Naomba msaada; Mchumba hataki mimi niende kusoma

Naomba msaada; Mchumba hataki mimi niende kusoma

Habari zenu wanajamvi,

Naomba ushauri kutoka kwenu,

Mimi ni binti wa early twenties na nina mchumba ambae mpaka kwa wazazi anajulikana na Mungu akipenda mwaka huu tutaoana.

Kilichonileta hapa ni hiki kuanzia mwaka Jana nilikua nataka nianze process nirudi shule nilipomshirikisha huyu mchumba kakataa kabisa tena kaenda mbali zaidi na kuniambia siku utakayokwenda shule kata mawasiliano na mimi.

Na mimi nimemwambia mbona inawezekana kwenda chuo na mambo yote yakaendelea kama kawaida lakini bado ameshikilia uzi huohuo wa mimi nisiende chuo.

Naombeni ushauri nisimamie wapi maana najikuta nawaza nashindwa kujua ni choose ni kitu gani.

Nb: Yeye amesoma

Kimbia mapema. Huyo siyo mchumba kwa taarifa yako anakuandaa kuja kuwa mfungwa wake maana elimu ndo itakufungulia dunia usimtegemee.

Narudia tena. Kimbia
 
Nani asiyejua maisha ya chuo yalivyo, anajua ukienda tu basi unaenda kutumika kama eraser
 
Unaenda kusoma nje?
Kama ni nje naungana na shemela kama ni hapa hapa mwambie shemela aache hizo
 
We kasome...utashangaa unakataa kwenda shule na kukuoa hakuoi...utakosa vyote....
Hajatoa posa hajatoa mahari ht km anajulikana hana haki ya kukupangia future yako..kasome..u r still young watu wanaolewa wakiwa vyuoni na wanazaa na kutunza familia vile vile..hakutakii mema huyo.....shule ndio mkombozi wako
 
Elimu haitakusaliti haitakupa talaka
Ila mwanaume....don't love too hard​
 
Back
Top Bottom