Naomba msaada; Mchumba hataki mimi niende kusoma

Naomba msaada; Mchumba hataki mimi niende kusoma

Kitucha kwanza kabisa kama wewe no mkristo uliyeokoka na unamjua Mungu hebu mshirikishe Mungu umuulize kama Hugo mwanaume anakufaa au la. Nina uhakika utajibiwa tu. Maana masuala ya kukurupuka kwa akili zako mwenyewevau shinikizo LA wazazi ujue maisha in yako mwenyewe, si ya wazazi wako. Mimi nakushauri nenda kasome shule kwanza. Were bado mdogo utakuja kuolewa tu. Tafuta kwanza elimu.
 
Habari zenu wanajamvi naomba ushauri kutoka kwenu.....
Mimi ni binti wa early twenties na nina mchumba ambae mpaka kwa wazazi anajulikana na mungu akipenda mwaka huu tutaoana......

Kilichonileta hapa ni hiki kuanzia mwaka Jana nilikua nataka nianze process nirudi shule nilipomshirikisha huyu mchumba kakataa kabisa tena kaenda mbali zaidi na kuniambia siku utakayokwenda shule kata mawasiliano na mimi.....

Na Mimi nimemwambia mbona inawezekana kwenda chuo na mambo yote yakaendelea kama kawaida lakini bado ameshikilia uzi huohuo wa mimi nisiende chuo.......

Naombeni ushauri nisimamie wapi maana najikuta nawaza nashindwa kujua ni choose ni kitu gani....
Nb: Yeye amesoma

Nenda shule, achana naye mara moja huyo mwanaume.

Kuwa na mwenza anayependa ufanikiwe siyo anayependa ubaki chini.
 
Kitucha kwanza kabisa kama wewe no mkristo uliyeokoka na unamjua Mungu hebu mshirikishe Mungu umuulize kama Hugo mwanaume anakufaa au la. Nina uhakika utajibiwa tu. Maana masuala ya kukurupuka kwa akili zako mwenyewevau shinikizo LA wazazi ujue maisha in yako mwenyewe, si ya wazazi wako. Mimi nakushauri nenda kasome shule kwanza. Were bado mdogo utakuja kuolewa tu. Tafuta kwanza elimu.
Aisee mimi sio mtu wa dini kiviile, sasa Mungu unamuuliza na anakujibu vipi?
 
Mmhhh kwa hiyo unanishauri vipi nikatoe huu ujinga ama
Mi nakushauri chagua moja kujiendeleza au kutokujiendeleza. Kwa muda mrefu dhana hii ya kila kitu kuamua mwanaume hata kama bado hajaoa imeshika kasi. Tuchukulie mmoja wapo anapata matatizo hapo mbeleni ya kutokuendelea kuwajibika kiuchumi je, kuacha kwenda kwako shule kutawezesha nini ikitokea kwake?
 
Mmhhh kwa hiyo unanishauri vipi nikatoe huu ujinga ama
Huyo mwanaume hakupendi angekua anakupenda asingethubutu kukwambia "siku ukienda chuo kata mawasiliano na mimi" why!!
Huyo hapendi maendeleo yako achana nae.
Ila uzito wa huba unaujua wewe.!!
 
Yupo sahihi sana, maana kumpata mwingine ni simple sana tena na madharau juu,
Make sure mnabwagana ndo uende kusoma bila kumpa mwenzio stress, hamchelewagi nyie
 
Hapo ni priorities tu zimetofautiana inabidi make chini mkubaliane kitu gani kianze kati ya elimu au ndoa. Mimi binafsi ningekushauri ndoa na uzae mtoto ndio uende chuo kama alivyo suggest mchumba wako. Chuoni kuna ujinga mwingi sana aisee na kudanganyana kwingi na utoto hata kwa watu wazima hasa wake za watu wanaharibu sana sijui kwa nn. Msikilize mmeo mtarajiwa amefocus mbali sana na anakupenda ndio maana anataka kulinda mali zake. Muoane mfurahie ndoa mtasoma baadae wakati ukiruhusu.
 
Fanya maamuzi yako, kama unaenda nenda kwa faida yako, kama utamsikiliza huyo jamaa shauri yako... Lakini ukae ukijua Chuo siyo mahala salama hata siku moja kwenye upande wa mahusiano...
 
Sina sababu mpenzi kukukatalia ila ninakuonea wivu yaani sikubali uwe peke yako huko nisije kukupoteza kwa vile sioni mtu mwingine wa kunifaa zaidi yako. Isitoshe hiyo elimu unayoenda kusomea haitokusaidia, nimekwambia utaenda tu baadae. I love you my baby.
 
Hana sababu ya msingi maana anasema hayo hayakua makubaliano yetu Mara aseme nisubiri tuoane nizae angalau mtoto mmoja ndo nirudi shule lakini kwa upande wangu naona ukishazaa majukumu yanaongezeka na ndio maana nko njia panda
Naona jamaa wako kama mkoloni hivi..Vipi mahusiano yenu yapo fresh?
 
Hana nia njema nawe huyo!!! Tena wa kumtupilia mbali. Mwanaume gani hataki maendeleo ya mwenza wake? Kama unatamani kuendelea kusoma bora ufanye hivyo saivi, kwenye ndoa itakua ngumu kidogo.
Wanaume wengine wanataka wakikuoa waku-control hadi unapotaka kununua peni. Wanaogopa ukiwa msomi utakua na akili yako na kuweza kujitegemea.
Wadada wengi ata hivyo tunakumbwa na tamaa tukiwa chuoni, anaweza akawa anaogopa mwanamke wake kuibwa.
Jaribu kuongea nae ujue sababu ya yeye kutotaka wewe usome. Utajua anakataa kwa mema au mabaya.
Kusoma kwa mwanamke sio maendeleo ya mme bank ni maendeleo binafsi...
 
Kwa umri wako ndoa sio kipaumbele sana ila naona shida iko kwa mwenza wako yeye kwa sasa anauhitaji wa ndoa.
Nakushauri soma ili uweze kujitegemea huwezi kujua huko mbele mambo yatakuaje.
Najua hiki ni kipindi kigumu kwa sababu ukichagua moja unaweza kukosa jingine.
Lakini ili ufanikiwe kwenye maisha lazima ufanye maamuzi magumu.
 
Mtaka vyote kwa pupa hukosa vyote kwa pupa....unaeza soma afu ukakosa ajira ukajuta why umepoteza muda mwingi afu unakuta jamaaa maisha yameitkia na tayar ana mke...wew sema na hisia zako humu kila mtu ata kushaur anavojiskia...Pesa ndo kila kitu elimu mbwembwe tu
 
Hana sababu ya msingi maana anasema hayo hayakua makubaliano yetu Mara aseme nisubiri tuoane nizae angalau mtoto mmoja ndo nirudi shule lakini kwa upande wangu naona ukishazaa majukumu yanaongezeka na ndio maana nko njia panda

Inawezekana anayo logic, nionavyo hana nia ya wewe kutokusoma, shida ana wasiwasi atakukosa mbeleni. Nionavyo kama ni destiny husband funga ndoa naye, then utaenda shule. Vyuo vikuu havina shida waweza soma mjamzito na ukalea na mtoto na mambo yote yakaenda sawa. Wengi wamefanya hivyo na mambo yote yanaenda vizuri tu
 
Hana nia njema nawe huyo!!! Tena wa kumtupilia mbali. Mwanaume gani hataki maendeleo ya mwenza wake? Kama unatamani kuendelea kusoma bora ufanye hivyo saivi, kwenye ndoa itakua ngumu kidogo.
Wanaume wengine wanataka wakikuoa waku-control hadi unapotaka kununua peni. Wanaogopa ukiwa msomi utakua na akili yako na kuweza kujitegemea.
Wadada wengi ata hivyo tunakumbwa na tamaa tukiwa chuoni, anaweza akawa anaogopa mwanamke wake kuibwa.
Jaribu kuongea nae ujue sababu ya yeye kutotaka wewe usome. Utajua anakataa kwa mema au mabaya.
Sio kwamba hapendi maendeleo mtu anataka kuanzisha familia halafu m/mke anataka kwenda shule huoni hapo unachelesha malengo ya mwenzake ya kuanzisha familia. M/ume ana malengo tofauti na huyu dada cha maana hapo ni kukaa chini na kujadiliana na kufikia muafaka. Usimwambie mwenzake kuwa m/ume wake hampendi au hapendi maendeleo yake si sahihi. Upendo wao wanaujua wenyewe ndio maana wamekubaliana waoane.

Ili jambo sio jepesi kama unavyowaza lina maana kubwa sana halafu nashangaa watu awakusomeshwa na wazazi wao huko nyuma unataka kumuoa anaona una hela ndio anaanzisha masuala ya kusoma aliyoyakosa kwa wazazi wake huko.

Olewa kwanza timiza wajibu wa ndoa ndio ujiendeleze baadae. Halafu sijui nani aliyeturoga kuwa elimu ya darasani ndio kila kitu. Mtu anaweza kusomea ujasiriamali wa kitu flani na aka concentrate na hicho hicho kikamtoa. Mambo ya kuanzia diploma akimaliza ataanza degree kisha masters mwanaume unasubiri tu
 
Kwa umri wako na elimu yako, better ukaenda shule kwanza. Kama ni ngumu kwake kukuruhusu uende shule sasa hivi; ni ngumu zaidi yeye kukuruhusu uende shule once you are married +watoto. Maisha hayarevolve around ndoa only, kuna Maisha nje ya ndoa. Sijui kama ndoa inaua ndoto za wanawake wengi, but ukishaolewa ni kazi zaidi kutimiza ndoto zako binafsi. Omba hata wazee wako waongee naye, maybe itasaidia kukuelewa. Kila la kheri
 
Back
Top Bottom