Naomba msaada; Mchumba hataki mimi niende kusoma

Naomba msaada; Mchumba hataki mimi niende kusoma

Nenda kasome mrembo, mume mtarajiwa asiyetaka maendeleo yako ya aina yoyote ile ikiwemo elimu hakufai. Kumbuka elimu ni ufunguo wa maisha. Kila la heri na baraka kwenye masomo yako.

Habari zenu wanajamvi,

Naomba ushauri kutoka kwenu,

Mimi ni binti wa early twenties na nina mchumba ambae mpaka kwa wazazi anajulikana na Mungu akipenda mwaka huu tutaoana.

Kilichonileta hapa ni hiki kuanzia mwaka Jana nilikua nataka nianze process nirudi shule nilipomshirikisha huyu mchumba kakataa kabisa tena kaenda mbali zaidi na kuniambia siku utakayokwenda shule kata mawasiliano na mimi.

Na mimi nimemwambia mbona inawezekana kwenda chuo na mambo yote yakaendelea kama kawaida lakini bado ameshikilia uzi huohuo wa mimi nisiende chuo.

Naombeni ushauri nisimamie wapi maana najikuta nawaza nashindwa kujua ni choose ni kitu gani.

Nb: Yeye amesoma
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ninakukwaza mkuu? Basi ntapunguza!
Mwacheni achukue maamuzi yake akiharibikiwa ndio tuanze kumshauri
..mm najua huyu akichukua maamuzi yake haipiti miezi 6 anakuja kulia humu
 
Kwanini upunguze!? Kama unalo la kushauri sioni sababu ya wewe kusita kufanya hivyo.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] ninakukwaza mkuu? Basi ntapunguza!
 
Habari zenu wanajamvi,

Naomba ushauri kutoka kwenu,

Mimi ni binti wa early twenties na nina mchumba ambae mpaka kwa wazazi anajulikana na Mungu akipenda mwaka huu tutaoana.

Kilichonileta hapa ni hiki kuanzia mwaka Jana nilikua nataka nianze process nirudi shule nilipomshirikisha huyu mchumba kakataa kabisa tena kaenda mbali zaidi na kuniambia siku utakayokwenda shule kata mawasiliano na mimi.

Na mimi nimemwambia mbona inawezekana kwenda chuo na mambo yote yakaendelea kama kawaida lakini bado ameshikilia uzi huohuo wa mimi nisiende chuo.

Naombeni ushauri nisimamie wapi maana najikuta nawaza nashindwa kujua ni choose ni kitu gani.

Nb: Yeye amesoma
Rudi shule kwanza usije kujuta badae
 
Nenda shule, achana naye mara moja huyo mwanaume.

Kuwa na mwenza anayependa ufanikiwe siyo anayependa ubaki chini.
Nikushaur kitu kimoja mapenz hua yanabadilika wakat mwingine, kua mtegemez IPO cku utaijutia ndoa, pia wanaume hua wanabadilika na akibadilika hapo ndipo utakaposema ningejua ningesoma, Nina uhakika ata ukimzalia hawez kukuruhusu uende shule atataka ulee watoto, cha msing nenda kasome waweza funga ndoa mkiwa chuo unazaa afu mnakubaliana malez ya mtoto, pia kila cku mambo ya elimu yanabadilika labda kama una div 1 ya form 6 mana chuo kupata sa iv ngumu na pia mkopo hakuna ila kwa kua utajilipia sawa, ila nadhan anahofu waweza kwenda chuo ukabadilika ukamwacha chakufanya omba chuo, kama anataka kuoa anaweza kukuoa ukiwa chuo kama atak chagua moja, mapenz au chuo mwanaume mwenye kujitambua atakusih usome ili mje saidizana na c kuendekeza wivu usio na future
 
Hebu Tafuta somo la Jana la GJ Malisa. Linahusu "VALUE CLASH" litakusaidia kufanya maamuzi.
Sawa mkuu asante ntalitafta
Nikushaur kitu kimoja mapenz hua yanabadilika wakat mwingine, kua mtegemez IPO cku utaijutia ndoa, pia wanaume hua wanabadilika na akibadilika hapo ndipo utakaposema ningejua ningesoma, Nina uhakika ata ukimzalia hawez kukuruhusu uende shule atataka ulee watoto, cha msing nenda kasome waweza funga ndoa mkiwa chuo unazaa afu mnakubaliana malez ya mtoto, pia kila cku mambo ya elimu yanabadilika labda kama una div 1 ya form 6 mana chuo kupata sa iv ngumu na pia mkopo hakuna ila kwa kua utajilipia sawa, ila nadhan anahofu waweza kwenda chuo ukabadilika ukamwacha chakufanya omba chuo, kama anataka kuoa anaweza kukuoa ukiwa chuo kama atak chagua moja, mapenz au chuo mwanaume mwenye kujitambua atakusih usome ili mje saidizana na c kuendekeza wivu usio na future
Mimi pia nmemwambia tuoane huku nikiwa shule kakataa... Kaniambia nifute hayo mawazo kama nataka kua ña yeye.....
 
Kitucha kwanza kabisa kama wewe no mkristo uliyeokoka na unamjua Mungu hebu mshirikishe Mungu umuulize kama Hugo mwanaume anakufaa au la. Nina uhakika utajibiwa tu. Maana masuala ya kukurupuka kwa akili zako mwenyewevau shinikizo LA wazazi ujue maisha in yako mwenyewe, si ya wazazi wako. Mimi nakushauri nenda kasome shule kwanza. Were bado mdogo utakuja kuolewa tu. Tafuta kwanza elimu.
Sawa ntamshirikisha na mungu pia katika hili.... Asante kwa ushauri
 
Huyo mwanaume atakuwa mwana JF maana mijadala ya kusomesha wachumba humu inaogopesha.
Hahahahaha...
Sidhani kama ni mwana jf ila kuna baadhi ya vitu sijaweka wazi ili ka yeye ni mwana jf asijishtukie sana........
Sio yeye anaenisomesha siwezi kupigia mahesabu fedha zake ikiwa hajanioa
 
Huenda ana wasiwasi ukienda chuo ndo ticket ya kunyang'anywa tonge mdomoni...

Amua moja unataka kuolewa kwanza ama chuo kwanza?
 
Mi nakushauri chagua moja kujiendeleza au kutokujiendeleza. Kwa muda mrefu dhana hii ya kila kitu kuamua mwanaume hata kama bado hajaoa imeshika kasi. Tuchukulie mmoja wapo anapata matatizo hapo mbeleni ya kutokuendelea kuwajibika kiuchumi je, kuacha kwenda kwako shule kutawezesha nini ikitokea kwake?
Mmmhh hapo umenena...... Nashukuru kwa ushauri
 
Sina sababu mpenzi kukukatalia ila ninakuonea wivu yaani sikubali uwe peke yako huko nisije kukupoteza kwa vile sioni mtu mwingine wa kunifaa zaidi yako. Isitoshe hiyo elimu unayoenda kusomea haitokusaidia, nimekwambia utaenda tu baadae. I love you my baby.
Hahahahahaha mmhh umenifanya ni cheke
 
Hahahahaha...
Sidhani kama ni mwana jf ila kuna baadhi ya vitu sijaweka wazi ili ka yeye ni mwana jf asijishtukie sana........
Sio yeye anaenisomesha siwezi kupigia mahesabu fedha zake ikiwa hajanioa
Kasome mrembo. Akikata mawasiliano tuwasiliane..🙂🙂🙂
 
Kwa umri wako ndoa sio kipaumbele sana ila naona shida iko kwa mwenza wako yeye kwa sasa anauhitaji wa ndoa.
Nakushauri soma ili uweze kujitegemea huwezi kujua huko mbele mambo yatakuaje.
Najua hiki ni kipindi kigumu kwa sababu ukichagua moja unaweza kukosa jingine.
Lakini ili ufanikiwe kwenye maisha lazima ufanye maamuzi magumu.
Sawa....... Thank you for the advice
 
Back
Top Bottom