Naogopa kifo

Naogopa kifo

Habari wana JF,

Mimi naogopa kifo sana,maana ukijiangalia ki sawa sawa huwezi amini kama siku moja utazikwa na kulaliwa na kifusi cha udongo.

Kwa kweli najuta sijui kwanini nilizaliwa? Nawakati unajua kuwa nitafariki na kuzikwa?


Eeee Mungu mimi naomba nisife! Nakuomba sana Mungu uniepushe na hili.

Mimi naendelea kuomba, Leo nimejifungia siku ya tatu ndani ya chumba changu naomba kufa na kupona, sili chakula wala nini namlilia Mungu mpaka nikwepe kifo.

Jamani epukeni dhambi tuungane pamoja.

Siku njema.
Wanasema tu kuwa ombeni nanyi mtapewa ila sio kweli. Hivyo haya maombi yako yatasubiri sanaaa
 
mshana jr , kwa mtu anayemwamini Kristo haogopi kifo kamwe. Katika waanzilishi na waasisi wote niliowahi kuwasikia ni Yesu pekee ndie alieshinda kifo. Na kila anayemwamini kifo ni njia ya kubadili tu kutoka mwili uharibikao na kuvaa mwili wa milele usiokufa na usiokua na maumivu wala magonjwa. Ni ndani ya Kristo tu, tunaweza kuongea habari za kifo kwa ujasiri.

yalimo, hakuna haja ya kuogopa kifo, japo sio jambo jepesi. Maadam umezaliwa, kifo hakiepukiki, weka uhusiano wako vizuri na Mungu wako, hapo utakua na tumaini baada ya maisha ya hapa duniani. Hata kama ukiishi miaka 1000, utakufa tu.
Barikiwa sana Samaritan
 
Kuna wakati utakiomba siku za maisha yetu ni miaka 70 Kama tuna nguvu ni 80
Wewe omba kifo kizuri
 
Yamkini nimeshaamini hakika Mungu ataniwezesha! ntaishi tu hakuna kinachoshindikana mbele za Mungu. hakika sitakufa ntaishi hata peponi.
Nakuogopea usije anza kuokota makopo
 
Religion is just a feeling good therapy

Ukitaka faraja hata kama ni ya uongo,utapata

Kifo ndio mwisho wa mwanadamu

Hadithi za Mbingu na Motoni ni kujifariji
Ok ngoja siku itapokunata....ndo utapojua kama ni therapy ama n8 hadithi....
 
Pole ndugu kwa uwoga huo....jitahidi kuushinda kumbuka kuwa hapa upo vitani ni lazima upambane death is must...and its very painfully...tena super pain..na kuoza kuoza ni kweli, kunuka ni kweli... Mengine pia ni kweli...kama kuogopwa nk yapo..

Cha kufanya kwasasa Pigania moments ulionayo katika uwepo wako ili hio siku ukivuta iwe memories kwa walimwengu kuwa ulifanya kitu duniani, kama ugunduzi utakao rahisha maisha, au maoni yatakayo fanya walimwengu wa starehe na wawe na amani na salama..panda miti mingi ya matunda... Tunza mazingira... Nk..

Kujifungia ndani sio solutions
 
MIMI NILIWAHI KUPIGWA NUSU KAPUTI KWA AJILI YA USINGIZI.SIKUHISI LOLOTE.HAKIKA KAMA KIFO NI HIVYO WALA HAKUNA SHIDA YOYOTE MAANA NITAKUWA SIPO!!!
 
wala usiogope,maana ukifa wala hutajua chochote kinachoondelea juu yaki;Ni kama vile unavyozaliwa kwa siku ya kwanza huelewi lolote linaloendelea,na kufa ni hivyo hivyo sema ukifa ogani zote mwilini zako zinakoma kufanya kazi
hii nayo balaaa
 
wala usiogope,maana ukifa wala hutajua chochote kinachoondelea juu yaki;Ni kama vile unavyozaliwa kwa siku ya kwanza huelewi lolote linaloendelea,na kufa ni hivyo hivyo sema ukifa ogani zote mwilini zako zinakoma kufanya kazi
balaaa
 
"Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake za kuishi si nyingi,naye hujaa taabu,AYUBU 14:1
 
Hata Mimi naogopa sana kufukiwa na hicho kifusi nahisi kama nitakuwa nahisi vile. Natamani hata nikifa wanitupe porini huko.
 
Back
Top Bottom