2021 tumefika wapi kwenye lengo la kutengeneza mabilionea 1,000 ambao Rais anataka wapatikane?

Freddie Matuja

JF-Expert Member
Jul 21, 2018
1,465
2,857
2021 ndio tushaingia na 2025 haiko mbali sana ambapo Mkulu wa sasa atakuwa anakabidhi kijiti kwa ajae. Je tutakuwa tumefika na lengo la Mkulu la kujenga uchumi wa kati kwa kutumia viwanda na kutengeneza mabilionea 1000 kama alivyojitainisha 2019.

Wakati mmoja mwaka 2016 Mhe, Rais alitamka akiongea na waandishi wa habari IKULU, alitoa wito na kuwataka waandishi wa habari nao wanataka kujenga viwanda, wafungue kampuni then wampe Msigwa (ambae ni mkurugenzi wa mawasiliano IKULU) ili amfikishie na wapate mkopo kwa ajili ya kuendesha kampuni.

Najaribu kuwaza kwa sauti, je waandishi wa habari waliitikia wito? Baada ya kumfikishia Msigwa taarifa za kampuni waliyofungua pengine na business plan yenye kufikia soko lenye uhitaji fulani, je, walipata mkopo; walilenga sekta gani hasa ambayo waliona uhitaji mkubwa? Au hawakufikisha kabisa, nini kiliwakwamisha;
Kama sio muandishi wa habari na huna access na Msigwa, bado kuna dirisha la kumfikishia Rais yeye kama yeye; maana alisema njooni kwangu.

Kwa mfumo wa uzalishaji wa biashara yoyote rasmi lazima kusajili kampuni BRELA, kupata Cheti cha mlipa kodi TIN toka TRA, Tax Clerance Certifiate, leseni ya biashara na ofisi ambapo biashara itaanza. Nadhani kwa hatua hii Watanzania wengi wanaweza kumudu.

Hatua ya pili ni kutambua uhitaji wa soko (na hiyo inakuwa fursa) ya kwanini business plan iwepo kwa kutumia fedha za mtaji (CAPEX) pia fedha za kuendeshea biashara/uwekezaji (OPEX).

Tanzania kuna changamoto kwa benki nyingi (Commercial Banks) kutohangaika na start-up ikiwamo kutoa mikopo ya uwekezaji, ila mtu akiweza kuwekeza anavyojua yeye, then wao wanamfuata kumshawishi akope kwao apate hela ya kuendeshea biashara (OPEX).

Katika uchumi mkubwa na uchumi wa kati, uhitaji wa soko unaweza kumpa mteja/mwekezaji dhamani ya mkopo ili akizalisha na kuuza kwa soko ambalo liko wazi, anarejesha mkopo.

Tanzania tuna fursa nyingi sana za kuwekeza kukidhi mahitaji ya ndani ya soko;
Kila mwaka wizara ya afya inanunua dawa za bil zaidi ya 900 toka nje ya Tanzania; kwa tafsiri rahisi ukijumuisha na private hospital mahitaji/soko la ndani kwa madawa na vifaa tiba ni zaidi ya TRIL 1;

Kila mwaka tunanunua mafuta ya kula kwa mahitaji ya ndani zaidi ya tani 320
Kila mwaka tunanunua toilet paper
Kila mwaka tunanunua toothpick
kila mwaka tunanunua mashuka ya hospitali
Kila tuna-import mbegu za nyanya, cabbage, mahindi,
Kila mwaka tuna-import maziwa ya ng;ombe (maziwa ya unga na kimiminika)
Kila mwaka tuna-import chupi za watoto yet pamba inalimwa Tanzania
Kila mwaka tuna import leso
Kila mwaka tuna import chupi za kike na sidiria
kila mwaka tuna import chupi za kiume na yet pamba inalimwa Tanzania

Unaweza kuongeza na mengine

Wizara ya fedha ni namna gani ina focus nini tufanye ili kuongeza uzalishaji (kwa kushirikiana na wizara zingine za kisekta) ili kukuza mzunguko wa fedha ambao in-turn utaongeza tax base;
Sio sawa hata kwa watalii wanatoka Ulaya na Marekani wakija bongo kutalii bado wanakula cornflakes (imported), kahawa wanayokunywa (imported); cocoa (imported);

Kuna faida gani kila mwaka tunatenga zaidi ya bilioni 500 kugharamia elimu na baada ya hapo hatuna uhakika hiyo fedha itarejeshwa vip na wahitimu wa vyuo vikuu ambao walipata mikopo.

Hata kwa darasa la kwanza mpaka kidato cha nne, lazima tuone return on investment kwa namna moja au nyingine.

Sina imani na kejeli za misemo kama "mitano tena" au #tutaelewana tu kama zita-solve matatizo yetu.

Ila tukiamua kusililizana kuna mahali tutafika.

Mwekezaji pale chuo kikuu cha Dar es Salaam (Mlimani City) hakuwa na fedha mkononi in term of billions; alikuwa na investment strategy ambayo alihitaji serikali impatie legal agreement ya kumkodishia eneo la uwekezaji kwa miaka kadhaa na atawalipaje; makubaliano yale (yalimfanya akawekeza); inawezekana baadhi wakasema, jamaa alitupiga sana. Ila tukfanya equation kama asingekuja na kabla ya yeye kuja, thamani ya fedha na mzunguko wa fedha mwenge na ubungo ulikuwaje; ukipima uwekezaji ule positively umeingiza bei gani kwa wananchi, tax base imepanuka kiasi gani na ripple effect kwa maeneo jirani na Dar as a whole; nadhani wengi tutakubaliana, tunapata si haba ukilinganisha na wakati hayupo; kama kuna mahali tunapigwa tuna nafasi ya kukaa nae chini kwa kuangalia yeye anapata nini, deni alilokopa kujenga ana-service vip na faida anayopata tokana na fedha anayochuma Tanzania.

Tukichukua uwekezaji wa mlimani city kama moja ya investment model, kumbe hazina, wizara ya ardhi, ofisi ya mwanasheria mkuu na TIC vingeweza kuwapa watu wengine just papers (legal docx) ili kutokea hapo tujenge uchumi jumuishi ambao unatoa tumaini kwa vijana wanaosoma wajue bado kuna mwangaza wa kuweza kuajiriwa private sector.

Kumbukumbu za wakoloni wetu zinasema "1893 visionary German agronomist Dr. Richard Hindorf introduced sisal into Germany East Africa ambayo ni Tanganyika.

Huyu mzungu aliiba miche ya mbegu 1000 za katani toka Mexico; mpaka anafika Tanganyika alikuwa na miche kama 90 iiyokuwa hai; ila matokeo yake ni Tanganyika kuwa miongoni mwa wazlishaji wakubwa wa katani na viwanda vingi vya kuchakata final products vikiwa Ujeruani na baadae UK.

Ili tufike, lazima tuwe na overt operations na covert operations kwenye uwekezaji. Serikali lazima iwe upande wa mbinu ambazo hazina lengo kuhujumu wengine duniani, ila kuona namna gani tunatumia competitive advantage kujijenga, kupunguza imports na kuongeza exports ili kuongeza fedha za kigeni nchini.

Nimalizie kwa kusema nakubaliana na kujenga viwanda, ila sio sawa kuruhusu wachina kuja na viwanda vya toilet paper, viwanda vya mifuko ya kufungashia. Hii sio sawa. Huwezi kwenda China ukaweka kiwanda cha toilet paper au India wakakubali; kuna vitu ambavyo wanajua sio rocket science kama kuna serious investor kuna maeneo ambayo kweli aruhusiwe na kuwe na uwezeshaji kama aliofanyiwa wa mlimani city ili neema ya cashflow iwe kwa wingi Tanzania.

Heri ya mwaka mpya 2021.

F
 
Utajichosha kwa kuandika maneno magumuuuuuu.

Ni sawa na kumwelekeza chizi jinsi rocket inavyofanya kazi.

Serikali ianze kwanza kwa vitendo kuonesha kuwa inaheshimu sekta binafsi kabla ya kutaka wawekezaji wapya.

Account number za makampuni kila siku zinafungiwa na TRA,

Wafanyabiashara waliopo utafikiri wako vitani na TRA, then hizi nyingine ni porojo tu
 
Utajichosha kwa kuandika maneno magumuuuuuu.

Ni sawa na kumwelekeza chizi jinsi rocket inavyofanya kazi.

Serikali ianze kwanza kwa vitendo kuonesha kuwa inaheshimu sekta binafsi kabla ya kutaka wawekezaji wapya.

Account number za makampuni kila siku zinafungiwa na TRA,

Wafanyabiashara waliopo utafikiri wako vitani na TRA, then hizi nyingine ni porojo tu
Mkuu, hata mimi nina mambo kadhaa kuhusu kampuni yangu na TRA kwani kodi ya 30% kwenye mauzo ghafi sio rafiki kiuhalisia.

Muuza sembe ya kufungashwa anakadiriwa 30% ya mauzo ghafi wakati anauza dhahabu serikali inakata 7%; hii si sawa kwa muuza sembe.

Hilo nalo iko haja ya kuendelesha kujadili na kushauri nini kifanyike ili mfanya biashara apate na kodi zilipwe kwa lengo la serikali kutoa huduma kwa wananchi wake na Tanzania tunayoitaka itokee.

Hoja yangu ni kuhimiza uzashaji wa ndani ambao kama tukifanya soko lake lipo. Ili kama leo nikiomba hata dhamana ya serikali kukopa nizalisha pamba za hosipitali na bandage na gauze kwa kutumia pamba inayolimwa, soko likuwa MSD; je serikali kupitia wizara ya fedha, wizara ya afyam wizara ya uwekezaji, ofisi ya AG, wizara ya ardhi, wana utayari wa kutoa legal docx ili kuoitia hiyo sisi Watanzania tukope ndani au nje ili uwekezaji wetu pengine utakidhi haja ya kuongeza ajira ambazo waajiriwa pia watakuwa sehemu kuongeza tax base kwa PAYE na corporate tax?

Wengine watasema, ahh yani tukupe gov guarantee wewe una nini? Mimi nina opportunity hii ambayo kama kuna huo uwezeshaji, sio tu kampuni hii ya Mtanzania itapata ila hiyo neema itakuja nchini badala ya kuendelea kwenda India au China.

Nadhani kwa namna hii kuna pahala tutafika kama tunalenga kujenga uchumi jumuishi.
 
Mkuu, hata mimi nina mambo kadhaa kuhusu kampuni yangu na TRA kwani kodi ya 30% kwenye mauzo ghafi sio rafiki kiuhalisia.

Muuza sembe ya kufungashwa anakadiriwa 30% ya mauzo ghafi wakati anauza dhahabu serikali inakata 7%; hii si sawa kwa muuza sembe.

Hilo nalo iko haja ya kuendelesha kujadili na kushauri nini kifanyike ili mfanya biashara apate na kodi zilipwe kwa lengo la serikali kutoa huduma kwa wananchi wake na Tanzania tunayoitaka itokee.

Hoja yangu ni kuhimiza uzashaji wa ndani ambao kama tukifanya soko lake lipo. Ili kama leo nikiomba hata dhamana ya serikali kukopa nizalisha pamba za hosipitali na bandage na gauze kwa kutumia pamba inayolimwa, soko likuwa MSD; je serikali kupitia wizara ya fedha, wizara ya afyam wizara ya uwekezaji, ofisi ya AG, wizara ya ardhi, wana utayari wa kutoa legal docx ili kuoitia hiyo sisi Watanzania tukope ndani au nje ili uwekezaji wetu pengine utakidhi haja ya kuongeza ajira ambazo waajiriwa pia watakuwa sehemu kuongeza tax base kwa PAYE na corporate tax?

Wengine watasema, ahh yani tukupe gov guarantee wewe una nini? Mimi nina opportunity hii ambayo kama kuna huo uwezeshaji, sio tu kampuni hii ya Mtanzania itapata ila hiyo neema itakuja nchini badala ya kuendelea kwenda India au China.

Nadhani kwa namna hii kuna pahala tutafika kama tunalenga kujenga uchumi jumuishi.
Dunia haijawahi kuwa na upungufu wa mitaji wala opportunities.

Issue kubwa ni SERA, USALAMA WA MITAJI na MAZINGIRA WEZESHI.

Hivi imagine, mwekezaji akiingia mgogoro na serikali ni wapi anakimbilia kuitafuta haki yake ??

Binafsi nafikiri, mjadala mkubwa unatakiwa kuanzia kwenye chanzo.

Huwezi kupanga kuongeza idadi ya watoto wakati watoto ulionao tu wanakula JALALANI na ka siku unapambana NAO.

Na kuhusu kuongeza pato la taifa letu nadhani siyo kipaumbele pia, ndio maana tulikuwa tuna mazao ya ayoingiza pesa nyingi tu za kigeni, tumetumia nguvu kubwa, tumeyaua: Mbaazi, Korosho, Kahawa, Katani
 
Bado tuna tatizo kubwa katika mifumo yetu ya kuingiza pesa na uwekezaji. Pamoja na hayo tunatakiwa tutambue role za

1) Investments BROKER.
2) Investments Consultants.
3) investments Advisors

Hawa wataalamu ni muhimu sana kuweza kupromote projecrs na vile vile kushawishi Foreign Direct Investment na tuhakikishe tunarasimisha.

Wawekezaji wengi mno hawaifahamu Tanzania na opportunities zilizopo Tanzania katika sector mbali mbali na faida wa nayo weza kupata ikiwa watawekeza.

Hali hiyo ni lazima wapatikane watu waiuze Tanzania nchi za nje kwa wenye uwezo wa wakuwekeza hasa viwanda au huduma ambao kwao wanakotoka wana masoko.

Na kwa kuruhusu hali hiyo, tutatimiza moja ya matakwa muhimu ya kuweza kutayarisha mazingira wezeshi ya kujenga Export oriented Economy.
 
Dunia haijawahi kuwa na upungufu wa mitaji wala opportunities.

Issue kubwa ni SERA, USALAMA WA MITAJI na MAZINGIRA WEZESHI.

Hivi imagine, mwekezaji akiingia mgogoro na serikali ni wapi anakimbilia kuitafuta haki yake ??

Binafsi nafikiri, mjadala mkubwa unatakiwa kuanzia kwenye chanzo.

Huwezi kupanga kuongeza idadi ya watoto wakati watoto ulionao tu wanakula JALALANI na ka siku unapambana NAO.

Na kuhusu kuongeza pato la taifa letu nadhani siyo kipaumbele pia, ndio maana tulikuwa tuna mazao ya ayoingiza pesa nyingi tu za kigeni, tumetumia nguvu kubwa, tumeyaua: Mbaazi, Korosho, Kahawa, Katani
inawezekana baadhi ya vitu visiwe vipaumbele hasa kwa maafisa ambao kila tarehe 23 account zao zinasoma.

Ila kujenga uchumi jumuishi na endelevu ni takwa la kizalendo kwa ajili ya kizazi chetu na kijacho.

Heidelberg Group ni kampuni toka Sweden ipo Tanzania toka 1966 kama shareholder wa Twiga kabla ya azimio la Arusha.
Lafarge S.A. ni shareholder wa Mbeya Cement,

Cocacola, Serengeti Breweries, TBL, Barrick Gold wote hawa ni wakubwa; pamoja na changamoto ile wasomi wanasema "unpredictable policies" hawa jamaa hawajakimbia;

Dangote kuna lots of issue ambazo huenda hakuwa ka-sort out hasa kwenye kupatikana kwa mkaa wa mawe wa kutosha.

Changamoto hizi haziwezi kutufanya kukata tamaa na kuona Tz sio sehemu ya kuwekeza, maana kuna maeneo ambayo ukiweza kuwekeza vema utauza tu based on available market

Imagine sukari kila mwaka tuna import, mbolea ya viwandani zaidi ya tani laki 6; viwatilifu vya kuua wadudu yet tuna gradutes wa kutosha wa kemia.

Na kama kuna shida, popote bora kuisemea hapa au popote kwa uwazi na kuja na possible solution ili likifanyiwa kazi sisi tufaidike.

Kama Congo ambako "zinapigwa risasi" kuna viwanda vya mafuta ya kula, viwanda vya sembe; hapa kwetu kwanini tusikomae na kushauriana na wenye mamlaka ili tuje na common goal ya sisi kupata na wao wapate??
 
Bado tuna tatizo kubwa katika mifumo yetu ya kuingiza pesa na uwekezaji. Pamoja na hayo tunatakiwa tutambue role za

1) Investments BROKER.
2) Investments Consultants.
3) investments Advisors

Hawa wataalamu ni muhimu sana kuweza kupromote projecrs na vile vile kushawishi Foreign Direct Investment na tuhakikishe tunarasimisha.

Wawekezaji wengi mno hawaifahamu Tanzania na opportunities zilizopo Tanzania katika sector mbali mbali na faida wa nayo weza kupata ikiwa watawekeza.

Hali hiyo ni lazima wapatikane watu waiuze Tanzania nchi za nje kwa wenye uwezo wa wakuwekeza hasa viwanda au huduma ambao kwao wanakotoka wana masoko.

Na kwa kuruhusu hali hiyo, tutatimiza moja ya matakwa muhimu ya kuweza kutayarisha mazingira wezeshi ya kujenga Export oriented Economy.
Uliyoyaongea ni muhimu lakini hayawezi kusaidia chochote kwa Tanzania.

Mimi nashughulika na taarifa za uwekezaji mkubwa Duniani. Na ninashiriki kwenye kuchakata taarifa za kuyapanga mataifa katika ubora wa mazingira ya uwekezaji.

Tanzania kwa kuangalia vigezo tunavyotumia kuyapanga mataifa katika mazingira bora ya uwekezaji, ipo chini sana.

Tanzania ina mazingira mabaya sana kwenye uwekezaji. Hakuna hata mwekezaji mmoja mkubwa anayeweza kuja kuwekeza Tanzania kwa sasa. Mwekezaji mkubwa wa mwisho kuja Tanzania alikuwa Dangote. Toka hapo hakuna hata mmoja aliyewekeza Tanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera sana kwa Uzi ulioshiba. ..hivi ndo vitu inabidi viwe vinaletwa humu sio habari za kujadili matukio. Kwa nchi zetu( waafrika) tuna safari ndefu sana maana hatuwezi fanikiwa kwa kukutegemea mipango ya miaka mitano mitano...hatuna mikakati ya miaka mirefu ambayo inasimamiwa kisheria sasa MTU utawekezaje. Kila mwanasiasa anakuja na lake tens inaweza akawa Huyo mmoja ndani ya muda mfupi akabadilisha Sera na utaratibu wa sheria na uendeshaji.
 
Dunia haijawahi kuwa na upungufu wa mitaji wala opportunities.

Issue kubwa ni SERA, USALAMA WA MITAJI na MAZINGIRA WEZESHI.

Hivi imagine, mwekezaji akiingia mgogoro na serikali ni wapi anakimbilia kuitafuta haki yake ??

Binafsi nafikiri, mjadala mkubwa unatakiwa kuanzia kwenye chanzo.

Huwezi kupanga kuongeza idadi ya watoto wakati watoto ulionao tu wanakula JALALANI na ka siku unapambana NAO.

Na kuhusu kuongeza pato la taifa letu nadhani siyo kipaumbele pia, ndio maana tulikuwa tuna mazao ya ayoingiza pesa nyingi tu za kigeni, tumetumia nguvu kubwa, tumeyaua: Mbaazi, Korosho, Kahawa, Katani
Suala la mitaji na opportunities ni pana kidogo kuliko linavyoweza kuonekana kwa macho ya haraka haraka.

Ukweli ni kuwa kuwekeza USD 10 kwenye mradi unaoweza kuleta hasara ni hela nyingi sana kuliko kuwekeza USD million moja kwenye mradi utakaoleta faida.

Kila opportunity ina cost associated kuweza kui exploite fully hiyo opportunity iwe profitable venture na inapokuwa ya muda mfupi, muda wa kati au muda mrefu ina attraction yake na value yake kwenye investmentable consideration.

Kuhusu Mazao, sasa hivi sio kweli kuwa serikali imeyawekea vikwazo kwa kuyauza ila ni biashara inayotaka pesa nyingi katika kununua, logistics na storages na wakati huo huo soko la dunia halitoi faida kubwa kwenye nazao ya kilimo labda pawe na upungufu duniani.
 
Dunia haijawahi kuwa na upungufu wa mitaji wala opportunities.

Issue kubwa ni SERA, USALAMA WA MITAJI na MAZINGIRA WEZESHI.

Hivi imagine, mwekezaji akiingia mgogoro na serikali ni wapi anakimbilia kuitafuta haki yake ??

Binafsi nafikiri, mjadala mkubwa unatakiwa kuanzia kwenye chanzo.

Huwezi kupanga kuongeza idadi ya watoto wakati watoto ulionao tu wanakula JALALANI na ka siku unapambana NAO.

Na kuhusu kuongeza pato la taifa letu nadhani siyo kipaumbele pia, ndio maana tulikuwa tuna mazao ya ayoingiza pesa nyingi tu za kigeni, tumetumia nguvu kubwa, tumeyaua: Mbaazi, Korosho, Kahawa, Katani
Hapo ulipo agiza kinywaji ntakuja kukulipia
Asanteee


Ova
 
Uliyoyaongea ni muhimu lakini hayawezi kusaidia chochote kwa Tanzania.

Mimi nashughulika na taarifa za uwekezaji mkubwa Duniani. Na ninashiriki kwenye kuchakata taarifa za kuyapanga mataifa katika ubora wa mazingira ya uwekezaji.

Tanzania kwa kuangalia vigezo tunavyotumia kuyapanga mataifa katika mazingira bora ya uwekezaji, ipo chini sana.

Tanzania ina mazingira mabaya sana kwenye uwekezaji. Hakuna hata mwekezaji mmoja mkubwa anayeweza kuja kuwekeza Tanzania kwa sasa. Mwekezaji mkubwa wa mwisho kuja Tanzania alikuwa Dangote. Toka hapo hakuna hata mmoja aliyewekeza Tanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ningeshukuru sana kama hayo mazingira ungeyataja ili na sisi tufaidike kwa kuyaelewa mazingira hayo pingamizi.

Na hasa nyinyi wakomavu mliopo kwenye kukusanya data za uwekezaji duniani.
 
Ukiwa na mln 50 tu bank maswali mengi
Pesa umetoa wapi unaifanyia nini?
Sasa kwa mfumo huo mabilionea watatokea kweli

Ova
Mpaka mtu kukuuliza "pesa umetoa wapi?" anatakiwa kuwa na kitu ambacho kisheria kinaitwa "probable cause". Yani anatakiwa kuwa na sababu maalum au ushahidi kwamba hujapata kihalali.

Kuwa na fedha nyingi tu si kinyume cha sheria.

Na fedha nyingine zinavyopatikana ni siri za kibiashara. Nikikwambia nilivyopata unaweza kuiga ukaharibu soko langu.

Sasa, kabla ya kujibu fedha nimepata wapi, naanza kukuuliza na wewe, kwa nini unataka kujua? Una msingi gani wa kisheria kujua? Kuna kosa unanituhumu nalo? Kama lipo, kosa gani?

Tatizo hakuna fairness, wanaweza kuchukua fedha zote bila mjadala mrefu.

Conclusion, benki za Tanzania si salama.
 
Mkuu ningeshukuru sana kama hayo mazingira ungeyataja ili na sisi tufaidike kwa kuyaelewa mazingira hayo pingamizi.

Na hasa nyinyi wakomavu mliopo kwenye kukusanya data za uwekezaji duniani.
Uliyoyaongea ni muhimu lakini hayawezi kusaidia chochote kwa Tanzania.

Mimi nashughulika na taarifa za uwekezaji mkubwa Duniani. Na ninashiriki kwenye kuchakata taarifa za kuyapanga mataifa katika ubora wa mazingira ya uwekezaji.

Tanzania kwa kuangalia vigezo tunavyotumia kuyapanga mataifa katika mazingira bora ya uwekezaji, ipo chini sana.

Tanzania ina mazingira mabaya sana kwenye uwekezaji. Hakuna hata mwekezaji mmoja mkubwa anayeweza kuja kuwekeza Tanzania kwa sasa. Mwekezaji mkubwa wa mwisho kuja Tanzania alikuwa Dangote. Toka hapo hakuna hata mmoja aliyewekeza Tanzania.

Sent using Jamii Forums mobile app
Juzi nilikuwa natafuta data fulani za TRA kuhusu ukusanyaji wa kodi.

Nilikuwa na shaka sana kwamba zile data zipo, na zaidi, kama zipo, zitakuwepo kwenye website.

Nikasema ngoja nijaribu. Mgaagaa na upwa hali wali mkavu.

Kujaribu, nikakuta si tu sipati data.

Nikakuta hata website yenyewe haipo online.

Mpaka sasa siipati www.tra.go.tz

Hivi hii ndiyo website sahihi au nakosea?
 
Back
Top Bottom