Naogopa kuitwa M'MBEA

Mkuu mbona ishu simpo hiyo...mwite shemeji mwambie hufuraii anavyomfanyia mshkaji wako kugawa tunda kwa sharo ganstar wake...kama kuna tatizo na mshkaji wako upo tayari kulisukuluhisha yeshe waishi kama wanandoa wa ukweli...

Asipokusikia...mtishe kuwa utamwambia mshkaji kama mbuae na iwe mbaue tuu heri uvunje ndoa...

Kisha mtafute sharo baro wake mchimbe bonge ya mkwara kiasi kwamba ataamini sasa umewadia wakati wa kungolewa uume wake kweupeee..maana ukimtishia kuliwa tigo weshazoea wala hawaogopi....
 
Simple
Mchukue huyo rafiki yako kaa nae
Hapo .. kunyweni kuleni chekeni..
Bibie akijitokeza mwache ye ajionee mwenyewe.. then hapo hautakuwa mmbea..
Bali utakuwa wa A _town / Manyara ..karibu.
Buji,kama unampenda utamlinda,kumwambia live ni ngumu ila hii njia ya afroD iko sahihi sana!!sio umbea ila hata mungu atakupa thawabu,sithani kama utakuwa na amani maishani mwako rafiki yako huyo baadaye akakuambia HIV inammaliza na hajui kaipata wapi lakini wewe utakuwa unajua!!
 
Naamini una simu yenye uwezo wa kupata picha za mnato na video.Pata picha mnato kadhaa wakiwa wanakula bata,jitahidi uzipate kama kwa siku tatu tofauti,record na video clips ikiwezana.
Baada ya hapo wafuate mezani kwao toa tamko rasmi kwa shemeji huku sharobaro wake akisikia,ya kuwa mpango huu ukiendelea utachukua hatua ya kumjuza mume.Pia mkanye sharobaro.(Picha na video zitatumika siku shemeji akikugeuka kwa kuleta longolongo kwa mumewe (rafiki yako))
 
Buji kuwa mwangalifua kaka esp namna ya kuufikisha ujumbe kwa rafiki yako manake mwisho wa siku unaweza fanya jambo jema lakini ukaonekana mbaya na haswa kama jamaa yako kashikwa kwa huyo mwanamke,nina jamaa yangu watu walimwambia unagongewa akafikisha majina ya washkaji kwa mkewe kama yalivyo na wao kuonekana wanoko wakimwambia jamaa tewnde tukupeleke sehemu mkeo anapopigwa jamaa linagoma.Be careful bro
 
Aah Buji, umekuwa mmbea kama mimi kwa shoste wangu eeh! Nafuatilia ushauri kwa karibu, ila sidhani kama naweza kumdunda mwizi wa shostito wangu!
 
Hatua 3 za kufuata unapotatua tatizo:
1. Kemea. Ukishindwa nenda hatua inayofuata.
2. Ondoa na mkono. Ukishindwa nenda hatua inayofuata.
3. Chukia moyoni.
Fata hatua hizo hapo juu.
 
Ukisema wakiachana utakuwa mbaya,waache wakamatane wao wenyewe hata ushahidi hutakiwi lkutoa.
 
Simple
Mchukue huyo rafiki yako kaa nae
Hapo .. kunyweni kuleni chekeni..
Bibie akijitokeza mwache ye ajionee mwenyewe.. then hapo hautakuwa mmbea..
Bali utakuwa wa A _town / Manyara ..karibu.
Huo ndio ushauri murua, usimwambie ila panga mipango ajionee mwenyewe
 
Rafiki yangu alifunga ndoa miezi miwili iliyopita na mchumba wake wa siku nyingi.
Kutokana na ukali wa foleni huwa ninakuwepo maeneo ya mjini nikipata moja baridi, moja vuguvugu na nyingine moto.

Kila siku huwa namuona huyu shemeji yangu akiwana na kasharobaro kamoja kenye kuvaa milegezo huku wakinyweshana pombe, denda kidogo na kutomasana kwa fujo.

Natamani kumwambia mumewe licha ya kuwa naumia moyoni.
Najua nikimwambia mumewe nitaharibu uhusiano wao, na siku wakipatana wataniita M'MBEA.

JE NIFANYEJE?


Unauliza ufanyeje wakati usha mwaga umbea JF? sasa kama si umbea huu ni nini? Unanchekesha!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom