Nani mwimbaji bora wa Gospo wa mda wote Tanzania?

Mimi nafikiri kila mtu atatoa opinion yake kutegemea na aina ya muziki unaomgusa....anayependa kitimtim na hekaheka anaweza kuangukia kwa akina Rose. Anayependa muziki wa kusifu na kuabudu anaweza kurudi kwa akina Muhone na Shusho (and the like)...
 
Rose Muhando? Bahati Bukuku? Christina Shusho? Bonny Mwaitege? Upendo Nkone? Jennifer Mgendi? Beatrice Muhone? Ambwene Mwasongwe? Martha Mwaipaja? Flora Mbasha?.............
Kwa wataalamu
wa muziki
Huyu ni mwimbaji mzuri hasa.quality=100%.vocal range=100%
good speed=100%.timing=100%.accurate articulation=100%
microphone position=100%.convey emotions=100%
(hii husababisha wrinkles wakati anavuta hisia,hapa si wote mtaelewa'')
Pia ana discipline
ila
si lazima afanye vizuri sokoni.
 
Jamani Acheni Ushabiki, huwa mnasikiliza izo nyimbo? ni zipi zenye upako zaidi? maana huwez kuwa na nyimbo nzr kama ww mwnyewe haupo vzr kiroho, sawa?
 

  • Watu8 kumbe na wewe umo, kiukweli nyimbo zile zilikuwa zinakosha, unajua zilikuwa zinakosha kiasi kwamba kwa wakristo wachanga kama sisi unakuta unapata mafundisho na visa za kwenye biblia.

    Ila Shusho na Upendo Nkone ni kiboka maana pamoja na kwamba hawaimbi zile nyimbo za kutumbuiza (entertaining) za kuruka huku na kule lakini bado wakiimba unawasikiliza mpaka mwisho​



Na hapo ndio Shusho anaponimaliza, hatoki jasho! Vijana wa mjini wanasema "mdogo, mdogo" lakini ujumbe unakuingia kumoyo. Soul soothing....
 
Jamani Acheni Ushabiki, huwa mnasikiliza izo nyimbo? ni zipi zenye upako zaidi? maana huwez kuwa na nyimbo nzr kama ww mwnyewe haupo vzr kiroho, sawa?
Kha! Mkuu hebu tuache wenzako. Upako hatuna basi hata kufurahia nyimbo na kukiri kuwa kwa hakika wenzetu hawa wana upako nako tushindwe. Upako ungekuwa lotion walahi kila mtu angekuwa nao:wink2:
 
Na hapo ndio Shusho anaponimaliza, hatoki jasho! Vijana wa mjini wanasema "mdogo, mdogo" lakini ujumbe unakuingia kumoyo. Soul soothing....
Aisee ni kweli maana wengine kweli wanaambia na wana pumzi hasa ya kuimba lakini ile nyongeza ya kucheza nayo inawafanya wanoge ila huyu yeye ni mdogomdogo kama unavyosema lakini naye yumo
 
Huyo Ambwene Mwasongwe ana wimbo wake mmoja unaitwa "misuli ya imani",aisee ulinitoa machozi sebuleni mbele ya wife nilipoona video yake,sijui alifikiria nini huyu jamaa una hisia kali sana, ktk nyimbo za injili nilizowahi kuzisikiliza huu umenigusa na nimejiapiza nikiwa mgeni kwa mtu ukipigwa nikiwa nae nitafanya kila njia nitoke nje kwa muda,sasa hata audio tu kuusikiliza unanisumbua sana lazima nitokwe machozi sijajua kilichonipata.
 
Christina Shusho is the best Gospel singer ever seen in Tanzania and the Great Lakes region
 
Vile vile ile kwaya ya kijitonyama upendo group naipenda mno kuna bwana mmoja nafkri ndo main vocalist ila sikuizi wamepoteana ila albam yao ina dumu sana tatzo njia tu ya kurekod ndo ilikua ya kizamani pengine wangepata vifaa vya kisasa mbona wangewaacha wale joyouz celebration wa SA maana ndo kwaya nayoipenda zaidi

Kiukweli najivunia kuwa mkristo ni raha mno kuwa ndani ya huyu Yesu
 
Huyu mama naye huwa ananikosha mno...

Nilimfahamu kupitia wimbo wake mmoja anaelezea kuwa pasipo maono watu wanaangamia...

Baadaye akatoa wimbo wake wa "Yesu ni wa rehema"...
Mie huyo mama alinikamata na ule wimbo wake unaoenda kwa jina la usifurahi ndugu yangu... ujue kwa maombi yako mimi nitasimama tena..
 
New Life Band, Ulyankulu Barabara ya 13...

Hao wengine wote uliowataja ni wafanyabiashara nyuma ya nyimbo za injili...

These are the best, jamani New life band imekwisha wamebaki watatu tu wale wa zamani, nilikuwa nikiwaona sana kny semina ya mwakasege wakiongoza sifa ila sidhani kama hivi karibuni wametoa
 
Walianza kupoteza uelekeo walipoanza kujitenga kina Amon na Upendo...

Sijawasikia muda mrefu kwenye pilika za kutoa albamu...

These are the best, jamani New life band imekwisha wamebaki watatu tu wale wa zamani, nilikuwa nikiwaona sana kny semina ya mwakasege wakiongoza sifa ila sidhani kama hivi karibuni wametoa
 
St. Joseph Arusha ni hatari, Watu8 amefunga orodha, ila kuna Ulyankulu wengine inaitwa mapigano kama sikosei, waliimba Mwenye Mamlaka. Hawa watu walikua wanaimba neno ndio maana nyimbo zao hazitakaa zichuje wala kuchosha kusikiliza.

Kuna Nkinga Christian Choir na Kilimanjaro Revival nao wanajitahidi.

Kwa ufupi, iwe ni kwaya au mwimbaji binafsi au kikundi, wakiimba neno na sio hizi nyimbo za maneno ya msimu, utagusa watu tu kwa nja moja ama nyingine.

Hapo ongezea na kimara lutheran....katika njia ya injili...na mabibo lutheran...sauti..aisee izi kwaya mbili zilikuwa moto..
 
Umeongea kweli,sijawahi kuona Kama ulyankulu barabara ya 13,nyimbo zao zinagusa,wamevaa kiheshima,nyimbo za nyingi zinaendana na maandiko,nawakubali Sana aisee

Napenda stail yao ya live... Hakuna kurukaruka lkn ujumbe ni full bible... Hakuna utamu wa Yesu nk hapo... Wapo fresh sana
 
Back
Top Bottom