Perry
JF-Expert Member
- Feb 24, 2011
- 10,082
- 2,354
Mambo wakuu?
Nina dada yangu mkubwa ana umri kama 38yrs hivi,sasa huyu dada alikua anaishi na mwanaume wake ila hawakua wamefunga ndoa,wameishi kama miaka 8 kama sikosei.wamebahatika kupata watoto watatu mpaka sasa, mumewe ni muajiriwa kwenye shirika flani kubwa tu hapa nchini,dada yangu yeye hana kazi yoyote ni mtu wa kubangaiza tu na kuuza nguo online kwa kifupi ni mama wa nyumbani tu.
Week mbili zilizopita waligombana na huyo mumewe, dada kwa maelezo yake anasema huyo mumewe alimfukuza nyumbani kwake usiku ule pamoja na watoto wake,ila kwa uchunguzi nilioufanya mumewe hakumfukuza ila ni yeye tu aliamua kukimbilia kwa ndugu yetu mwingine na watoto wake usiku ule.
Kilichonifanya nije kuomba ushauri humu ni hiki,kuna ndugu naona kama wamemshauri dada vibaya sana,kuna nyumba yetu ya urithi tuliachiwa na marehemu wazazi wetu,ndugu wamemshauri dada aondoke mazima kwa mumewe arudi pale nyumbani kwenye nyumba ya urithi akae,kweli dada nae akachukua huo ushauri wa ndugu kaenda kwa mumewe kabeba vitu karudi nyumbani na mzigo wa watoto watatu,yule mumewe kule mpaka leo hajampigia simu yeyote nyumbani kumueleza nini tatizo yuko kimya tu,dada yeye anasema amechoka manyanyaso,sasa nimeshindwa kumuelewa dada kama nilivyosema hana kazi yoyote ni anauza tu vinguo online,ana watoto watatu wawili kati yao wanasoma shule za English medium.huko napo nasikia bwana alimuambia kama ameamua kuondoka nyumbani na watoto wake basi asikae amtafute kwa lolote lile na hao watoto amempa yeye kama zawadi.
Dada hakua na maisha yoyote magumu kwa mume wake kwani shemeji alikua anajitahidi sana kujali familia yake.
Wasiwasi wangu ni kwamba,huenda dada akaanza kuishi maisha ya shida kwa kujitakia mwenyewe na akawa msalaba kwetu sisi,kwanza kitendo cha ndugu hawa kumshauri arudi nyumbani pasipokuangalia mustakabali wake na watoto wake naona ni janga,hapa ni week ya pili tu lkn ameshaanza usumbufu wa vizinga.nawaza ada za hao watoto wa English medium atatoa wapi?
Wakuu huenda mwandiko wangu ni mmbaya but tuvumiliane.
Naomba mnishauri nifanyeje huyu mtu arudi kwa mumewe huko kwani kama nilivyoeleza soon anaenda kuwa msalaba kwetu huyu au kama kuna ushauri mwingine naukaribisha.
Nina dada yangu mkubwa ana umri kama 38yrs hivi,sasa huyu dada alikua anaishi na mwanaume wake ila hawakua wamefunga ndoa,wameishi kama miaka 8 kama sikosei.wamebahatika kupata watoto watatu mpaka sasa, mumewe ni muajiriwa kwenye shirika flani kubwa tu hapa nchini,dada yangu yeye hana kazi yoyote ni mtu wa kubangaiza tu na kuuza nguo online kwa kifupi ni mama wa nyumbani tu.
Week mbili zilizopita waligombana na huyo mumewe, dada kwa maelezo yake anasema huyo mumewe alimfukuza nyumbani kwake usiku ule pamoja na watoto wake,ila kwa uchunguzi nilioufanya mumewe hakumfukuza ila ni yeye tu aliamua kukimbilia kwa ndugu yetu mwingine na watoto wake usiku ule.
Kilichonifanya nije kuomba ushauri humu ni hiki,kuna ndugu naona kama wamemshauri dada vibaya sana,kuna nyumba yetu ya urithi tuliachiwa na marehemu wazazi wetu,ndugu wamemshauri dada aondoke mazima kwa mumewe arudi pale nyumbani kwenye nyumba ya urithi akae,kweli dada nae akachukua huo ushauri wa ndugu kaenda kwa mumewe kabeba vitu karudi nyumbani na mzigo wa watoto watatu,yule mumewe kule mpaka leo hajampigia simu yeyote nyumbani kumueleza nini tatizo yuko kimya tu,dada yeye anasema amechoka manyanyaso,sasa nimeshindwa kumuelewa dada kama nilivyosema hana kazi yoyote ni anauza tu vinguo online,ana watoto watatu wawili kati yao wanasoma shule za English medium.huko napo nasikia bwana alimuambia kama ameamua kuondoka nyumbani na watoto wake basi asikae amtafute kwa lolote lile na hao watoto amempa yeye kama zawadi.
Dada hakua na maisha yoyote magumu kwa mume wake kwani shemeji alikua anajitahidi sana kujali familia yake.
Wasiwasi wangu ni kwamba,huenda dada akaanza kuishi maisha ya shida kwa kujitakia mwenyewe na akawa msalaba kwetu sisi,kwanza kitendo cha ndugu hawa kumshauri arudi nyumbani pasipokuangalia mustakabali wake na watoto wake naona ni janga,hapa ni week ya pili tu lkn ameshaanza usumbufu wa vizinga.nawaza ada za hao watoto wa English medium atatoa wapi?
Wakuu huenda mwandiko wangu ni mmbaya but tuvumiliane.
Naomba mnishauri nifanyeje huyu mtu arudi kwa mumewe huko kwani kama nilivyoeleza soon anaenda kuwa msalaba kwetu huyu au kama kuna ushauri mwingine naukaribisha.