuo alikuwa mzuri sana kama jokate na akawa anamdhalau namna fulani mvulana, ikafika siku mwanamke huyu wa chuo akamuacha mwanaume! Daah jamaa akawaza na zile confusion za kuachwa gafla na stress za hapa na pale akasema haiwezekan kwanza nina mpenz ananipenda zaidi yako ishia nenda zako.
Jamaa akakata nauli akamfuata yule wa kijijin alieishia advance akaja nae chuoni wakapanga wakawa wanaishi mtaani lakin lengo kubwa ninavyohisi ni zile paniking za kuachwa na kutaka kumuonesha aliemuacha kwamba amepata new lady ndani ya muda mfupi.
Ni kweli wakaishi pa1 hadi kumaliza chuo pamoja na changamoto za hapa na pale.
Baada ya hapo mwanaume akatafuta kazi akapata mkoa tofauti na alipoachwa huyu mchumba wake na wakat huo alikuwa na mtoto mmoja tayari kazalishwa.
Huko alikopata kazi walau kamshahara na malupu lupu yakawepo kilichofatia hakutaka kumuita huyu mpenzi wake, mpenzi wake akatumia nguvu na vishawishi ikiwemo kusema mtoto yuko taaban hoi kufa kila mara ikafika mahali kuepusha usumbufu jamaa akaamua kumuita kishingo upande.
Kule kazini jamaa akapta wenye mishahara wenzake tena wanofanya nao warsha za mikoani na safari za hapa na pale za kazini zisizoisha basi akanogewa huko.
Akatangaza ndoa huko kwa wengine kisa eti huyu hana elimu, hana kazi, hayuko smart.
Dada wa watu akachanganyikiwa akaanzisha timbwili daily kulia,daily kumfuata nyuma mwanaume na kuvizia mademu wa jama na kuanzisha mbwai mbwai anatumkiwa hatakiwi ila hasikii yan ni full fujo.
Mdada akatumia njia ya kukosanisha amani kwa mshikaji kama njia ya kufikia lengo lake kwamba yeye alimuharibia basi asitegemee yeye kuachwa lazima amugaribie tu.
Naona zile fujo za haja maana daily kuvunjiana simu, kuloanishiwa nguo, kuchaniwa nguo nk jamaa akasalender akamuoa kwa shingo upande.
Wapo wanaishi had sasa.
Somo langu hapa ni kwamba unaweza wekeza moyo wako kwa mwanaume na ukaacha vitu vya msingi sana hasa elimu vikakupita kisha ukaja kujutia akakubadilikia.
Shika elimu kwanza huyu elimu huwa mkombozi pale unapoweza kuachwa na kila kitu.
Mapenzi yapo ila elimu nzuri ni ile unayoipata with in time na with in stage nikimaanisha huna watoto wala majukumu ya kuambiwa toka darasni upokee simu yangu.
[emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125]