Naomba kujua lengo la kuanzishwa inspirations talks, motivations etc

Habari wana Jf!


Naombwa kujuzwa nini kilikuwa lengo hasa ya kuanzisha inspirations na motivations speech, hadi kuelekea watu kuanza kuandika vitabu?

Je tofauti na faida ya kumjenga kiimani ni faida gani kiuchumi mtu hupata( excludes wanaoandaa event)?

Ni kweli ukisikiliza motivations kila wakati utakuja kuwa millionaire?

Kuna uhusiano gani wa mtu kufanikiwa na hizi inspiration?

Je kusoma vitabu vingi ndio rahisi ufunguo wa mafanikio?

Ukisikia mtu anaongelea hizi events za motivations unazitafsiri vipi katika jamii ya sasa? mfano Dar kuna game changer na ile ya Joel Nanauka inaitwa mentalship program.

Je zimebadili uchumi wako kiasi gani?


Na kama zinainfluince katika jamii kwanini baadhi ya maeneo hazifiki?


How to get started? Ans: Start where you are with what you have.

inspiration/motivation speech ni wauza mbinu za mafanikio kupitia makongamano, kupitia hiyo makongamano ambayo lazima utoe pesa wao ndio hupatia pesa humo humo plus wadhamini, kwa nchi yetu sijaona mtu anaeongea hayo mambo kafanikiwa tukamwita billionea,

kingine naona mtu akishika million kadhaa na yy anakuwa muhamasishaji wa mafanikio eg: Idris, millard, jokate, etc ila tukumbuke kila mtu anafamilia aliyotoka na support zinatofautiana, wakati mwenzio anakwambia alianza kazi ya posho 30 huku nauli akipewa na mama yake, wewe hujui hata nauli ya kwenda kila siku sehemu ambayo wanataka ujitolee hujui utaipata wapi
 
Ni mpuuzi pekee ambaye hajui umuhimu wa vitabu ndio anaweza kujitokeza hadharani na kusema usomaji vitabu hauna umuhimu wowote kwa binadamu

Laiti hayo mnayosema yangekuwa sahihi binadamu tusingekuwa na maisha tuliyonayo sa iv kwani sehemu kubwa yanayogunduliwa sa iv muongozo wake upo kwenye maandishi kutoka kwa mababu wa kale

Umuhimu wa vitabu ni latika kupngeza maarifa yaan unaweza kuwa unafanya biashara bila ya kuwa na maarifa uka struggle sana lkn siku ukisoma kitabu chenye maarifa ya namna bora ya kuendesha biashara then tegemea mabadiliko makubwa kwenye biashara yako

Khs motivation speaker yes zina umuhimu wake hasa kwa wale wenye self doubt, hswa jamaa kazi yao ni kukupa courage kuwa inawezekana haina haja ya kuogopa so huwezi kuwakebehi watu km hawa wana umuhimu wao kwenye jamii, na hta jeshini watu wa motivation wapo, mwanajeshi kabla hajaingia kwenye ulingo wa vita lazima atakuwa na uoga flani sasa kazi ya kamanda wa notivation speaker ni kumpa speech ili kumjaza ujasiri hyu mwanajeshi ili kumuondolea hofu aliyokuwa nayo na kupambana , kwa hyp hawa jamaa wana umuhimu sio vizuri kuwakebehi



Wengi wao hawa ni wachumia tumbo tu hawana lolote, at best niwaite wajasiriamali kama wajasiriamali wengine wowote! Ikitaka akuongoze kwenye specific idea wanaingia mitini! Wamehamasisha kilimo cha matikiti maji na kufuga sungura mwisho wa siku hakuna masoko watu wamefilisiwa kwa mikopo!
Njia yakuelekea mafanikio sio mpaka kupigwa darasa, nops! Bali:
1: isikilize nafsi na dhamira yako
2: ifuatilie ndoto yako
3: usikubali kukata au kukatishwa tamaa
4: Trust in God, na kwa karama alizokujalia utafanikiwa hatimaye
 
inspiration/motivation speech ni wauza mbinu za mafanikio kupitia makongamano, kupitia hiyo makongamano ambayo lazima utoe pesa wao ndio hupatia pesa humo humo plus wadhamini, kwa nchi yetu sijaona mtu anaeongea hayo mambo kafanikiwa tukamwita billionea,

kingine naona mtu akishika million kadhaa na yy anakuwa muhamasishaji wa mafanikio eg: Idris, millard, jokate, etc ila tukumbuke kila mtu anafamilia aliyotoka na support zinatofautiana, wakati mwenzio anakwambia alianza kazi ya posho 30 huku nauli akipewa na mama yake, wewe hujui hata nauli ya kwenda kila siku sehemu ambayo wanataka ujitolee hujui utaipata wapi
True bro ni sawa mtu aje akufundishe jinsi ya kuanza bila vitendo
 
Wengi wao hawa ni wachumia tumbo tu hawana lolote, at best niwaite wajasiriamali kama wajasiriamali wengine wowote! Ikitaka akuongoze kwenye specific idea wanaingia mitini! Wamehamasisha kilimo cha matikiti maji na kufuga sungura mwisho wa siku hakuna masoko watu wamefilisiwa kwa mikopo!
Njia yakuelekea mafanikio sio mpaka kupigwa darasa, nops! Bali:
1: isikilize nafsi na dhamira yako
2: ifuatilie ndoto yako
3: usikubali kukata au kukatishwa tamaa
4: Trust in God, na kwa karama alizokujalia utafanikiwa hatimaye
Well done must be great than well said... Copy that
 
Ukitembea na walioshindwa 9 basi ujue namba 10 utakuwa ww. Acha wenzako tushibe maarifa ya akina less brown, paul sineck, Dr myles Monroe, dale carnigie, Robert kiyosaki, the late Jim rohn, zig zigral, denzel Washington, Arnold Shwarzinegal, depak Chopra, Ali daniel, Eric Thomas, Anthony Robbins, Stephen covey na wadau wengine endeleeni kuweka vichwa vingine. Tusaidie hichi cha wasio na imani. Mafanikio ni Imani kama ww huamini katika vitabu na motivational huwezi kuona impact yeyote. Kumbuka Bible is the most inspirational and Motivational book ever written in the history of mankind's.
Kama bible ni inspiration book nzuri kwanini huwa haifuatwi na wanao amini? Nadhani kuna shida mahali na hizi elimu ngeni...
 
Back
Top Bottom